Tangia jana katika mitaa ya Jiji la Arusha na viunga vyake, yametapakaa mabandiko ya kuhamasisha wananchi kushiriki kwa wingi katika Uchaguzi zw Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Desemba 14, 2014.
Moja ya mabandiko hayo ambayo mengine huwekwa kama stika kwenye magari yana heading kubwa "ANATAFUTWA" halafu chini yake kuna picha kubwa ya Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema ikifuatiwa na maelezo ya namna uchaguzi huo utakavyofanyika kuanzia kuchukua fomu kwa wagombea, kujiandikisha wapigakura na hatimaye kupiga kura.
Tathmini yangu ya haraka imeonesha mbunifu wa "tangazo" hili ambalo liko kwenye standard ya juu in terms of quality ameweza kufikisha ujumbe tarajiwa kwasababu wananchi wengi wanashtuka kuona Mbunge Jijini wao ANATAFUTWA na hivyo kujikuta wakivutika kusoma kilichomo. Mbunifu huyu ameweza kusoma vyema uvivu wa watanzania na kupata mahali pa kuwakamata vizuri.
Tafiti yangu imenijuza pia kuwa ubunifu huu wa watu wa Chadema umefikiwa baada ya kugundua wanachodai kuwa ni hila za CCM na Serekali yake kuficha baadhi ya taarifa muhimu kwa umma kuhusu uchaguzi huo ili wao waishie kujuzana na wanaCCM pekee kama moja ya mbinu za kujaribu kujiokoa na uwezekano mkubwa wa kukataliwa na wananchi katika uchaguzi huu. Mambo mengi yanaonekana kwenda kibubububu wakati tarehe zimeshafika..!
View attachment 203489Mh Lema akiwa kwenye safari zake mitaa ya Jii la Arusha. Unaweza kuona gari yake inalo bandiko hilo pia
View attachment 203491bandiko lenyewe hili hapa