Kweli Mkapa kalidanganya taifa, ona hapa jinsi Vicent Nyerere alivyo mtoto wa ukoo wa Nyerere

!


Kweli rafiki yangu aliwahi kunambia kuwa, hapa JF kuna washambuliaji na wachambuzi. Anhe User U'r the later. :hand:

Ni kweli, jamaa kafafanua vizuri lakini mtu mwingine anakuja na utumbo wa ajabu ajabu. Kwa wa huko actually hakuna tofauti ya mtoto wa Kambarage na Mtoto wa Kiboko. wote ni wa ukoo wa Nyerere. Madaraka si wa ukoo wa Nyerere kumzidi Vincenti. La baba wa madaraka kuwa raisi linamwongezea ujiko tu lakini mila zinabaki pale pale.
 
Shukrani kaka ukoo wa Nyerere ni mkubwa sana,huyo mbunge ana dada zake pia wako Italia na majina yao utakuta kwa mfano akina Watiku ,Rose wako kibao hapo kwenye ukoo wa Nyerere ,hata huyo mwandishi wa habari anaitwa Jacton Manyerere naye ni mwana ukoo huo huo ,hakika ukoo wa Nyerere (sio)Kambarage ni mkubwa mno tena mno na wametapakaa si Butiama tu bali duniani kote ,utakuta wajukuu nao wanatumia jina la Nyerere
 
Habari hii nimeipenda shukrani kwa aliyetufafanulia kuhusu ukoo wa Nyerere,na kwa kuwa huu ukoo ni maarufu na mwadilifu(hauna chembe hata moja ya ufisadi na ukopi na kuuhifadhi ili uwe mmoja wa nyaraka za kumbukumbu katika maktaba yangu,kwani si ajabu akatokea MWEHU mwingine akaja kuleta UONGO wake ,ili kumsuta kwa uongo wake tutamwekea huu waraka ili ajione kuwa yu mwehu
 
MWENYEKITI Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, ni mmoja wa wana ukoo wa Nyerere Burito.
Mkapa alipewa heshima hiyo mwanzoni mwa miaka ya 2000, baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sherehe za kumtambua rasmi kama mwana ukoo zilifanyika nyumbani kwa marehemu Chifu Edward Wanzagi Nyerere, kijijini Butiama.

Juzi, Mkapa amesikika akimshambulia Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema), wakati akizindua kampeni za CCM za Uchaguzi Mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki. Mkapa akasema amefanya kazi na Mwalimu, amemzika, hajawahi kusikia Mwalimu Nyerere ana mtoto wake mwenye jina kama hilo. Akasema inawezekana huyo analitumia ajinufaishe kisiasa.

Sasa kwanini wakati anaingizwa kwenye ukoo haukupewa shule hii?Mpaka anaanza kuropoka vitu asivyovifahamu!Tafuta namna kampe hii shule BWM!Ameshatia dosari kampeni nawananchi kwaujumla!
 
Asante kwa kutufafanulia juu ya ukoo wa Nyerere. Namkumbuka Beatrice Nyerere (R.I.P), alikuwa mtangazaji wa RFA wakati tu ndo inaanza pale Mwanza, hata baada ya kuolewa bado alijiita Beatrice Masandika Nyerere (R.I.P Masandika), na Julius Kambarage alikuwa ni babake mkubwa tu lakini wengi walikuwa wanajua ni mtoto wa kuzaliwa wa Julius kwasababu ya jina Nyerere
 
Che Nkapa ametusaidia kuijua historia ya ukoo wa Mwalimu Nyerere, ingawa tume learn in a hard way...

Bado majibu kuhusu Mkapa kumuua Nyerere, Je ni kweli walikuwa wametofautiana kuhusu ubinafishaji? Na je ni kweli kama ukoo mlikataa asipelekwe Uingereza kwa kuwa waingereza walikuwa na bifu naye ya kulete uhuru, Mkapa akalazimishwa aende huko kutimiza Conspiracy theory??? Tujuze kiongozi wa ukoo

Kuhusu penye rangi ya blue, jibu ni KWELI. Kuthibitisha hili, hebu katafute na kuisikiliza/kuisoma hotuba ya Mwalimu JK Nyerere, ya Mei Mosi 1996 pale katika Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Utajua msimamo wa Nyere juu ya sera ya Ubinafsishaji ilivyokuwa.
 
Ngoja kwanza, haiwezekani kusema mtu anaitwa jina la baba yake na mtoto anapewa jina la babu yake, ina maana huyo "mtoto" wakati anazaliwa hakuwa "mtu"?

Mpaka hapo ushachemka vibaya sana, hueleweki.

Hoja yangu ilikuwa ni kwamba mtaalam wa majina ya kizanaki ameshindwa kueleza kwa nini Julius Nyerere alitumia last name ambayo ni jina la baba yake, na kwa nini baba yake Julius, yani Nyerere Burito, nae pia alitumia last name ambayo ni jina la baba yake, badala ya Nyerere, kama Nyerere ndio jina la ukoo.

