Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) ameendeleza msimamo wake wa kutokumtambua Meya wa Jiji la Arusha, safari hii akiibua malumbano mbele ya wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya kulumbana na Naibu Meya wa Jiji hilo, Bashiri Msangi.
Malumbano hayo yalitokea wakati wabunge hao wa EAC walipokwenda kupanda miti kwenye shule ya msingi ya Nadosoito, Arusha. Wabunge hao waliongozwa na Mbunge kutoka Tanzania, Kate Kamba, akimwakilisha Spika wa Bunge hilo, Abdurahin Abdi, ambaye alishindwa kuhudhuria kutokana na majukumu mengine ya kiofisi.
Mara baada ya Lema kupewa nafasi ya kuzungumza alianza kwa kusema kuwa hamtambui meya wa Jiji hilo kwa kuwa hakuchaguliwa kwa mujibu wa sheria zilizopo. Wageni wengine waalikwa waliokuwa katika hafla hiyo ni madiwani, maofisa kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha, wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na walimu na wanafunzi.
Meya wa Manispaa ya Arusha, Gaudence Lyimo, hakuhudhuria hafla hiyo na badala yake alimtuma Naibu Meya, Bashiri Msangi, ambaye ni diwani wa Kata ya Daraja Mbili kumwakilisha.
"Napenda kuwaelezeni kwamba sitambui uwepo wa meya katika hafla hii…suala la umeya hapa Arusha tuna mgogoro nalo, hakuchaguliwa na yuko kinyume cha taratibu na sheria," alisema Lema. Akizungumza baada ya shughuli ya kupanda miti, Lema alisema alitoa kauli hiyo mbele ya wabunge wa EAC ili kufikisha suala la mgogoro wa umeya kwa jumuiya hiyo."Nilitaka kufikisha suala hili mbele ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili watambue kwamba hapa Arusha watu wananyimwa haki zao za kidemokrasia," alisema.
Naibu Meya, Msangi alipopata nafasi ya kuzungumza, naye alirusha madongo kwa Lema akisema anamtambua meya kwani alichaguliwa kihalali. "Mimi hapa hatuvutani kuhusu meya wa Arusha kwa sababu amechaguliwa kwa mujibu wa sheria zilizopo," alisema na kuongeza: "Sisi ni timu moja, hatutofautiani na mbunge wetu na ndio maana yupo hapa."
Lakini akizungumza na NIPASHE, baada ya kulipuliwa na Lema, Msangi alisema kitendo alichokifanya Lema ni cha hatari sana.
"Kauli ya Lema ni hatari sana, na hasa imetolewa mbele ya wageni…na hii inaonyesha jinsi asivyo na mapenzi na nchi yake," alisema.
Akitoa shukrani baada ya kumalizika kupanda miti, diwani wa Kata ya Terati, Julius Sekayani, alisema wanachohitaji wananchi wakati huu ni maendeleo na sio siasa.
"Suala la uchaguzi limeisha, wananchi wetu wanataka kuona kazi sasa na sio siasa, binafsi nitakuwa sina adabu nikisema simtambui meya kwani alichaguliwa kihalali na kwa mujibu wa sheria za nchi hii, zinazosimamiwa na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa," alisema na kuongeza:
"Naomba waheshimiwa wabunge waelewe kwamba wakati wa siasa umepita na sasa ni muda wa kuchapa kazi."
Source: Nipashe 24th May 2011
My take: kwenye red - CDM waanikeni hao kila kona ya dunia wakose hata sehemu za kuuza sura!
Malumbano hayo yalitokea wakati wabunge hao wa EAC walipokwenda kupanda miti kwenye shule ya msingi ya Nadosoito, Arusha. Wabunge hao waliongozwa na Mbunge kutoka Tanzania, Kate Kamba, akimwakilisha Spika wa Bunge hilo, Abdurahin Abdi, ambaye alishindwa kuhudhuria kutokana na majukumu mengine ya kiofisi.
Mara baada ya Lema kupewa nafasi ya kuzungumza alianza kwa kusema kuwa hamtambui meya wa Jiji hilo kwa kuwa hakuchaguliwa kwa mujibu wa sheria zilizopo. Wageni wengine waalikwa waliokuwa katika hafla hiyo ni madiwani, maofisa kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha, wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na walimu na wanafunzi.
Meya wa Manispaa ya Arusha, Gaudence Lyimo, hakuhudhuria hafla hiyo na badala yake alimtuma Naibu Meya, Bashiri Msangi, ambaye ni diwani wa Kata ya Daraja Mbili kumwakilisha.
"Napenda kuwaelezeni kwamba sitambui uwepo wa meya katika hafla hii…suala la umeya hapa Arusha tuna mgogoro nalo, hakuchaguliwa na yuko kinyume cha taratibu na sheria," alisema Lema. Akizungumza baada ya shughuli ya kupanda miti, Lema alisema alitoa kauli hiyo mbele ya wabunge wa EAC ili kufikisha suala la mgogoro wa umeya kwa jumuiya hiyo."Nilitaka kufikisha suala hili mbele ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili watambue kwamba hapa Arusha watu wananyimwa haki zao za kidemokrasia," alisema.
Naibu Meya, Msangi alipopata nafasi ya kuzungumza, naye alirusha madongo kwa Lema akisema anamtambua meya kwani alichaguliwa kihalali. "Mimi hapa hatuvutani kuhusu meya wa Arusha kwa sababu amechaguliwa kwa mujibu wa sheria zilizopo," alisema na kuongeza: "Sisi ni timu moja, hatutofautiani na mbunge wetu na ndio maana yupo hapa."
Lakini akizungumza na NIPASHE, baada ya kulipuliwa na Lema, Msangi alisema kitendo alichokifanya Lema ni cha hatari sana.
"Kauli ya Lema ni hatari sana, na hasa imetolewa mbele ya wageni…na hii inaonyesha jinsi asivyo na mapenzi na nchi yake," alisema.
Akitoa shukrani baada ya kumalizika kupanda miti, diwani wa Kata ya Terati, Julius Sekayani, alisema wanachohitaji wananchi wakati huu ni maendeleo na sio siasa.
"Suala la uchaguzi limeisha, wananchi wetu wanataka kuona kazi sasa na sio siasa, binafsi nitakuwa sina adabu nikisema simtambui meya kwani alichaguliwa kihalali na kwa mujibu wa sheria za nchi hii, zinazosimamiwa na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa," alisema na kuongeza:
"Naomba waheshimiwa wabunge waelewe kwamba wakati wa siasa umepita na sasa ni muda wa kuchapa kazi."
Source: Nipashe 24th May 2011
My take: kwenye red - CDM waanikeni hao kila kona ya dunia wakose hata sehemu za kuuza sura!