S.N.Jilala
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 540
- 507
Nimeskitishwa sana na hotuba ya mkuu wa nchi alivyoongelea kuhusu mauaji yanayofanyika kwenye mikutano ya wapinzani. Kwanza kitendo cha kuonyesha dhahiri wanaosababisha mauaji ni wapinzani na siyo polisi. Pili kutoonyesha dhahiri nia ya kukomesha mauaji yanayotokea na kusema Chama flani hakitaki watu wengine wahuzurie kwenye mikutano yao na kufanya mauaji. Tatu kuhubiri amani wakati hauonyeshi kufikia mwafaka sahihi. Nne, Kuonyesha dhahiri kuwa upinzani ndiyo unasababisha machafuko. Mawazo yangu, kwanza kiongozi mzuri niyule anayetumia muda wake kusululisha badala ya kuonyesha au kulaumu waziwazi upande mwingine. Pili, ivi tunasahau kuwa hata hii katiba yetu inaruhusu kuandamana kwa amani. Mwisho,nina wasiwasi kama kuna suluhu tuendako, wananchi tutazidi kuuwawa kama wanyama. Pia, viongozi wetu wachukue hatua kukomesha mauaji kwa njia ya maelewano na siyo kulaumu upande mwingine tu.