Billy Kimber
Member
- May 20, 2022
- 89
- 193
Japo laana ni suala la kiimani na vitu vya kiimani ni ngumu kuvithibitisha,lakini kwa namna flani haya mambo ya laana yapo.
Mwaka 1962 baada ya taji lake la pili la kombe la Ulaya alilowafunga Real Madrid 5-3 kwenye fainali, kocha mkuu wa Benfica Bela Guttmann aliomba nyongeza ya mshahara kwa mabosi wa klabu lakini ombi lake lilikataliwa licha ya mafanikio makubwa aliyoipatia klabu hiyo.
Pia mkataba wake ukakatishwa ghafla kwa kile kilichodaiwa kudai kwake nyongeza ni kosa la kinidhamu, inaelezwa baada ya hayo yote Guttmann alisema: "Not in a hundred years from now will Benfica ever be European champions." Akimaanisha kuwa Benfica haitabeba tena kombe la Ulaya kwa miaka 100 kutoka hapo.
Kilichofuata kutokea hapo ni kwamba Benfica imefika katika fainali tano za kombe la UEFA na fainali tatu za Kombe la UROPA tangu mwaka huo 1962, na fainali zote imeambulia kipigo. Jumla Benfica imefungwa katika fainali 8 za Ulaya, sio kawaida.
Laana kama hii iliikumba timu ya taifa ya Autralia. Australia lilimtumia mchawi kutoka zimbabwe ili wafuzu kucheza kombe la Dunia kwa mara ya 1 mwaka 1974 huko Germany, walifanikiwa lakini mtaalamu hawakumlipa. Toka hapo hawakufuzu tena hadi mwaka 2005 waliporudi Afrika kumsaka mtaalamu wamlipe.
Baada ya hapo Australia ilifanikiwa kufuzu kwenye kombe la dunia tena huko Ujerumani mwaka 2006 baada ya kutofuzu kwa miaka 32 tangu mwaka huo 1974, na imeendelea kufunzu kwa miaka yote ya mashindano hayo kuanzia 2010, 2014 na 2018 na 2022.
Laana kama hii pia inatajwa kumuandama kocha wa Man City Pep Guadiola kwa kumfanyia madharau aliyekuwa mchezaji wake Yaya Toure raia wa Ivory Coast. Inaelezwa kuwa masikitiko ya Toure yalimlenga Pep kutoshinda UEFA akiwa na klabu yeyote.
Wakala wa Toure Dimitry Seluk alisema kuwa mizimu ya Afrika haiwezi kumruhusu Pep ashinde kikombe cha ulaya akiwa na klabu yoyote ya soka mpaka amuombe radhi Toure.
View attachment 2283362
Mwaka 1962 baada ya taji lake la pili la kombe la Ulaya alilowafunga Real Madrid 5-3 kwenye fainali, kocha mkuu wa Benfica Bela Guttmann aliomba nyongeza ya mshahara kwa mabosi wa klabu lakini ombi lake lilikataliwa licha ya mafanikio makubwa aliyoipatia klabu hiyo.
Pia mkataba wake ukakatishwa ghafla kwa kile kilichodaiwa kudai kwake nyongeza ni kosa la kinidhamu, inaelezwa baada ya hayo yote Guttmann alisema: "Not in a hundred years from now will Benfica ever be European champions." Akimaanisha kuwa Benfica haitabeba tena kombe la Ulaya kwa miaka 100 kutoka hapo.
Kilichofuata kutokea hapo ni kwamba Benfica imefika katika fainali tano za kombe la UEFA na fainali tatu za Kombe la UROPA tangu mwaka huo 1962, na fainali zote imeambulia kipigo. Jumla Benfica imefungwa katika fainali 8 za Ulaya, sio kawaida.
Laana kama hii iliikumba timu ya taifa ya Autralia. Australia lilimtumia mchawi kutoka zimbabwe ili wafuzu kucheza kombe la Dunia kwa mara ya 1 mwaka 1974 huko Germany, walifanikiwa lakini mtaalamu hawakumlipa. Toka hapo hawakufuzu tena hadi mwaka 2005 waliporudi Afrika kumsaka mtaalamu wamlipe.
Baada ya hapo Australia ilifanikiwa kufuzu kwenye kombe la dunia tena huko Ujerumani mwaka 2006 baada ya kutofuzu kwa miaka 32 tangu mwaka huo 1974, na imeendelea kufunzu kwa miaka yote ya mashindano hayo kuanzia 2010, 2014 na 2018 na 2022.
Laana kama hii pia inatajwa kumuandama kocha wa Man City Pep Guadiola kwa kumfanyia madharau aliyekuwa mchezaji wake Yaya Toure raia wa Ivory Coast. Inaelezwa kuwa masikitiko ya Toure yalimlenga Pep kutoshinda UEFA akiwa na klabu yeyote.
Wakala wa Toure Dimitry Seluk alisema kuwa mizimu ya Afrika haiwezi kumruhusu Pep ashinde kikombe cha ulaya akiwa na klabu yoyote ya soka mpaka amuombe radhi Toure.