Ni kweli kuwa tarehe 17 kuna wano apishwa kuwa Advocates ila ukweli kwamba wengi wa wanaoapishwa hawajatokea hiyo law school bali ni kupitia Bar exam. Toka shulu hiyo ya sheria imeanzishwa matokeo ya madarasa manne yameshatoka ila idadi ya waliofaulu na kuapishwa haijafika hata 150 ingawa kila darasa lilikuwa na wastani wa wanafunzi 250.Hatimaye kilio cha muda mrefu cha wanachuo wa the Law school of TZ kujua hatima yao kimefikia ukingoni. Zaidi ya mawakili 300 wanatarajia kuapishwa hivi karibuni...
Nawatikia kila la heri na mafanikio ktk uadivoketi wenu.
Ni kweli kuwa tarehe 17 kuna wano apishwa kuwa Advocates ila ukweli kwamba wengi wa wanaoapishwa hawajatokea hiyo law school bali ni kupitia Bar exam. Toka shulu hiyo ya sheria imeanzishwa matokeo ya madarasa manne yameshatoka ila idadi ya waliofaulu na kuapishwa haijafika hata 150 ingawa kila darasa lilikuwa na wastani wa wanafunzi 250.
Am happy kuwa fani itapata ushindani
Nasikia waajiriwa wa Serikali waliomaliza Law School wamekataliwa kuapishwa!
Ni kweli kabisa, serikali inasema watakuwa wanafaidi pande zote mbili. Either unakuwa muajiriwa serikalini au wakili binafsi. Na sio vyote..
Jamaa wamekuwa disappointed sana.
ukiwa wakili wa serikali, afisa usuluhishi au mwamuzi, hakimu huwezi kuapishwa kuwa wakili wa kujitegemea. (sijui ni conflict of interest au nini)
Mh. Buchanan nilidhani wewe ungeweza kutoa mwanga zaidi kwenye hili lakini naona na wewe unazama kwenye huu mtumbwi.
Kweli nimezama ndugu, maana akina CJ wanatumia logic badala ya Sheria ambayo haiwakatazi watumishi wa Serikali kuwa Mawakili wa Kujitegemea! Kama ni conflict of interest mbona ma-lectures (Mgongo Fimbo, Shivji by then, Dr Lamwai, Dr Sengodo Mvungi, just to mention few) ni Mawakili wa Kujitegemea? Hapa hakuna double standard kweli?
Kwa hiyo wafanyabiashara hawajaapishwa? Au wao hawafaidi sehemu mbili? Pia, kwani suala ni kufaidi au kuhudumia jamii? Mbona Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na ma-lectures almost wote ni mawakili? Akina Dr Mwakyembe ni mawakili huku pia ni mawaziri! There must be something wrong somewhere!
Inawezekana pia ni strategy ya kutaka kudhibiti utitiri wa mawakili binafsi, wametafuta namna ya kupunguza idadi. Manake hao mawakili wapya 350 wote wana muhuri binafsi. Sioni sababu ya kuzuia watumishi wa umma kutokuwa mawakili binafsi. Mbona madokta wengi wa serikalini wana dispensari zao binafsi na hawajazuiliwa??? huu ni uonevu tu.
Sasa kama ni kudhibiti idadi ya mawakili wa kujitegemea mbona CJ analalamika kuwa ratio ya mawakili hao kwa population ni 1:36,000 kwa Tanzania ambayo ni ndogo sana ukilinganisha Kenya 1:3,500 na Uganda 1:6,000? Hili suala lisiangaliwe kibinafsi zaidi, tuangalie maslahi ya nchi zaidi!
Tanzania tupo tofauti saana na wenzetu EA. Hata ukiangalia uwiano kati ya Dktari na mgonjwa ni 1:50,000 wakati kawaida ni 1:100, tumeshika mkia duniani kama sikosei.
Tatizo ni viongozi wanaoamua. Sidhani kama ishu ni kusaidia wananchi kisheria, inawezekana kuna wakubwa flani wanajaribu kudhibiti soko la uwakili. Am telling u hata hao walioapishwa juzi wamesota saana. Kulikuwa na mabishano sana, kuna viongizi serikalini waligoma kuwaapisha kua mawakili. Nina uhakika na hili.
Huu muhimili nafikiri haujapata right person wa ku-break the wall! JK mwenyewe aliahidi mwaka 5005 kuanzisha system ya paralegals wawe wanawakilisha washtakiwa mahakama za mwanzo ambazo Mawakili hawaruhusiwi ku-appear! Inawezekana wazo hili lilikutana na watu wasiopenda mabadiliko, akina CJ!
Ni kweli kuwa tarehe 17 kuna wano apishwa kuwa Advocates ila ukweli kwamba wengi wa wanaoapishwa hawajatokea hiyo law school bali ni kupitia Bar exam. Toka shulu hiyo ya sheria imeanzishwa matokeo ya madarasa manne yameshatoka ila idadi ya waliofaulu na kuapishwa haijafika hata 150 ingawa kila darasa lilikuwa na wastani wa wanafunzi 250.
Wamezingatia conflict of interest.Ni kweli kabisa, serikali inasema watakuwa wanafaidi pande zote mbili. Either unakuwa muajiriwa serikalini au wakili binafsi. Na sio vyote.. Jamaa wamekuwa disappointed sana.
Wamezingatia conflict of interest.
CJ amefanya kazi nzuri sana na ya kusifiwa. hakuna CJ yeyote Tanzania hii aliyefikia rekodi yake. Kwa mwaka huu pekee ameapisha mawakili wasiopungua 500 kwa historia ya Tanzania haijawahi tokea. Msimlaumu Mzee Wa watu kwa kazi nzuri aliofanya. Lawama ni kwa serikali walioleta pingamizi dhidi ya wafanyakazi wake tena asubuhi siku waliokuwa wanatarajiwa kuapa. Kisheria kukiwa na pingamizi hata dogo kiasi gani lazima lisikilizwe ndo mambo yaendelee.