mkapa kaua, jamani baba wa taifa.
haya sisahngai kwa jibu lako..mimi nataka nikupe crediti zako wewe unapanic..ni wasi sio wewe nimeshapata jibu. asante kwa kuileta jamvini.
Mkapa atakuwa aliomba kujumuisshwa kwenye ukoo wa Nyerer kwa lengo la kujisafisha
MWENYEKITI Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, ni mmoja wa wana ukoo wa Nyerere Burito.
Mkapa alipewa heshima hiyo mwanzoni mwa miaka ya 2000, baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sherehe za kumtambua rasmi kama mwana ukoo zilifanyika nyumbani kwa marehemu Chifu Edward Wanzagi Nyerere, kijijini Butiama.
Juzi, Mkapa amesikika akimshambulia Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema), wakati akizindua kampeni za CCM za Uchaguzi Mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki. Mkapa akasema amefanya kazi na Mwalimu, amemzika, hajawahi kusikia Mwalimu Nyerere ana mtoto wake mwenye jina kama hilo. Akasema inawezekana huyo analitumia ajinufaishe kisiasa.
Baada ya kumsikia Mkapa kwa makini, nimeamua kuzungumza na Vincent Nyerere. Naye akaonyesha mshangao wake. Akajiuliza inakuwaje mwana ukoo mwenzake (Mkapa) amshambulie kwa sababu tu ya jina. Tena nikajiuliza, ilikuwaje siku ile alipokaribishwa rasmi kwenye ukoo, hakuhoji, mbona huyu Chifu anajitangaza kuwa mtoto wa Baba wa Taifa? Najua hakuhoji kwa sababu anajua kuwa Chifu Edward Wanzagi, baba yake ndiye huyo huyo baba yake Kambarage, yaani Nyerere.
Baada ya kutafakari, nimeona nijaribu kuweka sawa haya mambo. Kwanza nianze na ukoo huu wa Nyerere. Lakini haitakuwa vema kuuanza ukoo huu bila kumhusisha Mwalimu kwanza.
Kwa ufupi ni kwamba jina la Baba wa Taifa ni Julius Kambarage Nyerere. Jina Julius ni la ubatizo. Jina Kambarage ni la asili lenye maana ya mzimu wa mvua. Jina Mwalimu lilitokana na kazi yake ya ualimu. Kama walivyo walimu wengi, alipenda kuitwa Mwalimu badala ya Mheshimiwa au Dokta. Tena kwa wasiojua, jina la kwanza kabisa la Mwalimu Kambarage lilikuwa Mgendi, lenye maana ya mtembezi kwa lugha ya Kizanaki. Kwa nini wazazi wake waliliondoa jina hilo na kumpa jina la Kambarage, huo ni mjadala mwingine ambao nikiombwa nitauzungumzia.
Hivyo basi, mtiririko wa jina lake ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Burito Mazembe Wisigana Tandari. Hii ina maana kwamba Kambarage alizaliwa na Nyerere. Nyerere (Baba yake Mwalimu) alizaliwa na Burito. Burito alizaliwa na Mazembe. Mazembe alizaliwa na Tandari. Orodha ni ndefu.
Hadi hapo, utaona kuwa Nyerere si jina la Mwalimu. Bali jina lake ni Kambarage Nyerere, ikiwa na maana kwamba Nyerere ni ndiye baba yake mzazi. Ni kama leo kuna kina Mkapa wengi, hiyo haina maana kwamba wanaotumia jina hilo wanataka kujitanabahisha kuwa ni watoto wa Mkapa yule ambaye ni Rais Mstaafu. Unaweza kuuliza, iweje watoto wa Mwalimu waitwe majina kama Burito (Andrew) Nyerere, Anna (Watiku) Nyerere, Emil (Magige) Nyerere, Makongoro (Charles) Nyerere, John (Guido) Nyerere, Pauleta Nyerere, Madaraka (Godfrey) Nyerere au Rosemary Nyerere?
