Ladies hii imekaaje?

pureman2

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2019
Posts
1,491
Reaction score
2,563
Waungwana seba akojiwe !!

Naomba kujua huwa mnajisikiaje , nyinyi , ndugu zenu, na wazazi wenu.

Dada unapata mchumba na unaanza kumueleza changamoto zako binafsi , ndg zako na wazazi wako.

Unapewa pesa ya kujikimu , sio kidogo almost 2M per month

Unalipiwa pesa yote ya madeni kwenye vikoba

Unalipiwa mkopo wa Bank Kama 20 M hivi

Unapewa pesa ya maamdalizi ya kuvishwa Pete ya uchumba si chini ya 5M

Unaomba pesa ya kununua gari kama 17M

Unaomba pesa ya kununua kiwanja kama 15 M

Hayo yote ndani ya miezi 4 toka tufahamiane

Hili limekaaje ? Ni penzi au mkakati wa kuondoa umasikini wa ukoo

Kama ni wewe unajisikiaje na ukoo wako?

Ukiolewa unazani utalipia vipi gharama hizi
 
Ni wewe ndio umetoa pesa yote hiyo?

Kujikimu = 2mil per month
Mkopo = 20mil
Gari = 17mil
Kiwanja = 15mil
Pete = 5mil
Madeni Vicoba = undisclosed

Maana kama una uwezo wa kumpa mtoto wa mwanaume mwenzio pesa yote hii, ina maana una uwezo wa pesa na sijui kwa nini umeandika uzi wa kulalamika...
 
Kuna wimbo unaitwa kekundu almaarufu wajinga ndio waliwao.
 
Pole sana ndugu kwa kutoa mahela yote haya afu ukapigwa na kitu kizito kwenye FUVU...
 
ajabu iliyoje.
 
Kwake wewe ni asset
Hakika hakuachi asilani mpaka uwe liability πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Nimeyaona ulimwenguni mkuu
 

Amka usije ukajikojolea huko!
 
Sio siri limbwata lipo ndugu zanguni..πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…