Kiongozi na Mwanafalsafa nguli wa itikadi ya ukombozi wa bara la Africa, Kamarade Amilcar Cabral aliamini kuwa mafanikio ya mapambano ya ukombozi yatategemea sana nidhamu binafsi (Personal Moral Behaviour), uungwana (Dignity) na uaminifu (Honesty) wa viongozi wa mapambano hayo na wafuasi wake.
Na katika kuangalia mafanikio na matatizo mengi yaliyolikumba bara la frika miaka hamsini baada ya uhuru, wasomi kadhaa wametanabaisha kuwa ukosefu nidhamu binafsi, uungwana na uaminifu miongoni mwa viongozi waliopo na wale wanaotarajiwa kuchukua nafasi za waliopo pamoja na jamii kwa ujumla ni moja ya sababu kubwa za tatizo la ombwe la uongozi linalodidimiza bara letu hivi sasa.
Tangu na baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 kufanyika hapa nchini, chama cha CHADEMA kimejitanabaisha na mambo mengi mengi ambayo yameweza kuendeleza na kujenga hamasa kubwa zaidi miongoni mwa mashabiki wao na pia kuzua maswali kadhaa miongoni mwa watanzania wengine. Lilianza lile la kumsumsia na kutomtambua rais Kikwete, likaja la vita vya kumsulubu kisiasa Naibu Katibu Mkuu wao Kabwe Zitto, likaja la maandamano ya Arusha yaliyopelekea mauaji ya watu watatu ambao wote kwa pamoja wakapewa hadhi ya uhanga wa kile kinachoitwa Mapambano ya Demokrasia na sasa hili la mazishi ya kizalendo ya wahanga hao wawili. Wapo wanaosema kuwa haya ni moja ya mambo ya kawaida kujitokeza pale mafanikio yanapozidi kiwango matumaini na wapo wanaosema kuwa hiyo ni sura halisi ya haiba, fikira na dhima zinazotawala chama hicho.
Katika suala la maziko ya kizalendo ya waliohadhiwa kama wahanga wa maandamano hayo nimekuwa najiuiliza sana maudhui na mantiki mazima ya uhanga wa Marehemu Dennis Michael. Hii inatokana na taarifa kuwa wakati ni kweli Marehemu Ismail alikuwa ni mmoja wa waandamanaji , taarifa kutoka ndani ya familia ya Dennis Michael zinadai kuwa kijana wao Dennis hakuwa ameshiriki katika maandamano hayo bali alikuwa mpita njia katika eneo alilouawa akielekea kuchukua gari la jamaa yake mmoja baada ya kupigiwa simu muda mchache kabla ya tukio hilo. Wanaendelea kudai kuwa kamwe Dennis hakuwahi kushiriki katika mambo ya siasa na hata siku hiyo alikuwa akilalamika sana kuhusu uamuzi huo wa Chadema kukimbilia hatua ya maandamano ambayo yangeleta machafuko.
Kutokana na taarifa hizo imenibidi nijiulize hivi inakuwaje Marehemu Denis akawa mhanga wa mapambano ya demokrasia kama yalivyoitwa na Chadema na washabiki wao? Hivi nini maana ya mhanga wakati anayepewa hadhi hiyo hakuwa miongoni mwa waandamanaji na alipatwa na dharuba hiyo bila ya hatia yoyote? Lakini zaidi najiuliza, hivi Chadema hawakujua hili ama waliamua kufunika kombe ili uharamia upite? Lakini zaidi, ni kwa nini ndugu zake hawakuwa wakali kulinda haki yake ya kiutu na kumuacha Dennis kutumika kama turufu ya kisiasa?
Lakini zadi inanileta katika suala zima la hulka ya viongozi wetu wa kisiasa ambao wako tayari kutumia kila njia kuweza kufanikisha mradi wao wakati mwengine bila ya kujali misingi rahisi ya utu kama vile uungwana na uaminifu kwa unaoamini kuwa unawatumikia.
Ukweli ni kuwa pamoja na kuhoji uhalali wa kumtangaza Marehemu Dennis kama mhanga na kumtumia kufanikisha malengo ya kisiasa ambayo kwa kiasi fulani Chadema wamefanikiwa lakini pia hili linanileta katika kuamini kuwa tatizo la uongozi usioamini katika umuhimu wa nidhamu binafsi, uungwana na pia uaminifu ni kubwa kuliko tudhaniavyo. Na ubaya zaidi ni hali ya wengi wetu (raia) kuwa tayari kuyafumbia macho na kuyakumbatia mapungufu hayo sasa tukijidanganya kuwa kufanya hivyo kutatusaidia kuondokana na tatizo la sasa (CCM) huku tukisahau kuwa kuna zaidi ya sasa huko tuendako (Tanzania).