Matumizi ya jina Nyerere yamekuwa makubwa kwa sababu ni jina la ukoo. Ni jina kama yalivyo majina makubwa ya kina Mkwawa, Makongoro, na kadhalika. Hao watoto wa Mwalimu hawakutumia jina Nyerere kama jina la baba yao, bali ni la babu yao, yaani Nyerere Burito. Unaweza kusema Nyerere alikuwa maarufu, lakini aliyelipa umaarufu zaidi ni Mwalimu Kambarage.
Ni sahihi Makongoro akaitwa Makongoro Kambarage, Burito Kambarage, Madaraka Kambarage, Rosemary Kambarage, Magige Kambarage, Nyerere Kambarage, na kadhalika. Nadhani hadi hapo tupo pamoja.
Je, huyu Kambarage Nyerere hakuwa na ndugu wa tumbo moja? Alikuwa nao. Baadhi yao ni Nyangete Nyerere, Nyakahu Nyerere, Nyakigi Nyerere, Kizurira (Joseph) Nyerere na kitindamimba katika tumbo la Bibi Mgaya (Christina) Nyangombe (mama wa wote hawa) ni Kiboko (Josephat Nyerere). Kitindamimba huyu alifariki dunia miaka ya karibuni kabisa. Mkapa alihudhuria mazishi yake kijijini Butiama.
Huyu huyu, Josephat Kiboko Nyerere (kitindamimba katika tumbo la Bibi Mgaya), naye kapata watoto wengi. Hapa siwezi kuwaorodhesha wote. Lakini miongoni mwao ni VINCENT NYERERE KIBOKO NYERERE.
Wazanaki ni watu wanaoheshimu mila. Kurithishana majina ni moja ya mambo muhimu sana kwa Wazanaki. Ndiyo maana alipozaliwa huyu (mbunge), baba yake (yaani Kiboko Nyerere) aliamua kumpa jina la Nyerere akiwa amempa heshima hiyo baba yake mzazi, yaani Mtemi Nyerere Burito aliyefariki dunia mwaka 1942. Alikuwa Mtemi wa Butiama. Kama mbunge huyu angeamua kutumia majina ya Kizanaki, angeitwa Nyerere Kiboko Nyerere. Alipoamua kutumia majina ya ubatizo, akaweka jina Vincent na akaongeza la kwake la kuzaliwa la Nyerere; hivyo jina lake likawa Vincent Nyerere. Angeweza kuweka kando jina la ubatizo akatumia jina la Nyerere J.K. Nyerere (Nyerere Josephat Kiboko Nyerere). Alichoamua kufanya ni kutumia jina la ubatizo na jina la kuzaliwa linalobeba jina lake na la ukoo, yaani la babu yake.
Ni kwa sababu hiyo, mgeni yeyote anayefika Butiama anaweza kupigwa bumbuwazi kwa kusikia jina Nyerere likitamkwa kama salamu. Hiyo ni kwa sababu jina Nyerere ni la ukoo, na si la Mwalimu Kambarage. Mwalimu ni sehemu ya ukoo huo.
Lakini jina la Nyerere leo limefika mbali zaidi. Kuna waigizaji wanaitwa kina Steven Nyerere, kuna Nyerere wengi sana kila kona ya Tanzania. Afrika ina kina Nyerere wengi. Marekani ndo usiseme kabisa! Hii haina maana kwamba wanaoitwa Nyerere wanataka kujitafutia umaarufu kwa kutumia jina la Mwalimu au wanataka wajulikane kuwa wamezaliwa na Mwalimu Kambarage. Hapana.
Kwa ufafanuzi huu nadhani mwana ukoo Mkapa atakuwa ametambua kuwa huyu mbunge kuitwa Vincent Nyerere si kwa sababu ya kutaka kujikweza, bali hilo ndilo jina lake halisi. Endapo atajiita Vincent Kambarage Nyerere, hapo ndipo tunaweza kusema anataka kujitambulisha kama mtoto wa Mwalimu. Na ni kweli kwamba Mwalimu Kambarage ni baba yake mkubwa Vincent Nyerere. Hilo halina mjadala.
Tunamkaribisha mwana ukoo Mkapa akutane na sisi wazee ndani ya ukoo ili tupate kumpa somo. Akumbuke kuwa Mwalimu akiwa hai alimweleza kuwa ukoo wa Burito ni mkubwa. Huo unajumuisha familia za Chifu Wanzagi, Kambarage, Jackton, Wisigana, Muhunda, Nyamboga, Daniel, Kizurira, Nyakigi, Nyabisenye na nyingine nyingi. Kwetu sisi, Vincent Nyerere ni mwana ukoo na mjukuu halisi wa Nyerere Burito Mazembe Wisigana Tandari. Hajawahi, na hatawahi kujinasibu kama mtoto wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ingawa ukweli ni kwamba kiongozi huyo ni baba yake mkubwa. Wazazi wao wametoka kwa baba mmoja na tumbo moja la mama. Kama kuna kitu nimekisahau, basi mwana ukoo mwingine asaidie kukiweka wazi.
Kwa hiyo ukoo ni Burito au ni Nyerere? Unajichanganya....Akumbuke kuwa Mwalimu akiwa hai alimweleza kuwa ukoo wa Burito ni mkubwa.
Kama jina la ukoo maana yake ni jina la babu then kila mtu ana babu yake, kwa hiyo Julius and Vincent being of different generations should never share a surname because they have different grandfathers! Kwa hiyo Vincent alijipachika jina la babu, sio la ukoo!Alichoamua kufanya ni kutumia jina la ubatizo na jina la kuzaliwa linalobeba jina lake na la ukoo, yaani la babu yake.
Well, kama kuna such thing as jina la ukoo na Nyerere ndio jina la ukoo, na kama kimila unaitwa jina lako na la ukoo basi baba yake mwalimu, yani Chifu Nyerere, alipozaliwa angeitwa Nyerere Nyerere, yani alilopewa na la ukoo. Lakini akaitwa Nyerere Burito, yani lake na la baba yake. Kama ambavyo Julius nae alipozaliwa akaitwa Kambarage Nyerere, yani lake na la baba yake. Kwa hiyo tuseme hao waliowatoga majina Julius na pia Chifu Nyerere walikuwa hawajui system za kutoga majina za kizanaki? Walikosea mara mbili?Matumizi ya jina Nyerere yamekuwa makubwa kwa sababu ni jina la ukoo..... kwa sababu jina Nyerere ni la ukoo, na si la Mwalimu Kambarage. Mwalimu ni sehemu ya ukoo huo.
Kwa hiyo Vincent sio mtoto wa Kambarage wala sio mtoto wa Nyerere, ni mtoto wa Kiboko....baba yake (yaani Kiboko Nyerere) aliamua kumpa jina la Nyerere akiwa amempa heshima hiyo baba yake mzazi, yaani Mtemi Nyerere Burito aliyefariki dunia mwaka 1942. Alikuwa Mtemi wa Butiama. Kama mbunge huyu angeamua kutumia majina ya Kizanaki, angeitwa Nyerere Kiboko Nyerere. Alipoamua kutumia majina ya ubatizo, akaweka jina Vincent na akaongeza la kwake la kuzaliwa la Nyerere; hivyo jina lake likawa Vincent Nyerere. Angeweza kuweka kando jina la ubatizo akatumia jina la Nyerere J.K. Nyerere (Nyerere Josephat Kiboko Nyerere). Alichoamua kufanya ni kutumia jina la ubatizo na jina la kuzaliwa linalobeba jina lake na la ukoo, yaani la babu yake.
Copy paste and save for future use
kwa hiyo ukoo ni burito au ni nyerere? Unajichanganya.
Kama jina la ukoo maana yake ni jina la babu then kila mtu ana babu yake, kwa hiyo julius and vincent being of different generations should never share a surname because they have different grandfathers! Kwa hiyo vincent alijipachika jina la babu, sio la ukoo!
