Kyela: Wananchi waililia Bandari ya Itungi

Kyela: Wananchi waililia Bandari ya Itungi

Wananchi Wilayani Kyela wamesikitishwa na kusononeka baada ya kuambiwa kwamba Bandari yao waliyoitunza na kuipenda kwa miaka yote , nayo imechukuliwa na Waarabu wa DP WORLD

Huku wakibubujikwa na Machozi , wananchi waliopakana na Bandari hiyo kutoka vijiji vya Bujesi , Njisi , Ngonga na Kajunjumele wameonekana kukata tamaa kuhusu uwekezaji huo , hasa wakizingatia kwamba ni hivi karibuni Serikali ilitumia hela nyingi kujenga meli mbili za kisasa zilizotengenezwa na Kampuni ya Songoro Marine ya Ilemela Mwanza , Taarifa zaidi zinasema kwamba wananchi hao kwa umoja wao wanatafakari hatua za kuchukua ama Wamuachie Mungu aamue.

Taarifa za Bandari za ziwa Nyasa kubinafsishwa kwa Waarabu zimefichuliwa na Mwenyekiti wa Chadema , Freeman Mbowe alipoongea na Waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Chama chake jana na kwamba Bandari za Mbambay , Manda na Itungi nazo zimekwenda na maji kwa muda usiojulikana .

Mungu Ibariki Kyela .
Ujielewi mtadanganya wajinga hivi Dp work wawekeze bandari ya kyela Ili wapate Nini hakuna ata mixigo cdm ni mpango wa ovyo atuwezi ata kuwapa nchi
 
Ujielewi mtadanganya wajinga hivi Dp work wawekeze bandari ya kyela Ili wapate Nini hakuna ata mixigo cdm ni mpango wa ovyo atuwezi ata kuwapa nchi
Soma kwanza mkataba wa DP WORLD halafu ndio urudi kuchangia , unashangaa Itungi wakati kuna bandari duni zaidi ya hiyo wamepewa .

Muda hautoshi ningekuwekea bandari zote walizouziwa hapa
 
Back
Top Bottom