You are a confuser who is already confused. Taratibu za koo za watu zitabaki na kuhemiwa nao bila confusion
 
Ahsante mtoa mada. Ila avatar yako na jina unalotumia ni mkuki moyoni mwangu
 
Sasa hapo nimetambua katika ukoo wa Nyerere, ni nani aliyekaribisha na nani aliyekaribishwa; kati ya Vincent Kiboko Nyerere na Benjamin Mkapa Nyerere
 
@MAGAMBA MATATU: Ni matumaini yangu kuwa bado unanitafutia majibu ya maswali yangu kama yalivyo katika post# 35 ya uzi huu.
 
Che Nkapa ametusaidia kuijua historia ya ukoo wa Mwalimu Nyerere, ingawa tume learn in a hard way...

Bado majibu kuhusu Mkapa kumuua Nyerere, Je ni kweli walikuwa wametofautiana kuhusu ubinafishaji? Na je ni kweli kama ukoo mlikataa asipelekwe Uingereza kwa kuwa waingereza walikuwa na bifu naye ya kulete uhuru, Mkapa akalazimishwa aende huko kutimiza Conspiracy theory??? Tujuze kiongozi wa ukoo

Nadhani hutegemei jibu kutoka kwa magamba matatu kwenye hili, ukizingatia uzito wa tuhuma yenyewe. Wote tuliokuwa tunafuatilia hotuba za mwishoni mwishoni mwa uhai wake, mfano MEI MOSI 1999 MBEYA, kama sijakosea mwaka, lakini hotuba ile naweza kuikariri neno kwa neno vipengele ambavyo yeye hakupendezwa navyo katika utendaji wa serikali ya Benja hasa suala la ubinafsishaji wa mashirika ya umma. Mwenye ubavu wa kurusha kombora mtindo huu ni mwanafamilia kama Vincent, na kuishia kuambiwa hana adabu, lakini MESSAGE DELIVERED! HUREEEEEE VINCENT. Umetusemea wengi na sasa tumepumua!
 
Umenena: Mkapa akasema amefanya kazi na Mwalimu, amemzika, hajawahi kusikia Mwalimu Nyerere ana mtoto wake mwenye jina kama hilo.

Inaonyesha Mkapa alimaanisha si BLOOD SON wa Kambarage ambavyo natumaini ni kweli ingawa Vincent ni mwana ukoo wa Nyerere.
Hiyo ni hisia yako! Hakuna mahali popote katika hotuba ile ya Benja palionesha hisia hiyo! Moja kwa moja yeye Benja alidhani Vincent kajiita jina la Nyerere kujitwika uzito wa Marehemu Baba wa Taifa, lakini si miongoni mwao! Usafwani ni kitu cha Kawaida kuwasikia watu Wakiitwa majina ya Kiislamu, kama Kassim. Rajab, n.k lakini ni WAPENDA MAJINA TU, WAO wanaweza kuwa wakristo au, wapagani
lakini si LAZIMA AWE MWISLAMU!
Hiyo ndo hisia aliyokuwa nayo BENJA!
 
Tunataka tu kujua nu kwweli amemuua baba yake makongoro, ili tupate pa kuanziaQUOTE=Skills4Ever;3519180]Che Nkapa kaombe radhi....umechemka mazima!!!![/QUOTE]
 
Ze kila of ze faza wa taifa
Hiyo ni hisia yako! Hakuna mahali popote katika hotuba ile ya Benja palionesha hisia hiyo! Moja kwa moja yeye Benja alidhani Vincent kajiita jina la Nyerere kujitwika uzito wa Marehemu Baba wa Taifa, lakini si miongoni mwao! Usafwani ni kitu cha Kawaida kuwasikia watu Wakiitwa majina ya Kiislamu, kama Kassim. Rajab, n.k lakini ni WAPENDA MAJINA TU, WAO wanaweza kuwa wakristo au, wapagani
lakini si LAZIMA AWE MWISLAMU!
Hiyo ndo hisia aliyokuwa nayo BENJA!
 
wewe huna hoja...
Unajua kweli mana ya surname? Kanywe uji....

April 13, 1922 Chief Nyerere alipata mtoto akampa jina Kambarage.
Alipoandikishwa shuleni mwaka 1934 pale Mwisenge aliitwa Kambarage Nyerere.

Kambarage Nyerere aliamua kubatizwa mwaka 1945 na kuwa mkatoliki akapewa jina jipya Julius. Chief Nyerere amefariki miaka ya 1940 na na inawezekana jina Julius la mwanae hakuwahi kulitamka.

Hivyo, majina halis yake ni Julius Kambarage. Nyerere ni la baba yake.

Josephat Kiboko ni majina ya kitinda mimba wao Julius Kambarage. Kiboko alipomzaa mtoto akamuita jina Nyerere.
Nyerere alipobatizwa akaitwa jina Vincent. Hivyo, huyu ana majina mawili ya kwake yaani Vincent Nyerere.

Kama Julius na Vincent wasingebatizwa basi wangeitwa Kambarage Nyerere na huyu wa CHADEMA angaitwa Nyerere Kiboko.

Kumjua kwenue Julius kuliko wengine hiyo ni shauri yenu lakini huu ndiyo ukweli kwamba mwenye kulitumia jina Nyerere kama lake ni huyu wa CHADEMA na si Julius Kambarage.
 
Back
Top Bottom