Lazima Lowassa ashitakiwe kwa Ufisadi!!

Acha atutembeze katika barabara ya ukweli
Hawezi kufungwa tupo tutamdhamini.

Ukweli Upo na umekuwa ukiishi katika fikra zetu.
Ukitaka asisemwe Basi aachie ofisi ya umma.

Alipo sasa yeye ni waumma.
Lazima asemwe.
Bora ukachunge ng'ombe kuliko kudharau Mamlaka. Utaishia jela bure!
 
Acha ujinga wewe, nenda mahakamani haraka sana acha kutafuta kick. Alafu we mwandishi kwa kukushauli tu, rudi shule ukatoe ujinga kwani elimu bure saizi.
 
Acha ujinga wewe, nenda mahakamani haraka sana acha kutafuta kick. Alafu we mwandishi kwa kukushauli tu, rudi shule ukatoe ujinga kwani elimu bure saizi.
Umekuwa mjinga kama jina lako "APUTWIKE". Endelea na ujinga wako!!
 
ukiyaleta ya Lowasa ni sawa na kuyaleta ya nyumba za serikali,kivuko cha bagamoyo,Escrow na mengine mengi.kumshtaki Lowasa ni sawa na kuishitaki serikali iliyopo madarakani
 
Kwa nini sasa wanaendelea kumsakama?
Hoja kama hizi zinakupunguzia sifa japo unajiona kama unaonekana jasiri na mabavicha wenzako
Mahakamani si pa kumuombea mtu kupelekwa awe na ushahidi au la,lakini kwa akili za Bavicha hili unalitaka
Na subiri litakuwa soon,na akifungwa mtu wako usije kusema mahakama imenunuliwa
 
Magu mwenyewe anasema anadili na ufisadi wa miaka mitano iliyopita, je ndani ya hiyo miaka Lowasa alihusika na nini?

Kama kuna ushahidi kesi jinai haina mipaka ya muda (limitation of time). Hata EPA inaweza kuletwa. Wanaharakati mmelala?
 
Mweeeeeeee!

Unataka wajitumbue wenyewe siyo???

Kwani hukumsikia mwenyewe anasema kuwa "Ni lipi alilolifanya Mweshimiwa Raisi hakulijua???"

Mi naomba walipotezee tu maana hata ubora na viwango vya Anko Magu hatutaviona tena. Na kwa hakika ni heri wakaruhusu mikutano na maandamano kuliko kufungulia hiyo kesi.

Wangu mtizamo tu huo lakini....!
 
Gangongine hebu soma hii uje tena na mitusi yako!!

Nakushukuru mheshimiwa Spika kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii. Lakini la pili nimpongeze Dr. Harrison Mwakyembe Mwenyekiti wa Kamati teule,kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri sana.Kwa kazi nzuri kwa maoni yao na wameiwasilisha vizuri.Lakini Mheshimiwa Spika, nimesimama kuweka kwenye Kumbukumbu kutokuridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa.

Mhesimiwa Dr. Harrison Mwakyembe ni mwanasheria tena daktari alikuwa anafundisha wanafunzi Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni Natural justice. Wewe pia Mheshimiwa Spika ni Mwanasheria, unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba katika Kamati Teule, imesikiliza watu wengine wote, pamoja na waliowaita minong’ono ya mitaani. Wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja katika watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja!

Mheshimiwa Spika. Nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya bunge mpaka ofisini kwangu hata wangeniita ningeenda kwa mguu kama hamna gari. Na nilikuwa tayari kufanya hivyo.Hawa ni watu makini sana, siwezi kuamini kwamba wanaweza kufanya Oversight kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga, walisema Waziri Mkuu ilikuwa hivi, kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza, Waziri Mkuu wanasema ulitoa dokezo hili ni sawa sawa ni kweli? Kulikuwa na shida gani kwa mfano Mheshimiwa Spika, kufuata utaratibu wa Westminster kuthibitisha hapo unaposema, wenye Richmond nifulani uka- table Record na ushahidi kwamba ni fulani.

