The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 11,100
- 13,698
Siyo siri wala uvumi tena. CCM sasa iko msambweni tokana na matamko ya makada wake wawili Mwenyekiti Samia Suluhu Hassan na Mnec Josephat Gwajima. Laiti wawili hawa wangenyamaza badala ya kuanika nguo zao za ndani hadharani.
Kwanza, Gwajima kama. mtu aliyetolewa jalalani na Magufuli na kumpa ubunge, siyo saizi ya Samia ambaye si Mwenyekiti tu bali Rais wa Jamhuri.
Pili, Gwajima alitaka kujipendekeza akaishia kujiteketeza kwenye chama kilichomvumilia kwa biashara yake ya kitapeli ya kiroho.
Tatu, ni rahisi kujua kuwa CCM itapata kazi kubwa kumshughulikia Gwajima ingawa nina uhakika watamshughulikia.
Nne, badala ya kuvuana nguo, wangeshughulikia tatizo la utekaji na ukamataji wapinzani na kuwabambnikizia kesi.
Tano, kwanini Gwajima kaona hili tatizo karibu na uchaguzi wakati lilianza wakati wa Magufuli aliyemtengeneza Gwajima kama alivyodai mbunge na msukuma mwenzake Kasheku Msukuma?
Sita, je Gwajima ana udhu wa kuaminika hata kuheshimika wakati alikuwa ndani ya chama kile kile anachokizodoa kwa kushindwa kusitisha utekaji?
Mbona. hajaongelea ufisadi na ugaidi vya kutisha ambavyo naye ni mshirika na mnufaika?