Well, kama kuna such thing as jina la ukoo na nyerere ndio jina la ukoo, na kama kimila unaitwa jina lako na la ukoo basi baba yake mwalimu, yani chifu nyerere, alipozaliwa angeitwa nyerere nyerere, yani alilopewa na la ukoo. Lakini akaitwa nyerere burito, yani lake na la baba yake. Kama ambavyo julius nae alipozaliwa akaitwa kambarage nyerere, yani lake na la baba yake. Kwa hiyo tuseme hao waliowatoga majina julius na pia chifu nyerere walikuwa hawajui system za kutoga majina za kizanaki? Walikosea mara mbili?
Kwa hiyo vincent sio mtoto wa kambarage wala sio mtoto wa nyerere, ni mtoto wa kiboko.
Jina lake lilitakiwa liwe vincent kiboko, kama ambavyo mwalimu aliitwa julius nyerere, lake na la baba yake. Na kama ambavyo mwenyewe umekubali kwamba ingekuwa absolutely correct kwa andrew kuitwa andrew kambarage.
Kwa nini umruke babaako mzazi ukajiite jina la babu mwanzisha ukoo ambae wengi wetu hatujui aliishi lini na wapi, alifanya nini maishani, kwa nini ana ujiko wa sisi kuchukua jina lake, yeye mwenyewe jina lake la ukoo ni nani, kwa nini tuanzie kwake, na kwa nini baba yangu aliyenifikisha hapa nilipo asahaulike?
Utaona mwalimu hakuitwa last name ya burito ambayo ndio babu yake, kwa sababu alikuwa proudful na baba yake, akajiita julius nyerere. Kwa hiyo kuna sababu za wazi za kusadiki kwamba vincent is shying away from "kiboko" as his surname.
!Kama jina la ukoo maana yake ni jina la babu then kila mtu ana babu yake, kwa hiyo Julius and Vincent being of different generations should never share a surname because they have different grandfathers
Vicent Nyerere amemlipua Msajili wa Vyama vyaSiasa, John Tendwa, kwa kimzuia kumzungumzia Hayati Mwalimu Nyerere.
Amemshauri kuwa kama anahitji kuwa mmoja wa familia yao, anaruhusiwa kuandika barua kuomba kujiunga na ukoo wao kama alivyofanya Mkapa......Gazeti la Nipashe
MWENYEKITI Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, ni mmoja wa wana ukoo wa Nyerere Burito.
Mkapa alipewa heshima hiyo mwanzoni mwa miaka ya 2000, baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sherehe za kumtambua rasmi kama mwana ukoo zilifanyika nyumbani kwa marehemu Chifu Edward Wanzagi Nyerere, kijijini Butiama.
......
utaratibu huu wa kutumia surname ulikuja wakati wa wakoloni, kabla ya hapo ndio hizo system ya mtu kuitwa jina la baba yake, na mtoto au mjukuu kupewa jina la babu yake, kama ulivyo sema mfano Emil kambarage, lakini hapo hapo Emil angeweza kupewa jana la Nyerere au Nyakigi nk kama hishima ya hao wakubwa wa Kambarage kama wajomba zake, Baba yake ambaye atakuwa ni Babu kwa Emil nk, sasa katika hiyo transition ya ku-adopt jina moja kuwa la ukoo kulitokea mchanganyiko huo wa jina la ukoo pia kupewa watu binafsi katika koo hizo hizo wakifuata mila na desturi zao za zamani, na hii si huko tu zanaki au musoma na kwingineko, hata wewe ukiuliza asili ya jina la ukoo wako utakuta kuna hitilifu hizo. sababu za kufuata mfumo huo wakoloni waliona wakati ule kutokana na kutukuweko kwa kumbukumbu watu wengi ndugu walipotezana, baada ya kuhama au kwenda vitani. leo chukulia mtu wa ukoo wa mkapa, tuseme walizaliwa watano, lakini kama ilivyo kuwa desturi za wakati huo kila moja akatukuza hilo jina la baba yake bila kuweka kina saba cha babu, halafu watu hao hao wakatoka machinga mwingine akaenda kilwa na labda huko akao, kama alikuwa mkristo kule kilwa akapata binti wa sheikh hivyo akabadili jina na wengine kwa heshima ya sheikh aliye mfungisha ndoa akawekeza na jina la sheikh , unafikiri baada ya muda watoto wake watawajua ndugu zao wa machinga, na hapo ni moja tu aliye kwenda kilwa, hapo hapo waweza kukuta dada kaolewa msumbiji, mwingine alikwenda malawi, mwingine alikwenda shinyanga kwenye machimbo au morogoro kama manamba, mwingine alikwenda burma kwenye vita kuu. je watu hawa baada ya muda wataunganika vipi? haya ndio yalikuwa nimatatizo yetu.Kwa hiyo ukoo ni Burito au ni Nyerere? Unajichanganya.
