Kwanini watumishi wa Umma wawe na Masters na PhD?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Nimefuatilia hoja za viongozi wengi wa Umma wenye PhD na Masters, kila wanaposimama kuzungumzia mstakabali wa nchi yetu wamekuwa wepesi sana KUTUDANGANYA.

Matumizi ya elimu za wasomi ambao ndio viongozi waandamizi wa Taifa letu hayaendani kabisa na kile wanachokichangia kwa Taifa.

Msemaji wa serikali ana PHd ila sikiliza hoja zake katika vipindi na maeneo mbalimbali utagundua lipo tatizo la kusema ukweli hapa nchini na tatizo linachangiwa na wasomi.

Msikilize Mbobezi wa sheria, Mzee wa Mambo ya nje anapozungumza kuhusu nchi yetu utagundua lipo gonjwa la uongo ndani yetu. Waziri wa Mambo ya nje alituaminisha sisi ni matajiri na kuwaita matajiri MABEBERU huku akijua tunao mabalozi nje wanaotuombea tupate misaada na wahisani, ni kulewa UONGO wa kisomi.

Nenda kutana na mtumishi wa Umma mwenye master's na Phd zungumza naye japo kwa dakika kadhaa unagundua wazi hata kile anachokifanya hakijui.

Najiuliza kwanini tunadhani tunahitaji wasomi wakubwa kuingoza sekta ya umma hapa Tanzania?
 
Kuna mtengano mfinyu sana kati ya Elimu na Maendeleo

Serikali ndio inayohitaji kuaandaa Mipango ya Maendeleo kwa watu wake

Sasa hapo unaweza kujua serikarini hakuna kabisa mtengamano kati ya kiwango cha Elimu cha watumishi wake na upatikanaji wa Maendeleo kwa wananchi wake

Ukiwa huna Elimu fanya Miradi yako utafanikiwa sana kama unae Elimu nenda serikali utaenjoy bila hata ya jasho

Hii kitu ningetakiwa kuipa jina ningeipa kihehe kabisa 'High Level of Incompetence' inalipa sana provided tu uwe nayo what so called 'Elimu'
 
Hawa wengine wana phd za mtandaoni, nao wanajitabanaisha kama walioelimika, kumbuka kwenye msafara wa mamba huwezi kukosa angalau kenge wawii.
 
Nilishaliongelea sana humu. Bongo hakuna Phd Kuna wahuni waliosoma degree 3 ili waitwe Dr au wapande vyeo makazini. Wabongo wanasoma kwa cv tu sio kuelimika
 
Degree moja inatosha MASTAZ NA pihechidii ni upotevu wa nguvu,muda,na rasilimali fedha .
 
Ninavyoelewa mimi ma- professor wengi wa nchi za wenzetu huwa kwenye academic institutions wakifundisha na kuendelea kufanya research mbali mbali ambazo siku moja zitamuwezesha kushinda hata Nobel Prize. Vile vile huandika vitabu na publications mbali mbali kama njia moja wapo ya kujiingizia kipato na vile vile kuwa kama visiting lecturers kwenye university nyingine.

Hapa kwetu ni different story. Wengi wameingia kwenye siasa na kuzitupa academic credentials zao kapuni na kuwaacha watoto wetu vyuoni wakikosa hata wahadhiri wa kuwafundisha.

Ningependa kuona ma- professor wetu kwa mfano wa Math, basi anakuwa na hata you tube channel fulani hivi ya kuwasaidia vijana wetu kulielewa na kulipenda somo ambalo mpaka sasa ni kizungumkuti kwao. Tumeliona kwa kwa ma - professor wa nchi za ughaibuni.

To his credit, Nampongeza sana Professor Ngowi wa pale Mzumbe ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuwaelimisha wananchi katika masuala ya kiuchimi na budget kwenye media mbalimbali. Hivyo ameitendea haki jamii na na fani yake ya uchumi kwa ujumla.
 
Tanzania vyakula vyetu Ni ndizi na ugali. Cha ajabu hakuna hata mtanzania mmoja mwenye PhD ya ugali au mtori.

Utakuta mtu ana PhD ya kuondokana na umaskini lakini yeye mwenyewe Ni mpigaji na kijijini kwake Kuna umaskini mpaka kwenye sharubu.

Bure kabisa.

Kuna maprof Wana degree za Sheria lakini Ni wavunjifu wa Sheria number moja
 
sio kweli mkuu, labda kuna jambo moja hulielewi mkuu. Naomba nianze nawewe nipe maana ya masters na PhD. Na je hizo masters na PhD wanaomea nini? Je wasomea kuongea kwenye majukwaa au kuhutubia watu? Na je ulishawahi kuwauliza kwenye hizo PhD na masters wanasomeaga nini? Mwisho usilaum laum Kabla ya kufanya evaluation. Acha tena Acha kuwafokea zaidi utabakia kuwa mbumbu tu mpaka mwisho.
 
Kuna PhD mwingine huku jana kawadanganya Wananchi Wanyonge eti Tanzania itakua Nchi ya kwanza Afrika kuendesha Treni ya Umeme!!
 
PhD zipigwe marufuku kwani nao walionazo wamewaponza wenzao kwa kutoonesha ufanisi kwenye masuala yote.
 
