Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,288
Ebo! Kwahiyo mnapiga stori kwenye thread ya mwenzenu?
Kinakuuma nini bibie? Kutiwa atiwe mwenzio, kiuno ukatike wewe... Inahuu?
Ebo! Kwahiyo mnapiga stori kwenye thread ya mwenzenu?
Afaanalek! Ashakum kwikwikwiKinakuuma nini bibie? Kutiwa atiwe mwenzio, kiuno ukatike wewe... Inahuu?
mie naona lafudhi inatokana na mazoea yanayorithishwa toka kizazi hadi kizazi, hii inatokana na hali ya jamii ilivyo mfano wamarekani lugha yao ni ya mkato mkato haraka na jazba iliyojificha.
ingawa ni kiingereza kile kile jamaika pia wanakaribiana nao ingawa jamaika wamezidi ilitokana na kutokuelewana ambapo watu mara nying waliongea kwa kubishana na kurushiana maneno. tukiangalia watu wa mwambao walipata lugha laini kwa vle hawakuwa wafanya kaz ngumu pia waliishi maisha mazur kukaza kwa herufi imepatikana maeneo ya kaskazini kujionesha kuwa wao ni mashujaa hata kupitia sauti angalia hata wazulu wakiongea urithi wa hz lafudhi toka kizazi hadi kizaz umetufikisha hapa leo na ndio maana unakuta kuna watu wana lugha laini za kukaza za mkato na za kutirika na nyingne charehani watu wa vijiji kama bungu na maeneo kuizunguka rufiji na baadhi ya watu wa badgamoyo kifupi vijiji vya jirani na dar kupita coment nahs utafikiri beyound the ordinary.
nahs lugha mama sio 7bu ya kuzuka kwa lafudhi
Kitaaluma tungesema hivi:
Lafudhi ni matamshi ya msemaji wa lugha fulani ambayo yanatokana na athari za kimazingira. Mazingira hayo yanaweza kuwa eneo atokalo mtu, mahali alikosomea, kiwango chake cha elimu, tabaka lake la kijamii na kadhalika.
Kwa hiyo hapa chanzo kikubwa cha lafudhi ni mazingira alimo huyo mtumiaji lugha, mazingira hayo ni kama yalivyotajwa hapo juu. Lugha mama pia inaweza kuwa chanzo cha lafudhi tofautitofauti, kwa mfano katika kiswahili, hawa watu wakizungumza wazungumzaji wa kiswahili watajua wanatoka mkoa gani au ni kabila gani:
Lafudhi sio kitu kibaya, lakini pia huweza kubadilika kwa kutambua au bila kutambua (hii inaweza kutokea hadi umri wa miaka ishirini na). Lakini chanzo kikubwa cha lafudhi ni mzaingira alimo huyo mzungumzaji.
- Usiniretee maswara ya ubaguzi wa kikabira hapa
- Amemupiga mutoto ya watu juu amemuibia mfaranga makumi mawili
- Ukikaa nchale, ukichimama nchale
- Wewe unakamuaga mangombe tu moja kwa moja
- Mbona unakuwa kinganganizi, nilishakwambia sikupendi lakini wewe bado unaningangania tu!
Lugha mama ndio chanzo! Lugha moja hadi nyingne hutofautiana sana hasa kupitia sayansi ya lugha (Isimu)..utofaut huo unaweza kuupata katika
1.Idadi ya sauti za irabu
2.Idad ya saut za konsonant..
