Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,582
- 284,132
Wananchi Wilayani Kyela wamesikitishwa na kusononeka baada ya kuambiwa kwamba Bandari yao waliyoitunza na kuipenda kwa miaka yote , nayo imechukuliwa na Waarabu wa DP WORLD
Huku wakibubujikwa na Machozi , wananchi waliopakana na Bandari hiyo kutoka vijiji vya Bujesi , Njisi , Ngonga na Kajunjumele wameonekana kukata tamaa kuhusu uwekezaji huo , hasa wakizingatia kwamba ni hivi karibuni Serikali ilitumia hela nyingi kujenga meli mbili za kisasa zilizotengenezwa na Kampuni ya Songoro Marine ya Ilemela Mwanza , Taarifa zaidi zinasema kwamba wananchi hao kwa umoja wao wanatafakari hatua za kuchukua ama Wamuachie Mungu aamue.
Taarifa za Bandari za ziwa Nyasa kubinafsishwa kwa Waarabu zimefichuliwa na Mwenyekiti wa Chadema , Freeman Mbowe alipoongea na Waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Chama chake jana na kwamba Bandari za Mbambay , Manda na Itungi nazo zimekwenda na maji kwa muda usiojulikana .
Mungu Ibariki Kyela .
Huku wakibubujikwa na Machozi , wananchi waliopakana na Bandari hiyo kutoka vijiji vya Bujesi , Njisi , Ngonga na Kajunjumele wameonekana kukata tamaa kuhusu uwekezaji huo , hasa wakizingatia kwamba ni hivi karibuni Serikali ilitumia hela nyingi kujenga meli mbili za kisasa zilizotengenezwa na Kampuni ya Songoro Marine ya Ilemela Mwanza , Taarifa zaidi zinasema kwamba wananchi hao kwa umoja wao wanatafakari hatua za kuchukua ama Wamuachie Mungu aamue.
Taarifa za Bandari za ziwa Nyasa kubinafsishwa kwa Waarabu zimefichuliwa na Mwenyekiti wa Chadema , Freeman Mbowe alipoongea na Waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Chama chake jana na kwamba Bandari za Mbambay , Manda na Itungi nazo zimekwenda na maji kwa muda usiojulikana .
Mungu Ibariki Kyela .