Kwaya ya CCM yahamia CHADEMA

Kwaya ya CCM yahamia CHADEMA

Watatusaidia kutupa nyimbo mpya za uamasishaji na kuwainspire watanzania kudai haki zao zilizowekwa kizuizini na Chama Cha Mafisadi

Hongereni sana wana wa Nyanza.
 
Maombi ya prophet Lema hayo.
huyu jamaa waliojaribu kumponda wanasema elimu yake ina utata lakini uwezo na mvuto wake vinaweza kuwa juu ya uwezo wetu wa kufikiri.

Msimamo, mvuto na nguvu zake ni kubwa mno

 
Mungu anamsikiliza sana Godbless Rema. amefunga na kuomba kwa siku saba tu lakini Mungu kamtendea Makubwa sana katika kipindi kifupi baada ya kumaliza mfungo.
wao wana pesa sisi tuna Mungu by G.Rema.
 
Kwa mwendo huu lema atashinda rufaa ili kumwondoa kwenye hiyo operation bomoa c c c m jenga chadema
 
Tunawakaribisha sana lakini wasitegemee ubwabwa na kanga kwetu. Sisi huku tunachangia Chama tuleta ukombozi, hatupo kwa ajili ya pesa. Natumaini wamekuja kwa moyo wa kukomboa nchi yetu

Safi sana na sipati picha tarehe 9dec 2015 sikukuu itakavyopendeza chini ya Raisi wa kwanza toka opposition,RAIS WA KWANZA TOKA CDM.KAMA UHURU DAY VILE.
 
Kwaya ijulikanayo kama Kwaya ya Ng'ombe ya Magu Mjini Mkoani Mwanza yenye watu 45 imejiengua CCM na kuhamia CHADEMA. Wanakwaya hao wamepokelewa na Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Magu ndugu Katinde aliyeongozana na Katibu wa CHADEMA Jimbo la Magu mjini Bahati Simon.

Hii ilikuwa ni Kwaya ya waliyoitumia sana kwenye kampeni na kwenye kila matukio yao na vifaa vyao vyote vya muziki vilitunzwa kwenye ofisi za CCM wilaya ya Magu. Siku mbili kabla ya kuhamia CHADEMA walitafuta kambi ya muda na wakatunga nyimbo za kumsifia Dr. Slaa ambaye atafanya ziara hivi karibuni wilayani Magu.


Uongozi mbaya ndo unaiua CCM, mzee wao yeye kazi kuzurura tu nchi za nje na mawaziri aliowaweka si watendaji sasa anategemea nani atakayesimamia? kweli nimeamini ndo maana mikoa mingi ya Puani haina maendeleo kumbe tatizo ndo hilo. Yahani jamaa anaua chama na nchi pia anaiua. Haya msubiri kuokota mipira kwenye nyavy
 
mmh,kwaya tena?
Si ndo yale yale ya kuanza kuchezewa ngoma kabla ya hotuba
au kukagua maendeleo?

Waingie kama wana chama tu,kucheza ngoma na kuimba imba
kwaya za ajabu hakuna mda sasa,time is money.

usiwe na shaka watapewa shule kuhusu katiba, kanuni, taratibu na itikadi za cdm, kuimba, kuvaa kijani na njano, kula ubwabwa, kanga vitenge kofia cdm hakuna tupo vitani kuikomboa nchi tutaimba zile nyimbo zetu za ukombozi sio kwaya za ajabu ajabu!!CHADEMA MWENDO MDUNDO!!
 
Uongozi mbaya ndo unaiua CCM, mzee wao yeye kazi kuzurura tu nchi za nje na mawaziri aliowaweka si watendaji sasa anategemea nani atakayesimamia? kweli nimeamini ndo maana mikoa mingi ya Puani haina maendeleo kumbe tatizo ndo hilo. Yahani jamaa anaua chama na nchi pia anaiua. Haya msubiri kuokota mipira kwenye nyavy

Ni janga kubwa sana kuwa na rais mzembe na baraza la mawaziri wazembe, system yote inaoza!!
 
Safi sana na Tunasubiria kusikia Dkt Limbu akiachia ubunge maana miaka 10 hakuna alichofanya cha maana jimboni kwake

Kwani Limbu bado ni mbunge? Nilisikia anaumwa sana kapona?
 
Mimi ni mwenyeji wa Magu hiyo kwaya ilikuwa ikitumika katika kampeni na kueneza propaganda za CCM Magu vijijini na mjini.
 
Hii kali, kwa hiyo Magamba hawana band huko Mwanza. Unabidi Komba ajiuzulu Ubunge akaimarishe bendi ili Kikwete aburudishwe
 
Tunawakaribisha sana lakini wasitegemee ubwabwa na kanga kwetu. Sisi huku tunachangia Chama tuleta ukombozi, hatupo kwa ajili ya pesa. Natumaini wamekuja kwa moyo wa kukomboa nchi yetu

umenifurahisha hapo kwenye kufuata ubwabwa na posho,ukombozi ni gharama asante kwa kuwakumbusha kuja na nauli zao na mji na mchango pia wa kukiimarisha chama.
 
Back
Top Bottom