Hvyo hata ktka matamsh utofaut utakuwepo tu... kwa hapa TZ..katika lugha za makabila yetu mara nyngi lugha yenye matamsh lain huwa na irabu (schwa sound) siijui kswahl tunaiitaje...saut hii ambayo iko katka mfumo wa irab lakn utamkaj wake kifup twawezasema ni mjumuisho wa irabu kuu tano (a,e,i,o,u) na pale itakapotumika kwenye konsonant hutaweza kuickia kama ni a,e,i,o au u. Mfano makabila ya Mikoa ya Arusha+Manyara!
nakubaliana nawe ila kule wale black american tunajua wametokea africa je kuna muafrica anayezungumza kama mmarekani katika kujifunza kwake kiingereza kwa mara yakwanza jibu ni hapana.
mazingira yamewafanya wazungumze vle maingliano pia yamewafanya hata wazungu wazungumze kama wao,
Nakubaliana na wewe mkuukatka mazngira ya elimu ni kiwango kiduchu sana mkuu..maana tuna watu wengi sana na degree zao kibao lakin akiongea utajua tu anakotoka!!
Hahahaa...wewe ulishafika kwa fasi ya Goma?Nimeipenda no. 2 ambayo ni ya Kongo Mashariki...
Ebo! Kwahiyo mnapiga stori kwenye thread ya mwenzenu?
nakubaliana nawe tukisema chanzo ni lugha mama tunawazungumziaje wamarekani au hzo lugha mama zenyewe zina lafudh hiz lafudh zimetokana na nini hapo pamoja xna
lafudhi hutokana na lugha mama..... kumbuka kiswahili siyo lugha mama kwa kila mtu. mfano. mchaga aliyezaliwa na kukulia Dar, hawezi kuwa na lafudhi sawa na wa kiboro... kibororoni kweli! kwa sababu lugha mama haijamuathiri. kumbuk lugha zinatofautiana. mfano wamakonde hawana 's', wanyaki hawana 'v' nkhii hutokana na lugha mama ama lahaja ya mtu anayozungumza. sio kwenye kiswahili pekee, mfano : wataliano wa Napoli hawatamki sawa na wataliano wa Milan
Tanzania ni moja ila haina kabila moja ...kumbuka hilo
Kiswahili ni lugha moja ila ndani yake kuna lahaja nyingi sana, na kila lahaja ina namna yake ya kutamka. mfano watu wa tanga na mombasa wanafanana kiasi kimatamshi. Dar na Unguja pia hufana kiasi fulani.(kwa kuwa Dar ni mji kubwa na kuna watu wa makabila mengi ,kwa hiyo pana mchanganyiko wa lafdhi)
Lugha mama ina mchango mkubwa sana katika kuathiri lafudhi ya mzungumzaji, Mazingira, maingiliano, sawa kabisa ila hii inajikita zaidi katika lahaja, unachojaribu kukizungumzia hapa mkuu naona ni lahaja na wala sio lafudhi.nakubaliana na usemi kuwa lugha mama ni chanzo ila cjakubaliana nao moja kwa moja tuangalie kuna wabantu ambao lugha zao ni za kawaida si za kukaza na kuna wanaokaza herufi ikiwa wabantu asili yetu moja kwanini tumetofautiana hapa ndo utagundua kuwa mazngira elimu na maingiliano na dunia ya nje. yalianza kuleta mabadiliko ya taratibu kwa watu baada ya miaka mingi na kujikuta lafudhi zao zinakuwa tofauti kabisa. mpaka sasa hizo lafudh za lugha mama zimeendelea kuathiri matamshi yao katika kiswahili chao
Lugha mama ina mchango mkubwa sana katika kuathiri lafudhi ya mzungumzaji, Mazingira, maingiliano, sawa kabisa ila hii inajikita zaidi katika lahaja, unachojaribu kukizungumzia hapa mkuu naona ni lahaja na wala sio lafudhi.
Hahahaa...wewe ulishafika kwa fasi ya Goma?
Hapo kwenye nyekundu ni 'isimujamii'... Vipi tena mzee?Kwa wamarekani ni suala jingine, hao tunaweza kusema eneo la kijiografia ndo limechangia (eneo la kijiografia pia ni moja ya sababu za kiisimu katika kutofautiana kwa lafudhi) na ndo maana kiingereza cha Marekani, Uingereza na Australia ni tofauti inagawaje wote lugha yao ya kwanza ni kiingereza, hii inathibitisha eneo la kijiografia kuchangia katika tofauti ya lafudhi.