Mheshimiwa Spika Taifa letu ni taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa Demokrasia pa kubwa katika nchi yetu pote, hapa ndipo penyewe. Kama katika chombo hiki haki haitaonekana kutendendeka, Mheshimiwa Spika nchi haitakwenda vizuri.

Hapa ndipo tunategemewa kuonyesha umakini, umahiri wetu katika mambo ya Demokrasia. Kwa hiyo nilichofanyiwa Mheshimiwa Spika napenda kuweka kumbukumbu sahihi…sawa. Kwamba naona si sahihi, na nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana na nimeonewa sana katika hili. Maana zimechukuliwa tuhuma zikaja kuelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo, mimi sijaulizwa. Kulikuwa na shida gani kuniuliza. Kwa nini muamini minong’ono ya mitaani kuliko maelezo yangu?

Sisi wote hapa ni wanasiasa, tukianza kuamini minong’ono ya mitaani, niambieni mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi… Tume wamepewa muda wa kutosha kabisa, lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.

Lakini mheshimiwa Spika, hata pale uliponinong’oneza ukaniambia “una ushahidi wowote”? Nilikupa ushahidi huo wa maandishi. Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka Ofisi ya Waziri Mkuu, hata mmoja! Lakini kitabu cha Majedwali kimejaa majedwali meengi pamoja na Magazeti mpaka ya Udaku, lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika. Mimi naamini ingekuwa ni heshima wangeliweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii na hii na hii. Mimi nadhani ingejengwa hoja. Lakini kujenga hoja na kuja hapa bungeni, tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki, amefanya hiki bila kumsikiliza, nachelea kuuliza, hivi watu wa chini itakuwaje?

Lakini Mheshimiwa Spika nimetafakari kwa makini sana jambo hili, nikajiuliza, hivi hasa kulikoni. Mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu, wenye heshima zao. Mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo, kulikoni?

Mimi nadhani, they have a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Nadhani tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndiye amefanya haya, ionekane Waziri Mkuu amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe. Mheshimiwa Spika. Nimetafakari sana, kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya serikali yangu, nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.

Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa, kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji lakini na kutokukubaliana na utaratibu uliotumika kusema uongo ndani ya bunge wa kunisingizia.

Mheshimiwa Spika nitumie nafasi hii kumshukuru sana Rais kwa heshima aliyonipa ya kutumikia nchi hii kwa Uwaziri Mkuu kwa miaka miwili, namshukuru sana mheshimiwa Rais. Nakushukuru wewe, nawashukuru Mawaziri na Manaibu Mawaziri, nawashukuru waheshimiwa Wabunge, na wanachama wa CCM tuliosimamia Ilani ya Uchaguzi ya Chama chama Mapinduzi. Baada kusema hayo nakushukuru Mheshimwa.
Kama ingekuwa hahusiki kwa nini ajiuzulu? Mbona Pinda kuna wakati alipewa shinikizo lakini hakujiuzulu? Alikimbilia "UWAZIRI MKUU" kama namna ya kufuta aibu ionekane ameonewa. Asingeweza kuacha UWAZIRI MKUU bila sababu ya msingi. Halafu huyo wa juu aliyemuagiza mbona hamsemi? Acheni mahaba, HANSARD iko wazi inaeleza RICHMOND SAGA kwa mapana yake!
 
Gangongine huu mchezo hauhitaji hasira.Kwenye hotuba hiyo ya Lowassa kuna maswali yanahitaji majibu lakini mpaka sasa hamtaki kutujibu.

