Kwenye sakata la mchanga wa dhahabu, nafahamu ukweli wa ndani

Nimefanya kazi katika moja ya migodi mikubwa Tanzania inayozalisha mchanga wa dhahabu kwa zaidi ya miaka 2 so najua at least 90% ya kinachohusiana na mchanga wa dhahabu

Mchanga unaosafirishwa nchi za nje kutoka katika Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu ni mchanga wenye mchanganyiko wa dhahabu, copper, silver, iron na vinginevyo. Process inayofanya ili kutengeneza mchanga wa dhahabu ni flotation ambayo nia yake ni kupunguza uwepo wa copper katika material ambayo hupelekwa katika Carbon In Leach (CIL) circuit. Uwepo wa copper katika CIL circuit uwa unaathiri uzalishaji wa dhahabu maana cyanide uwa inareact sana na copper than dhahabu na mwisho dhahabu hutoka katika makapi. Hii ndio sababu pekee ya inayofanya migodi kupunguza copper katika circuit.

Kiwango cha dhahabu katika kontena moja la Mgodi XXX uliopo Kahama uwa ni around 150 - 270 g/t, Copper uwa ni 12 – 18% (1% = 10,000 ppm, 1 ppm = 1 g/t) na silver ni around 200g/t. For example katika mwaka wa 2011, Average gold iliyozalishwa na kuwekwa katika makontena ilikua ni around 262.031 g/t na copper ilikua ni 16.532 %. Pia September 2013, Average gold ilikua 186.83 g/t na copper ilikua ni 12.58 %.

Tanzania Minerals Audit Agency (TMAA) ni agency ya serikali ambayo uwa inachukua sample za mchanga kwa ajili ya analysis ili kucompare majibu ya huo mchanga na majibu ya mgodi kwa ajili ya kodi. Cha kujiuliza ni je watu wa TMAA wanachukua sample kwa usahihi? Uwa wanachukua spear ngapi katika kila kontena ili wapate representative sample? Je watu wa TMAA wanafanya Analysis kwa mashine ambazo zinakua calibrated kila baada ya muda? Je ni muda gani wanacalibrate hizo mashine zao? Je wamewahi kuchukua sample zao na kupeleka katika Laboratory nyingine ili kumake comparison ya majibu yao na ya wengine ili kuona kama wako sahihi au lah?

Baada ya sample kuchukuliwa, ni wakati wa maafisa wa mgodi husika, TRA, MEM na TMAA kuyafunga yale makontena kwa kutumia seal.

Napenda kusema kua kauli iliyotolewa na Engineer mmoja pale bandarini kua ndani ya makontena hayo asilimia 90 ya mchanga ni dhahabu na sio shaba ni ya UONGO kwa asilimia zaidi ya 100. Napenda kusema kua alikosea sana na alistahili kutoa kauli ya kuunda tume ili kuhakikisha walichoreport TMAA na Migodi kama viko sahihi au lah. Kauli yake inaonesha kua TMAA na Migodi uwa wanatupa report za uongo kuhusiana na kiwango cha madini kilichopo ndani ya makontena. Kauli ya aliekua Katibu Mkuu wa Wizara kua iundwe Tume ilikua ni njia sahihi kuthibitisha kua kilichomo ndani ya Makontena ni kitu sahihi kama report zilivyowasilishwa na TMAA na Migodi au lah.

Note: 1. Calibration is the process of calibrating an instrument or experimental readings.

2. Spear ni kifaa maalumu cha kuchukulia sample katika yale makontena


No research.. No right to speak Ndg. Engineer Kakonko
Uko sawa, kwenye ule mchanga ni ni vigumu sana kuwekwa 500g/t.
 
Mi nachekaga sana ninapo somaga comments za watu humu, mleta UZI sidhani kama utasikilizwa, ulicho kiongea ndio ukweli wenyewe but who will listen to you? Ulicho ongea ndio ukweli wenyewe. Eti container moja lina over 90% ya dhahabu. Mjinga gani asafirishe dhahabu nyingi hivyo kwa kutumia lorry? Hivi mchanga kilo 20 tu wenye 90% ya dhahabu si unatafuta mercury tu then unatia hapo and then upate dhahabu? Maderava wa malori wasingekua na sababu ya kuiiba diesel lita 100 ili wauze wakati ana dhahabu kaibeba kwa container. Anyway, nilicho gundua sasa hvi hata wataalamu wetu nao wameamua kuongea uongo tu ili kumridhisha mhe raisi, hawataki kuongea ukweli ni full kudanganya. TMAA, TRA, GST wote wanaujua ukweli but nashangaa nao eti wamekaa kimya kabisa.
hapo kwenye mfano wa mchanga wa kg 20 unatia mercury...umenifahamisha vyema sana juu ya mambo ya dhahabu, maana si mwenye kuyajua kabisa.
 
Huyu mleta mada ndo afisa uhusiano wao nini,Mheshimiwa alichokuwa anakitaka huo mchanga uyeyushwe hapa hapa nchini,kuweka kwenye kontena kunaleta sintofahamu,watanzania tunataka mtuyeyushie huo mchanga hapa hapa kwetu kwani c mnajua vijana wetu wengi hawana ajira
 
Ni zaidi ya mchanga mfano mzuri ni mtoto anayetumwa halafu akakataa kisha kesho yake anaomba hela ya tuition, mlitumwa kuihudumia jamii ni ngumu kuwatetea kama mnalipana bonus kubwa halafu hamna maendeleo stahiki kwa wananchi
 
Huyu mleta mada ndo afisa uhusiano wao nini,Mheshimiwa alichokuwa anakitaka huo mchanga uyeyushwe hapa hapa nchini,kuweka kwenye kontena kunaleta sintofahamu,watanzania tunataka mtuyeyushie huo mchanga hapa hapa kwetu kwani c mnajua vijana wetu wengi hawana ajira

Umesoma mkataba?

Yani jambo lipo kisheria,na kontena zina seal ya serikali. Tunawacheleweshea wawekezaji kwenda kupembua mchanga wao,itakula kwetu.
 
wakati mkuu wa nchi alipoanza na mbwembwe alipoingia madarakani tulipinga sana yale maamuzi ya kukurupuka ila wenzetu mlitukejeli sana nafiki mmeanza kuisoma namba, kwa hili la madini kwa kweli litaturudisha pale tulipokuwa miaka ya 1970-1980-1990 hapa cha kufanya ni serikali ifuatilie mapato yake kwa ukaribu sio kumrazimisha mfanyabiashara achenjulie mabaki ya madini hapahapa tanzania, serikali yenyewe imeshindwa kujenga hata kiwanda cha tooth-pick walivyokuwa navyo wameviua tena vya kusindika vyakula sembuse vyuma tuache ujinga wawekezaji watahama na tutawatafuta kwa manatiiiii.
 
hapo kwenye mfano wa mchanga wa kg 20 unatia mercury...umenifahamisha vyema sana juu ya mambo ya dhahabu, maana si mwenye kuyajua kabisa.
Wachimbaji wadogo hutumia mercury kui separate dhahabu kutoka kwenye udogo though wakubwa na wa kati wao wanatumia Sodium Cyanide, the difference between these 2 chemicals is, Mercury inaweza ku recover dhahabu only by 15% na cyanide yenyewe inaweza ku recover up to 96% ya dhahabu iliopo kwenye ore.

Siku nyingine nitaeleza na kuwapongeza wale wenzetu waliokwenda Msumbuji kutafuta dhahabu; walitumia hiyo njia ya pili, kwasasa niishie hapo tu.
 
Amesema ana uhakika 90% ya kilichopo kwenye mchanga kuna dhahabu,na sio ana uhakika 90% ya mchanga ni dhahabu
Mh! Kama ni hivyo sidhani kuwa ingekuwa habari. Maana mchanga wenyewe unaitwa mchanga wa dhahabu.
 
Napenda kusema kua kauli iliyotolewa na Engineer mmoja pale bandarini kua ndani ya makontena hayo asilimia 90 ya mchanga ni dhahabu na sio shaba ni ya UONGO kwa asilimia zaidi ya 100. Napenda kusema kua alikosea sana na alistahili kutoa kauli ya kuunda tume ili kuhakikisha walichoreport TMAA na Migodi kama viko sahihi au lah. Kauli yake inaonesha kua TMAA na Migodi uwa wanatupa report za uongo kuhusiana na kiwango cha madini kilichopo ndani ya makontena. Kauli ya aliekua Katibu Mkuu wa Wizara kua iundwe Tume ilikua ni njia sahihi kuthibitisha kua kilichomo ndani ya Makontena ni kitu sahihi kama report zilivyowasilishwa na TMAA na Migodi au lah.
Mkuu, nimekusoma kuanzia mwanzo hadi mwisho; kwanza umeongea kitaalamu na pia umeongea kama shahidi wa tukio kwa maana ya kufanya kazi kwenye moja kati ya hiyo migodi, sitachangia tena uzi hu cause what you said ndicho kitu halisi. Yule jamaa wa bandarini ukweli ana represent sample ya wataalamu wengi wa serikalini kwasasa, wengi wao wanapenda kuongea kitu kitakacho mfurahisha mkubwa na sio ukweli halisi, In science you cant cheat, wana sharia wanaweza bishana mahakamani na wakili A akamshinda wakili B hata kwa uongo, kwenye sayansi sio hivyo; napendekeza ule mchanga uliodaiwa una over 90% ya dhahabu ichukuliwe sample na ipelekewe kwenye maabara yoyote duniani na sample hiyo hiyo ipelekwe GST Dodoma, maabara ya TMAA ya Dar na wapeleke pia maabara za SGS zilizopo nchini, sina hakika kama TBS pia wanaweza kupima. Wengine wanatumbuliwa kwa false information tu; huyu wa wizarani pamoja na engineer Mramba the ex CEO wa Tanesco. Otherwise, thanks brother kwa kuusema ukweli.
 
Naomba ni declare interest kuwa, mimi ni mmoja wa wataalam wanaouhusika na ishu iyo ya mchanga.

Kifupi naomba nieleze kile ambacho kipo kwenye makontena. Kilichopo kwenye makontena kwa asilimia kubwa ni copper(Cu) , ifufuatiwa na silver (Ag) na dhahabu (Au) haizidi asilimia 0.05.

Yule Afisa wa Bandari aliyesema kuwa zaidi ya asilimia 90 ni dhahabu ni muongo na anapaswa kuiomba radhi ACACIA na watanzania kwa ujumla na atumbuliwe kwenye nafasi yake.

Kiwango kilichopo kwenye yale makontena zaidi ya 256 ni kati ya sililimia 0.012 -0.02, g/t

Mh spika alidhani kiwango cha asilimia 0.02 kuwa ni kidogo na hauwezi kupata faida iwapo utalisafirisha kontena kutoka mgodini mpaka China, Japan au Ujerumani.
Naomba nimuulize, anajua gharama ya kusafirisha hilo kontena? Kifupi haizidi milioni 8.

Nikija kwenye mchanganua wa hiyo asilimia 0.02 kwa contena, naomba nimfafanulie mh spika kama ifuatavyo:-

(1) 0.02% hii ni gram kwa tani, kwa maana hiyo hii ukiizidisha kwa tannage zilizopo (eg 20.5tn), utapata 0.41%.
(2) Hii 0.41 ili upate ppm, unatakiwa uizidishwa kwa 10000, utapata 4100ppm au g/t.
kwa maana nyingine, yule mtaalam wa TMAA aliwaambia kwenye kila container kuna takriban kilo 4.1. sasa hii ni ndogo?
(3) Kwa sasa kilo ya dhahabu ni takribani mil 90. 90x4=360m.
sasa iwapo utasafirsha container moja kwa 10m, huoni kuna faida?

Pia Kamati ya Bunge kupitia Spika alidai kwa mwaka ACACIA, Buzwagi na Bulyanhulu huzalisha takribani idadi ya makontena elfu 50, na kwa maana hiyo contena milioni moja yameisha safirishwa. HUU SIO UKWELI.

Ukweli ni kwamba hizo ni tani za mchanga wa dhahabu na sio idadi ya kontena.

Mpaka sasa, migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi wameisha safirisha makontena yasiozidi elfu 50.

Mpaka sasa Bulyanhulu peke yake wamesafirisha contena sizizozidi elfu 42. Sasa hizo contena 1m, zimetoka wapi?

