LATRA yatoa mwongozo wa kujikinga na maambukizi ya COVID-19

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mamlaka ya Udhibiti na Usafiri Ardhini (Latra) imetoa mwongozo wa namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Covid 19 unaosababishwa na virusi vya corona kwa wamiliki wa magari yanayosafirisha abiria na mizigo.

Mwongozo huo unaowalenga pia waendesha bodaboda na bajaji umetolewa leo Alhamisi Februari 25, 2021 na mkurugenzi mkuu wa Latra, Gilliard Ngewe akiwataka abiria kuzingatia mambo mbalimbali ikiwemo kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni wanapoingia na kutoka katika vituo vikuu vya mabasi na treni.

Ngewe amewataka abiria hao kufunika mdomo na pua wanapokohoa na kupiga chafya kwa kutumia sehemu ya ndani ya kiwiko cha mkono.

Pia amewataka abiria kukaa umbali wa mita moja kati ya mtu na mtu wakati wa kusubiri usafiri vituoni.

“Kuvaa barakoa wakati wote unaposafiri na basi, daladala, treni, bodaboda au bajaji hasa pale unapohisi kuwa na dalili za corona ili kumlinda mwenzako na kutumia barakoa ambazo zimeidhinishwa na kupitia Wizara ya Afya ama za kitambaa cha kushona mwenyewe,” amesema Ngewe.

Amewataka waendesha teksi, bodaboda na bajaji kuhakikisha abiria wanapaka vitakasa mikono kabla ya kuwapakia kwenye vyombo vyao.

“Abiria waendelee kutumia njia za asili za kujikinga na maradhi kabla na baada na baada ya kutumia vyombo vya usafiri,” amesema.

Chanzo: Mwananchi

1614266159233.png


1614266180542.png
 
Wakae mita 1 toka mtu hadi mtu vituoni na kwenye mabasi, madala dala, ma ferry je?

Au huko kuji coronaise ruksa?

Ikumbukwe mzee baba Alicia ruksa ya watalii kuji coronaise.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hivi ni Taasisi gani inahusika na kuwaambia hawa watu ambao kila siku wanafanya ufunguzi wa miradi....

Sidhani kama wanazingatia hayo..., au huko ni Corona Free ?
 
Wakae mita 1 toka mtu hadi mtu vituoni na kwenye mabasi, madala dala, ma ferry je?

Au huko kuji coronaise ruksa?

Ikumbukwe mzee baba Alicia ruksa ya watalii kuji coronaise.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Tangu afisa wa Latra atake kumchinja na jambia dereva wa lori kule Mtwara niliwapuuza kabisa!
 
Mamlaka ya Udhibiti na Usafiri Ardhini (Latra) imetoa mwongozo wa namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Covid 19 unaosababishwa na virusi vya corona kwa wamiliki wa magari yanayosafirisha abiria na mizigo.

Mwongozo huo unaowalenga pia waendesha bodaboda na bajaji umetolewa leo Alhamisi Februari 25, 2021 na mkurugenzi mkuu wa Latra, Gilliard Ngewe akiwataka abiria kuzingatia mambo mbalimbali ikiwemo kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni wanapoingia na kutoka katika vituo vikuu vya mabasi na treni.

Ngewe amewataka abiria hao kufunika mdomo na pua wanapokohoa na kupiga chafya kwa kutumia sehemu ya ndani ya kiwiko cha mkono.

Pia amewataka abiria kukaa umbali wa mita moja kati ya mtu na mtu wakati wa kusubiri usafiri vituoni.

“Kuvaa barakoa wakati wote unaposafiri na basi, daladala, treni, bodaboda au bajaji hasa pale unapohisi kuwa na dalili za corona ili kumlinda mwenzako na kutumia barakoa ambazo zimeidhinishwa na kupitia Wizara ya Afya ama za kitambaa cha kushona mwenyewe,” amesema Ngewe.

Amewataka waendesha teksi, bodaboda na bajaji kuhakikisha abiria wanapaka vitakasa mikono kabla ya kuwapakia kwenye vyombo vyao.

“Abiria waendelee kutumia njia za asili za kujikinga na maradhi kabla na baada na baada ya kutumia vyombo vya usafiri,” amesema.

Chanzo: Mwananchi

View attachment 1711789

View attachment 1711790
Kidogo kidogo tunaanza kuongea lugha moja, ukweli ukidhihiri uongo hujitenga
 
“Kuvaa barakoa wakati wote unaposafiri na basi, daladala, treni, bodaboda au bajaji hasa pale unapohisi kuwa na dalili za corona ili kumlinda mwenzako na kutumia barakoa ambazo zimeidhinishwa na kupitia Wizara ya Afya ama za kitambaa cha kushona mwenyewe,” amesema Ngewe.
Pia amewataka abiria kukaa umbali wa mita moja kati ya mtu na mtu wakati wa kusubiri usafiri vituoni.
Kwahiyo abiria wakae umbali wa mita moja wakati wakisubiri usafiri lakini warundikane kwenye mabasi/daladala mithili ya mifugo inayosafirishwa, sijaona seriousness, this is madness
 
Tangu afisa wa Latra atake kumchinja na jambia dereva wa lori kule Mtwara niliwapuuza kabisa!

Ulifanya la maana sana mkuu.

Ila ungewapuuza na wale wanaotupiga changa la macho na nyungu, covidol, na bupeji hali wao ni wanufaika wa ile baba lao ya Pfizer ungekuwa umefanya maana zaidi.

Tuwapigie kelele kwa umoja wetu mabinafsi hawa.

Uthamani wa maisha ya watu hauna chama!

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kwahiyo abiria wakae umbali wa mita moja wakati wakisubiri usafiri lakini warundikane kwenye mabasi/daladala mithili ya mifugo inayosafirishwa, sijaona seriousness, this is madness

Wanasema staajabu ya Mussa.
 
Back
Top Bottom