Lamine Yamal kuburuzwa mahakamani

Lamine Yamal kuburuzwa mahakamani

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
11,235
Reaction score
22,581
1752598452028.jpg


Nyota huyo wa Barcelona anakabiliwa na uchunguzi huo kutokana na malalamiko ambayo mamlaka imesema imeyapokea kutoka kwa Chama Cha Mambilikimo nchini Uhispania kinachoitwa ADEE.

Duru za ndani zinaeleza kwamba Mbilikimo hao walikuwa katika sherehe hiyo iliyofanyika mwishoni mwa juma lililopita kama watumbuizaji.

Wizara ya Haki za Kijamii ya Uhispania imeitaka ofisi ya mwendesha mashtaka kuchunguza tukio hilo. Yamal alifikisha miaka 18 mnamo Julai 13 na tafrija yake hiyo ilihudhuriwa na wachezaji na watu wengi mashuhuri duniani.
 
😂 sasa jamani kwani kuwatumia mbilikimo kuna shida gani!!, mbona wao walikubali kutumbuiza ila watu wakikutafutia jambo watazua lolote walitakalo!.
Hii kesi imenichekesha si kidogo...🤣
 
Hao mbilikimo ni under 18 au above? Kama ni watu wazima, na walikubaliana kisha wakalipwa kabla na baada ya show, shida iko wapi?

Kwanini Pepe Kalle yeye hawakumshitaki kwa kumuajiri Emolo kwenye bendi yake ya Empire Bakuba? Au ni kwavile Pepe Kalle yeye alikuwa hatajwi kuwania Balloon D'or? Maswali ni mengi sana.
 
Bitozi nyangema Mr mawani ...nilijua tu pesa zote hizo lazima atachanganyikiwa tu...walikuepo masupastaa bwana akina Adriano ..saivi ni apeche alolo analewa chakari katika mitaa ya Jiji la Rio de Janeiro....akina Neymar wakasema ni Messi mpya...akawa hata anatamani kutembea hewani kwa kunyata ...huyu kaanza mapema hivi miaka 18? Hehehe...Nampa pole in advance
 
View attachment 3407068

Nyota huyo wa Barcelona anakabiliwa na uchunguzi huo kutokana na malalamiko ambayo mamlaka imesema imeyapokea kutoka kwa Chama Cha Mambilikimo nchini Uhispania kinachoitwa ADEE.

Duru za ndani zinaeleza kwamba Mbilikimo hao walikuwa katika sherehe hiyo iliyofanyika mwishoni mwa juma lililopita kama watumbuizaji.

Wizara ya Haki za Kijamii ya Uhispania imeitaka ofisi ya mwendesha mashtaka kuchunguza tukio hilo. Yamal alifikisha miaka 18 mnamo Julai 13 na tafrija yake hiyo ilihudhuriwa na wachezaji na watu wengi mashuhuri duniani.
Aliwasafirisha kutoka Kongo hadi Spain ( Human traffick) au?
 
Bitozi nyangema Mr mawani ...nilijua tu pesa zote hizo lazima atachanganyikiwa tu...walikuepo masupastaa bwana akina Adriano ..saivi ni apeche alolo analewa chakari katika mitaa ya Jiji la Rio de Janeiro....akina Neymar wakasema ni Messi mpya...akawa hata anatamani kutembea hewani kwa kunyata ...huyu kaanza mapema hivi miaka 18? Hehehe...Nampa pole in advance
Hii pole unaitoa ukiwa wapi?

Buza kwa mama kibonge au tegeta kwa ndevu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom