Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,210
- 42,072
Ukweli ni kwamba kwenye sekta ya utalii lazima tukubali kuwa Rais Samia awezi kuwa na ushawishi wa kuwavuta watalii au kuvuta watu kuangalia filamu ya royal tour maana hakuna kitu ambacho anawezi kuwavutia wengi hasa duniani kuitazama!
Washauri wa Rais walipaswa kujua kuwa ili watu watazame filamu fulani lazima kuwe na sababu nyingi ikiwemo umaarufu wa mtu aliyeshiriki kwenye filamu hiyo! Walitakiwa kujua kama wanataka Samia aonekane kwenye Tv basi wangemuacha aonekane lakini watafute mtu mwingine mwenye ushawishi duniani kote na kwa watu wengi ili filamu iwe na mvuto si kwa wamakonde tuu bali dunia nzima!
Mfano kama Samia angekuwa na Ronaldo kwenye filamu unafikiri kingetokea nini?
Kama Samia angekuwa na Mess kwenye Filamu kingetokea nini?
Kama Samia angekuwa Kanye west kwenye Filamu kingetokea nini?
Hii ni moja ya mifano ambayo nimejaribu kuifikiri kwa haraka ambayo naona ingelipa zaidi kuliko Rais samia kushiriki peke yake kwenye filamu hii kitu ambacho hakitakuwa na effect yeyote kwa nchi zaidi tutajikuta tunalishwa propaganda kuwa watalii fulani wmeletwa na Royal tour kumbe siyo!
Kwenye ulimwengu wa watu mashuhuri na wenye ushawishi duniani lazima tukubali ukweli mchungu kuwa Rais Samia sio mmoja wao hivyo hakufaa kuwepo au kushiriki pekee kwenye hiyo fialmu kama tunataka matokeo kweli na sio siasa!
Kama swala ni hela ukweli ni kwamba nchi hii haiwezi kushindwa kutumia hata zaidi ya billion hata 30 kuwekeza kwenye utalii na matangazo kwani tumekuwa na matumizi mabovu zaidi ya mabillion na mabillion!
Hivyo ni ukweli usio pingika katika hili la kuitumia filamu kutangaza vivutio tumepata hasara kwa kuwa tumeshindwa kujua tumtumie nani kuwafikia wakina nani!
Washauri wa Rais walipaswa kujua kuwa ili watu watazame filamu fulani lazima kuwe na sababu nyingi ikiwemo umaarufu wa mtu aliyeshiriki kwenye filamu hiyo! Walitakiwa kujua kama wanataka Samia aonekane kwenye Tv basi wangemuacha aonekane lakini watafute mtu mwingine mwenye ushawishi duniani kote na kwa watu wengi ili filamu iwe na mvuto si kwa wamakonde tuu bali dunia nzima!
Mfano kama Samia angekuwa na Ronaldo kwenye filamu unafikiri kingetokea nini?
Kama Samia angekuwa na Mess kwenye Filamu kingetokea nini?
Kama Samia angekuwa Kanye west kwenye Filamu kingetokea nini?
Hii ni moja ya mifano ambayo nimejaribu kuifikiri kwa haraka ambayo naona ingelipa zaidi kuliko Rais samia kushiriki peke yake kwenye filamu hii kitu ambacho hakitakuwa na effect yeyote kwa nchi zaidi tutajikuta tunalishwa propaganda kuwa watalii fulani wmeletwa na Royal tour kumbe siyo!
Kwenye ulimwengu wa watu mashuhuri na wenye ushawishi duniani lazima tukubali ukweli mchungu kuwa Rais Samia sio mmoja wao hivyo hakufaa kuwepo au kushiriki pekee kwenye hiyo fialmu kama tunataka matokeo kweli na sio siasa!
Kama swala ni hela ukweli ni kwamba nchi hii haiwezi kushindwa kutumia hata zaidi ya billion hata 30 kuwekeza kwenye utalii na matangazo kwani tumekuwa na matumizi mabovu zaidi ya mabillion na mabillion!
Hivyo ni ukweli usio pingika katika hili la kuitumia filamu kutangaza vivutio tumepata hasara kwa kuwa tumeshindwa kujua tumtumie nani kuwafikia wakina nani!