Watawala wajinga huamini silaha ni nyenzo ya kazi kwa ajili ya kuogopesha, katika hali hiyo hiyo ya ukungu katika ubongo wao hudhani magereza ni tishio ambalo hakuna mwanadamu yuko tayari kukubali kwenda kuishi kwa amani na kwa furaha. Msimamo huu wa serikali dhalimu zote duniani na kwa kuwatumia polisi na vyombo vya usalama katika nchi hukwama pale wanapowapata wanadamu kama mahatima gandhi, madela, steve beko na sasa lema wa tanzania na wengineo wengi. Mheshimiwa godbless lema kawambia serikali ya tanzania na vyombo vyake vya usalama kuwa kama anapata nafasi ya kuchagua kifo na kuishi, ili watanzania na wanaarusha wakombolewa atachagua kifo, kama anapata nafasi ya kuchagua kuishi jela maisha yake yote ili wananchi wake wapate amani na uhuru wa kweli atachagua kwenda magereza na amefanya hivyo kwa vitendo.
Sote tunatambua kuwa bunduki za polishi, mbwa wa polisi, maji washa, mabomu ya machozi yanaletwa na kutumiwa kwa ajili ya ulinzi na usalama wa wananchi na kuwaadhibu wale walioshindwa kukidhi matakwa ya amani kwa tafsiri ya katiba si vinginevyo.
Magereza yyanajengwa kuwatunza wakosaji sasa inapotokea vyombo hivi vinakuwa tishia toto serikali na vyombo vyake vya ulinzi wamejikwaa na kuangukia pua. Tunayokila sababu ya kujua kuwa watu wengi walioko kule wengi wao wako kule kwa sababu ya kukithi matakwa ya watawala au watu waliokaribu na watawala au watu walikwisha tambuliwa kuwa ni walala hoi hawana mtetezi na muono huu ndiyo unakamilisha dhana ya tisha toto ambayo hutumiwa na polishi na serikali .
Ipo siku watu hawa wote watakuwa na moyo wa lema magereza hayatatosha, askari hawatatosha, risasi hazitatosha wala magari ya maji washa. Polisi mnalijua hilo na kama hamlijui tazameni misri, tunisia, na sasa yanayotokea yemen na syria
Sote tunatambua kuwa bunduki za polishi, mbwa wa polisi, maji washa, mabomu ya machozi yanaletwa na kutumiwa kwa ajili ya ulinzi na usalama wa wananchi na kuwaadhibu wale walioshindwa kukidhi matakwa ya amani kwa tafsiri ya katiba si vinginevyo.
Magereza yyanajengwa kuwatunza wakosaji sasa inapotokea vyombo hivi vinakuwa tishia toto serikali na vyombo vyake vya ulinzi wamejikwaa na kuangukia pua. Tunayokila sababu ya kujua kuwa watu wengi walioko kule wengi wao wako kule kwa sababu ya kukithi matakwa ya watawala au watu waliokaribu na watawala au watu walikwisha tambuliwa kuwa ni walala hoi hawana mtetezi na muono huu ndiyo unakamilisha dhana ya tisha toto ambayo hutumiwa na polishi na serikali .
Ipo siku watu hawa wote watakuwa na moyo wa lema magereza hayatatosha, askari hawatatosha, risasi hazitatosha wala magari ya maji washa. Polisi mnalijua hilo na kama hamlijui tazameni misri, tunisia, na sasa yanayotokea yemen na syria