  1. Spika alipewa ushahidi na Lowassa ili ampe Mwakyembe na Mwakyembe alipewa huo ushahidi lakini hakuutumia. Kwa nini?
  2. Kina Mwakyembe walisafiri hadi Marekani kuhoji mashahidi lakini hawakumhoji mtuhumiwa aliyekuwa na ofisi yake mita 200 toka Ofisi za bunge. Kwa nini?
  3. Sakata la Richmond mpaka Lowassa anajiuzulu taifa lilikuwa limepata hasara kiasi gani? Kwa nini haisemwi ni hasara kiasi gani imepatikana?
  1. Mitambo ile iliyoletwa na Richmond ndiyo hiyo hiyo iliuzwa kwa Dowans kisha Dowans wakaiuza kwa Symbion ambao nao wanaitumia kuzalisha umeme wanaouziwa Tanesco. Uharamu wa Richmond ulikuwa ni mitambo au ulikuwa nini hasa?
 
Afadhali sasa mahakama ya mafisadi imeshaanza kufanya kazi. Ila nimesikitika sana mtu wa kwanza kushitakiwa siyo Lowassa.
 
Afadhali sasa mahakama ya mafisadi imeshaanza kufanya kazi. Ila nimesikitika sana mtu wa kwanza kushitakiwa siyo Lowassa.

Kikwete aliwackear wote Chenge na Lowassa, akasema hakuna pesa zilizopotea. Huwezi kumushitaki Lowassa bila ya Kikwete. Kikwazo kipo hapo.
 
Kikwete aliwackear wote Chenge na Lowassa, akasema hakuna pesa zilizopotea. Huwezi kumushitaki Lowassa bila ya Kikwete. Kikwazo kipo hapo.
Nimeamini maneno yako maana leo Gazeti la chama chao limeandika kwamba mahakama ya mafisadi imekosa kesi. Inakosaje kesi wakati walituambia hiyo mahakama ya Mafisadi ikianza Lowassa atakiona cha mtema kuni!
 
Kama wana kesi na Ushahidi wa kutosha, Wangesubiri nini hadi leo kumkamata na Kumshitaki? Hamtumii akili zenu? Lowassa ameshaingia Upinzani kwahyo serikali hawana sababu yoyote ya kumlinda kwa sababu sio mwenzao tena, Kwanini Wamemuacha? Unazan wanamwogopa?Kwa lipi?? Fikiri kabla ya kupost, Nyambaf
 
MANENO YA MWAKYEMBE ALIPO HOJIWA KUHUSU SAKATA LA RICHMOND
July 21 2016 Waziri wa katiba na sheria, Dk. Harrison Mwakyembe alikuwa akihojiwa katika kipindi cha Clouds 360 cha clouds TV na kujibu maswali mbalimbali yanayohusu katiba na sheria na hili sakata la Richmond likagusiwa.

Mtangazaji wa clouds TV, Hudson Kamoga alimuuliza Waziri mwakyembe kuhusiana na sakata la Richmond wakati akiwa mwenyekiti wa kamati iliyokuwa inachunguza sakata hilo ambapo walikuja na ripoti ambayo ilipelekea aliyekuwa Waziri mkuu kwa wakati huo, Edward Lowassa kujiuzulu. Hudson ametaka kujua kama kuna mambo ambayo watanzania hawakuyajua kuhusu sakata la Richmond

Waziri Mwakyembe amesema ….>>>‘kesi ya Richmond tuliifanya kwa roho safi na kwa kupiga magoti kwa Mungu na tuliifanya haki kwa kila mtu tulichoamua hata tuamue kesho asubuhi nirudie tena hata koma haitabadilika itakuwa vilevile na mimi nitafurahi sana’

>>>’chini ya kanuni tunaruhusiwa kuifufua tena Richmond ili ichunguzwe upya na ninaaapa wanaweza wote wakahama wakaniacha peke yangu na uhakika mimi mwenyewe nilichonacho nitajenga hoja sidhani kama kuna mtu hata mmoja atasalimika kwenda jela‘
Huyu si ndio waziri wa sheria aliyesimamia uanzishwaji wa mahakama ya mafisadi ?

Mkuu Mwakyembe nakung'ata sikio , usipompeleka lowassa mahakamani iko siku utapelekwa wewe kwa upotoshaji wako , abhajanga abho abikusyobha , Lwako gwimwene nu bhutunghulu bwako .
 
Back
Top Bottom