Kweli usimdharau mtu.

Kweli usimdharau mtu.

Wakati naanza maisha kuna jamaa kazini tena juniors kwangu walikua wananitishia maisha sana "nakaa kwangu nimejenga" siku nimewatembelea makwao ndio nikaona haya maisha usijipe pressure zisizo na msingi!
Unakuta mtu nyumba madirisha ameziba mabati makuukuu,chumba chenye mlango ni chake tu,choo mlango gunia,umeme na maji hana uhakika wa kupata leo wala kesho,ila anakutishia kwa vile umepanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo muda fulani nilichepuka niende kununua materials ya ujenzi pale Kamaka. Kwa wasiojua, Kamaka ni kampun ya Warusi wanauza vifaa vya ujenzi..Ni duka kubwa

Sasa wakati nimemaliza kila kitu wanapakia mzigo, tukawa tunapiga stori ya yule mtunza stoo pale, yupo mchafu mchafu hivi..Mimi hapo nimetoka kazini niko nadhifu vibaya mno sitaki hata vumbi linirukie..

Sasa badae wakati naondoka nikawa napiga stori na walionibebea mzigo kwenye gari wakawa wanasema hili gari(canter) ni la yule dogo pale. Nikauliza dogo gani wakasema yule storekeeper pale..

Daaah! nduo stori zikaanza hapo kuwa dogo ni darasa la saba tuu na mshahara wake ni milioni 2.8, ana hizo 3 za kubeba mizigo na mambo mengine kibao. Wakawa wanasema Mrusi haajiri wenye elimu kubwa kwenye vitengo hivyo, akasema wapo wengi tu humu darasa la saba

Akanambia unamwona mlinzi yule ana nyumba 3. Nikasema haiwezekan, akasema subiri akamwita akamwambia oya nyumba ya Kivule ushamaliza, akasema ipo kwenye madirisha. Basi poa nataka panga nyumbani kwako kabsa, ile nyumba ya ....,akamwambia,ya ngap sasa hiv hyo kiutan,akasema mungu ni mwema ya 3.

Nkasema ama kweli....

Uzi tayar

Sent using Jamii Forums mobile app
Yupi,erick au

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati naanza maisha kuna jamaa kazini tena juniors kwangu walikua wananitishia maisha sana "nakaa kwangu nimejenga" siku nimewatembelea makwao ndio nikaona haya maisha usijipe pressure zisizo na msingi!
Unakuta mtu nyumba madirisha ameziba mabati makuukuu,chumba chenye mlango ni chake tu,choo mlango gunia,umeme na maji hana uhakika wa kupata leo wala kesho,ila anakutishia kwa vile umepanga

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo alizingua snaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na kwanini umdharau mtu??? Me nashangaa sana sisi watu tulivyo wa ajabu,utamsikia mtu anasema usimdharau usiye mjua ina maana unayemjua ndio umdharau???maisha tunategemeana sana na hakuna wa muhimu zaidi kuliko mwenzie..USIMDHARAU yeyote chini ya jua hili,.full stop.

Komenti tayari.
Ngoja nijaribu kumtetea mleta maada.
Wakuu, iko hivi watu tunaojuana hua tumezoeana sana ama kidogo. Hivyo basi hua tunaheshimiana kulingana na hadhi zetu katika jamii tunayoishi. Hapa mwenye pesa, cheo, ushawishi (mfano mpigisha stori mzuri kwenye kahawa), taaluma n.k.

Utakuta mzee akisalimiana na kijana mwenye kauwezo flani, anakusanya mikono pamoja kuonyesha heshima wakati huohuo Huyo mzee akisalimiana na mwanae hakusanyi mikono wala kuonyesha unyenyekevu.

Ndugu zetu waliotuzidi umri tunawapa shikamoo, lakini tukikutana na tusiowajua wenye umri sawa na ndg zetu hua tunawaambia, "habari yako n.k"!

Hivyo sio ajabu kuona hatuheshimu tusiowajua (japo wapo wanaoheshimu kila mtu, namimi nimo ) maana hatujui wana nini, cheo, taaluma, hela, n.k.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni levo mkuu.... kwa mtazamo wako ukijilinganisha na ww huyo dogo katusua kukuzidi ww na kibarua chako....lkn kumbuka humu JF akina Gullam wamiliki wa viwanda wamo.....

Laiti angalijua wakati mwingine anajibiwa text na figures kubwa hatari na wakati mwingine anawatukana, we acha tu.... wakivaaga suti huwa wanaona wao ni kila kitu, haki ya nani!
 
Mkuu humo kwenye magodown na maviwanda kuna dili zinapigwa za kufa mtu huwezi jua kuna mmoja ni mfanyakazi wa kawaida kiwanda kimoja kipo mbezi beach ana nyumba 2 za maana ana gari mbili za kutembelea (ila kazini haendi nazo anapanda daladala) anasomesha mtoto shule ya bei m 2 kwa mwaka take home yake ni laki 6 na hajawahi kopa bank can you imagine
 
Back
Top Bottom