Na katika kuangalia mafanikio na matatizo mengi yaliyolikumba bara la frika miaka hamsini baada ya uhuru, wasomi kadhaa wametanabaisha kuwa ukosefu nidhamu binafsi, uungwana na uaminifu miongoni mwa viongozi waliopo na wale wanaotarajiwa kuchukua nafasi za waliopo pamoja na jamii kwa ujumla ni moja ya sababu kubwa za tatizo la ombwe la uongozi linalodidimiza bara letu hivi sasa.
Tangu na baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 kufanyika hapa nchini, chama cha CHADEMA kimejitanabaisha na mambo mengi mengi ambayo yameweza kuendeleza na kujenga hamasa kubwa zaidi miongoni mwa mashabiki wao na pia kuzua maswali kadhaa miongoni mwa watanzania wengine. Lilianza lile la kumsumsia na kutomtambua rais Kikwete, likaja la vita vya kumsulubu kisiasa Naibu Katibu Mkuu wao Kabwe Zitto, likaja la maandamano ya Arusha yaliyopelekea mauaji ya watu watatu ambao wote kwa pamoja wakapewa hadhi ya uhanga wa kile kinachoitwa Mapambano ya Demokrasia na sasa hili la mazishi ya kizalendo ya wahanga hao wawili. Wapo wanaosema kuwa haya ni moja ya mambo ya kawaida kujitokeza pale mafanikio yanapozidi kiwango matumaini na wapo wanaosema kuwa hiyo ni sura halisi ya haiba, fikira na dhima zinazotawala chama hicho.
Katika suala la maziko ya kizalendo ya waliohadhiwa kama wahanga wa maandamano hayo nimekuwa najiuiliza sana maudhui na mantiki mazima ya uhanga wa Marehemu Dennis Michael. Hii inatokana na taarifa kuwa wakati ni kweli Marehemu Ismail alikuwa ni mmoja wa waandamanaji , taarifa kutoka ndani ya familia ya Dennis Michael zinadai kuwa kijana wao Dennis hakuwa ameshiriki katika maandamano hayo bali alikuwa mpita njia katika eneo alilouawa akielekea kuchukua gari la jamaa yake mmoja baada ya kupigiwa simu muda mchache kabla ya tukio hilo. Wanaendelea kudai kuwa kamwe Dennis hakuwahi kushiriki katika mambo ya siasa na hata siku hiyo alikuwa akilalamika sana kuhusu uamuzi huo wa Chadema kukimbilia hatua ya maandamano ambayo yangeleta machafuko.
Kutokana na taarifa hizo imenibidi nijiulize hivi inakuwaje Marehemu Denis akawa mhanga wa mapambano ya demokrasia kama yalivyoitwa na Chadema na washabiki wao? Hivi nini maana ya mhanga wakati anayepewa hadhi hiyo hakuwa miongoni mwa waandamanaji na alipatwa na dharuba hiyo bila ya hatia yoyote? Lakini zaidi najiuliza, hivi Chadema hawakujua hili ama waliamua kufunika kombe ili uharamia upite? Lakini zaidi, ni kwa nini ndugu zake hawakuwa wakali kulinda haki yake ya kiutu na kumuacha Dennis kutumika kama turufu ya kisiasa?
Lakini zadi inanileta katika suala zima la hulka ya viongozi wetu wa kisiasa ambao wako tayari kutumia kila njia kuweza kufanikisha mradi wao wakati mwengine bila ya kujali misingi rahisi ya utu kama vile uungwana na uaminifu kwa unaoamini kuwa unawatumikia.
Ukweli ni kuwa pamoja na kuhoji uhalali wa kumtangaza Marehemu Dennis kama mhanga na kumtumia kufanikisha malengo ya kisiasa ambayo kwa kiasi fulani Chadema wamefanikiwa lakini pia hili linanileta katika kuamini kuwa tatizo la uongozi usioamini katika umuhimu wa nidhamu binafsi, uungwana na pia uaminifu ni kubwa kuliko tudhaniavyo. Na ubaya zaidi ni hali ya wengi wetu (raia) kuwa tayari kuyafumbia macho na kuyakumbatia mapungufu hayo sasa tukijidanganya kuwa kufanya hivyo kutatusaidia kuondokana na tatizo la sasa (CCM) huku tukisahau kuwa kuna zaidi ya sasa huko tuendako (Tanzania).