Hata mimi nakubaliana na wewe katika hili siku hizi mahari haina maana yoyote. Mahari ilikuwa na maana zamani na hasa mahari ya kweli ilikuwa inatolewa mfano uchaggani na/au uhayani.
Kule ilikuwa inapelekwa zaidi zaidi pombe alafu mkishakubaliwa mnainywa wenyewe kwa pamoja na wenyeji, kisha mnarudishiwa madumu yenu matupu mnaondoka.
Siku hiyo ya mahari ilikuwa kama siku ya wazee wa pande mbili kufahamiana (get together flani). Siku hizi ujanja ujanja umekuwa mwingi nao wanatozana pesa nyingi, utafikiri wanauza binti yao.
Ndiyo maana hata heshima ya ukwe/mkwe imepungua sana kama siyo kuisha kabisa. Zamani mkwe alikuwa mkwe kweli kweli siyo haya ya siku hizi ambapo baba/mama mkwe analewa pamoja mke/mme wa mtoto wake kisha wakishalewa wanakokotana kwenda nyumbani. Hakuna heshima kabisaa.
Sasa mtu unamtoza mamillioni ya pesa eti mahari, mwisho wa siku anaichukulia kama biashara nyingine kama vile kanunua gari showroom ataanzia wapi kukuheshimu kama mkwe??