Kama jina la ukoo maana yake ni jina la babu then kila mtu ana babu yake, kwa hiyo Julius and Vincent being of different generations should never share a surname because they have different grandfathers! Kwa hiyo Vincent alijipachika jina la babu, sio la ukoo!
Well, kama kuna such thing as jina la ukoo na Nyerere ndio jina la ukoo, na kama kimila unaitwa jina lako na la ukoo basi baba yake mwalimu, yani Chifu Nyerere, alipozaliwa angeitwa Nyerere Nyerere, yani alilopewa na la ukoo. Lakini akaitwa Nyerere Burito, yani lake na la baba yake. Kama ambavyo Julius nae alipozaliwa akaitwa Kambarage Nyerere, yani lake na la baba yake. Kwa hiyo tuseme hao waliowatoga majina Julius na pia Chifu Nyerere walikuwa hawajui system za kutoga majina za kizanaki? Walikosea mara mbili?
Kwa hiyo Vincent sio mtoto wa Kambarage wala sio mtoto wa Nyerere, ni mtoto wa Kiboko.
Jina lake lilitakiwa liwe Vincent Kiboko, kama ambavyo mwalimu aliitwa Julius Nyerere, lake na la baba yake. Na kama ambavyo mwenyewe umekubali kwamba ingekuwa absolutely correct kwa Andrew kuitwa Andrew Kambarage.
Kwa nini umruke babaako mzazi ukajiite jina la babu mwanzisha ukoo ambae wengi wetu hatujui aliishi lini na wapi, alifanya nini maishani, kwa nini ana ujiko wa sisi kuchukua jina lake, yeye mwenyewe jina lake la ukoo ni nani, kwa nini tuanzie kwake, na kwa nini baba yangu aliyenifikisha hapa nilipo asahaulike?
Utaona mwalimu hakuitwa last name ya Burito ambayo ndio babu yake, kwa sababu alikuwa proudful na baba yake, akajiita Julius Nyerere. Kwa hiyo kuna sababu za wazi za kusadiki kwamba Vincent is shying away from "Kiboko" as his Surname.
Kutokana na nlichokipata hapo juu toka kwa mtoa mada ni kwamba Mkapa alisema hajawahi sikia kama kuna mtu anaitwa Vincent Nyerere kwenye familia ya Mwalimu Nyerere; kama ilikua hivyo na kulingana na ufafanuzi wa namna ukoo wa Nyerere ulivyo basi sioni kama Mkapa alikosea kwa kauli hiyo lkn kama angesema hajawahi sikia jina hilo kwenye ukoo au Familia ya Nyerere basi hapo mtu mzima angekua ameteleza; Kwa mantiki hiyo basi ukweli wabak kuwa Vincent Nyerere ni mtoto wa Nyerere na si mtoto wa Mwl.JKN
Ngoja kwanza, haiwezekani kusema mtu anaitwa jina la baba yake na mtoto anapewa jina la babu yake, ina maana huyo "mtoto" wakati anazaliwa hakuwa "mtu"?utaratibu huu wa kutumia surname ulikuja wakati wa wakoloni, kabla ya hapo ndio hizo system ya mtu kuitwa jina la baba yake, na mtoto au mjukuu kupewa jina la babu yake,
Namkumbuka kiboko (josephat) nyerere alisumbua sana pale musoma mjini.