Mh. rais kuna wanakupotosha, na hili utalithibitisha kupitia sample zilizochukuliwa na Mh Waziri Mkuu jana katika mgodi wa Buzwagi, kwani kati ya makontena aliyochukua sample, moja wapo ni kontena ambalo lililkua na seal na document zote za serikali na lilikua tayari kusafirishwa kwenda Ujerumani. Baada ya tamko la rais kontena hilo lilirudishwa mgodini pamoja na makontena mengine 3, yakiwa tayari yamefika Isaka.

My take:-

Kwenye hili sakata la mchanga, mihemuko isitumike. Wawekezaji wa ACACIA hawamuibii mtu kwani hata kama kungekua na 90% ya dhahabu, TMAA huchukua sample pia, kiasi kwamba wangeweza kuiambia serikali kuwa ACACIA wanawaibia kwa kutoa takwimu za uongo.

Iwapo mikataba haiwafaidishi watanzania, ifanyiwe review kwani ACACIA hutumia mikataba hiyo hiyo kufanya calculation zao.

Iwapo itathibitika kuwa ACACIA pia hawawaibii watanzania kwa kuficha dhahabu kwenye mchanga, basi pia Katibu Mkuu aombwe radhi.
Mtoa hoja..kupotoshwa ni jambo moja na kupoteza rasilimali kama nchi ni dhahiri....ima kwa mikataba mibovu or otherwise....
 
kilo moja kwa kilo moja tofauti inatoka wapi BossKazi?
Yep kama hili unatambua basi nadhani tutakua pamoja kwenye suala la container la mchanga.

Jua mchanga unavyopakiwa kwenye lile container hautakiwi kuzidi tani 50. Katika hizo tani 50 ni pamoja na uzito wa gari na uzito wa container.

Sasa tufanye mchanga unaweka tani 40. Ambayo ni kg 4000. Katika kilo gram 4000 asilimia 90 ni dhahabu. Kwa hiyo kwa sbb dhahabu density yake ni kubwa maana ake utakua na mchanga kidogo lakini ni mzito. Kwa hiyo unaweza kuta labda mchanga ni robo ya container ila uzito wake ni kilo 4000 ukichukua 90% ni kilo 36,000.

Kama ukichukua mchanga wa kawaida ambao hauna dhahabu ili upate tani 40 utalazimika kujaza container wakati ule wenye dhahabu unahitaji kuweka robo ili upate tone 40.natumai kama umefanya hata basic mathematics utakua umenielewa. So tuna vyo sema mchanga una 90% ya dhahabu ni kwa uzito ule uliobebwa.

Container lime beba tani 40 za mchanga. Katika tani 40 asilimia 90 ni dhahabu. Kwa hiyo dhahabu ni tani 36. Sawa ndg?
 
mkuu, africa ya kusini walianza kuchimba dhahabu miaka 100 iliyopita kimsingi dhahabu ilishakwisha wanakula marudio, ni sawa na spain ndio iliyokuwa nchi ya kwanza kuwa na migodi ya dhahabu chini ya mfalme napoleoni leo walishasahau kama waliwahi kuwa na dhahabu.
Hujajibu swali langu. Hayo marudio wanachenjua wenyewe?
 
Mwekezaji alipigia mahesabu pia huo mchanga ndo mana akaweka kiwanda, ndo mana leo anasema, gold from CIL and Gravity huchangia 50% ya revenue yake na concentrate pia huchangia 50% ya revenue yake.
Hapo nashawishika kuwa tunaibiwa, yaani kwenye production pale site anapata 50% tu ya faida na 50% nyingine IPO kwenye huo mchanga, hata kama kuna copper ndio iwe faida yote hiyo? Ebu fikiria kidogo uzalishaji uliopo eneo la tukio la mradi wenyewe, linganisha na huo mchanga, halafu faida iwe nusu kwa nusu!!!
 
mkuu, africa ya kusini walianza kuchimba dhahabu miaka 100 iliyopita kimsingi dhahabu ilishakwisha wanakula marudio, ni sawa na spain ndio iliyokuwa nchi ya kwanza kuwa na migodi ya dhahabu chini ya mfalme napoleoni leo walishasahau kama waliwahi kuwa na dhahabu.
Una uhakika dhahabu SA imeisha? Hebu nipe takwimu mkuu. Maana nijuavyo wao ndo wanaongoza Africa. Ni kwa hayo marudio tu? Nipe link nijisomee.
 
Back
Top Bottom