Tunahitaji wasomi wakubwa kwa sababu mifumo yetu yote ni ya kisomi kuanzia mifumo ya HR,Finance na Public Service yote inahitaji wasomi hata junior staff wa Public Service wanatakiwa kuwa wasomi wazuri.

Hatuwezi kuweka ngumbalu waongoze Public Service. Ngumbalu nikimpa mfumo wa SPSS,EDMS,TANSIC nk ataiwezea wapi!!!

Ubovu wa wasomi wachache kwenye PS usi qualify kwamba hatuhitaji wasomi wazuri kwenye utumishi

Hiyo haipo
 
Nimefuatilia hoja za viongozi wengi wa Umma wenye PhD na Masters, kila wanaposimama kuzungumzia mstakabali wa nchi yetu wamekuwa wepesi sana KUTUDANGANYA.

Matumizi ya elimu za wasomi ambao ndio viongozi waandamizi wa Taifa letu hayaendani kabisa na kile wanachokichangia kwa Taifa.

Msemaji wa serikali ana PHd ila sikiliza hoja zake katika vipindi na maeneo mbalimbali utagundua lipo tatizo la kusema ukweli hapa nchini na tatizo linachangiwa na wasomi.

Msikilize Mbobezi wa sheria, Mzee wa Mambo ya nje anapozungumza kuhusu nchi yetu utagundua lipo gonjwa la uongo ndani yetu. Waziri wa Mambo ya nje alituaminisha sisi ni matajiri na kuwaita matajiri MABEBERU huku akijua tunao mabalozi nje wanaotuombea tupate misaada na wahisani, ni kulewa UONGO wa kisomi.

Nenda kutana na mtumishi wa Umma mwenye master's na Phd zungumza naye japo kwa dakika kadhaa unagundua wazi hata kile anachokifanya hakijui.

Najiuliza kwanini tunadhani tunahitaji wasomi wakubwa kuingoza sekta ya umma hapa Tanzania?
Matakwa ya kimuundo 1st dwgree inatoaha

Kwa vyeo vya madaraka/uteuzi ni masters.

PhD ni kwa learning institutions.
 
Vyeti ni ni uthibitisho kuwa uli attend masomo..

Sio uthibitisho kuwa umefanikiwa kuwa msomi
 
Exactly, walio wengi 90%, ukiongea nao, au utendaji wao wa kazi hauendani na vyeti vyao. Kama ni subordinate wako ukimtaka akuandikie report inayohusiana na kazi yake utabaki mdomo wazi.
Nimefuatilia hoja za viongozi wengi wa Umma wenye PhD na Masters, kila wanaposimama kuzungumzia mstakabali wa nchi yetu wamekuwa wepesi sana KUTUDANGANYA.

Matumizi ya elimu za wasomi ambao ndio viongozi waandamizi wa Taifa letu hayaendani kabisa na kile wanachokichangia kwa Taifa.

Msemaji wa serikali ana PHd ila sikiliza hoja zake katika vipindi na maeneo mbalimbali utagundua lipo tatizo la kusema ukweli hapa nchini na tatizo linachangiwa na wasomi.

Msikilize Mbobezi wa sheria, Mzee wa Mambo ya nje anapozungumza kuhusu nchi yetu utagundua lipo gonjwa la uongo ndani yetu. Waziri wa Mambo ya nje alituaminisha sisi ni matajiri na kuwaita matajiri MABEBERU huku akijua tunao mabalozi nje wanaotuombea tupate misaada na wahisani, ni kulewa UONGO wa kisomi.

Nenda kutana na mtumishi wa Umma mwenye master's na Phd zungumza naye japo kwa dakika kadhaa unagundua wazi hata kile anachokifanya hakijui.

Najiuliza kwanini tunadhani tunahitaji wasomi wakubwa kuingoza sekta ya umma hapa Tanzania?
 
Ninavyoelewa mimi ma- professor wengi wa nchi za wenzetu huwa kwenye academic institutions wakifundisha na kuendelea kufanya research mbali mbali ambazo siku moja zitamuwezesha kushinda hata Nobel Prize. Vile vile huandika vitabu na publications mbali mbali kama njia moja wapo ya kujiingizia kipato na vile vile kuwa kama visiting lecturers kwenye university nyingine.

Hapa kwetu ni different story. Wengi wameingia kwenye siasa na kuzitupa academic credentials zao kapuni na kuwaacha watoto wetu vyuoni wakikosa hata wahadhiri wa kuwafundisha.

Ningependa kuona ma- professor wetu kwa mfano wa Math, basi anakuwa na hata you tube channel fulani hivi ya kuwasaidia vijana wetu kulielewa na kulipenda somo ambalo mpaka sasa ni kizungumkuti kwao. Tumeliona kwa kwa ma - professor wa nchi za ughaibuni.

To his credit, Nampongeza sana Professor Ngowi wa pale Mzumbe ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuwaelimisha wananchi katika masuala ya kiuchimi na budget kwenye media mbalimbali. Hivyo ameitendea haki jamii na na fani yake ya uchumi kwa ujumla.
Kanifundisha health policy and planning
 
Back
Top Bottom