ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Miongoni mwa maendeleo ambayo Mkoa wa Morogoro unajivunia kwa sasa ni ongezeko la nyumba za kulala wageni ambazo nyingi zinamilikiwa na wahadhiri wa vyuo vikuu vilivyomo mkoani huo hasa SUA. Pengine ilnadaiwa kuwa kwa sasa Morogoro inaweza kuwa inaongoza kwa nyumba nyingi za kulala wageni zilizojengwa na watumishi wa Umma.
Hata hivyo, uchunguzi unaonyesha kuwa baadhi ya nyumba hizo, nyingi zimejengwa holela na pasipo kuzingatia viwango vya ubora wa majenzi (sustainable building standards) hasa kwa upande wa "size" za vyumba na hata malighafi zinazotumiwa (nyingi ni mchina!).
Tazama viwango vya upana wa choo hiki ambacho kipo moja ya nyumba mpya kabisa ya kulala wageni maeneo ya Msamvu. Japo wahenga wanasema kwenda haja kuna starehe yake kama ilivyo kwa "tendo la kukutana kimwwili", kwa muundo wa hiki choo hasa kwa wale wenye miguu mirefu kamwe huwezi kujisikia starehe..hapa hata kupata huduma ya bafu (kuoga) mtu mmoja ni shida sana, ukiwa na mwenzio ushamwaga maji chumba chote, ...khaa..hakuna hata sehemu ya kupigia mswaki...