hunchback
JF-Expert Member
- Nov 10, 2014
- 658
- 289
Hivi kizazi cha sasa watoto wetu tunawaleaje? Leo mjini Morogoro mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 6 aliwaduwaza watu waliokuwa ibadani baada ya kuvua nguo na kujisaidia haja ndogo katikati ya umati wa watu waliokuwa wamekusanyika kwa ajili ya mnada. Kitu kilichozua mshangao ni kuwa mtoto huyu hakuonyesha chembe ya uoga baada ya kumaliza haja na kwenda alipokuwa mamaye huku akicheka. Hivi ni kweli mtoto wa miaka sita anashindwa kumuambia mamaye nataka kujisaidia. Ni malezi gani tunawapa watoto wetu?