Kwanini wanawake hawajiamini katika mapenzi.

Kwanini wanawake hawajiamini katika mapenzi.

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,932
Reaction score
11,850
Wanawake wamekuwa hawajiamini katika mahusiano na ndoa zao na muda mwingi huhisi wanaibiwa wanaume, ukienda kwa waganga wa kienyeji wanawake wamejazana kutafuta madawa ya kuwatuliza wanaume hasa wajukuu zangu wahaya, wanaume tumekula mengi jamani,kwanini viumbe hawa hawajiamini kama sisi wanaume au ni kweli na wanaume tumezidi ukicheche ndo maana wenzetu roho juu.
 
Inaelekea na wewe pia hujiamini, huko kwa waganga huwa unafuata nini hadi unakutana na hao wanawake? Acha na wewe kumlisha mtoto wa watu majitu ya ajabu mura.
 
Mada za uganga zinaendelea, nakubaliana na maneno yako wanaopenda mambo ya ushirikina hawajiamini, halafu cha ajabu huyo mganga nae ni binadamu kama wewe, sasa kwanini usimuombe Mungu ambae haonekani kuliko binadamu ambae anafanya matendo kama wewe kwa mfano kula,kucheka,kukasirika nk
 
Wengi wao wana akili zakuambiwa!! Na siku zote swala la mwanamke kwenda kwamganga halianzii moyoni mwake'' hua ni ushauri wa mashoga zao!! Ambao maranyingi wanajifanya kuwasaidia kumbe kiundani huwa wanawasanifu na kutaka kuvuruga mahusiano au ndoa zao.

Lakini mtoto wakike paka aje ajue hilo nipaka yamtokee puani' ndo anagundua kumbe shogaake ndio mbaya wake.
 
Inaelekea na wewe pia hujiamini, huko kwa waganga huwa unafuata nini hadi unakutana na hao wanawake? Acha na wewe kumlisha mtoto wa watu majitu ya ajabu mura.

Ni kautafiti nilifanya kutoka kwa waganga na wanadai wateja wao wakubwa ni wanawake wanaotafuta madawa kuwatuliza mabwana wao.
 
Mada za uganga zinaendelea, nakubaliana na maneno yako wanaopenda mambo ya ushirikina hawajiamini, halafu cha ajabu huyo mganga nae ni binadamu kama wewe, sasa kwanini usimuombe Mungu ambae haonekani kuliko binadamu ambae anafanya matendo kama wewe kwa mfano kula,kucheka,kukasirika nk

Habari ya muda huu mkuu HARUFU
 
Last edited by a moderator:
Hii ipo sana tu hata kama anakutafuta demu ndoo zao yaanani hasa wa mjini kwa kalumanzila wamezidi lkn wanaowafanya wanaume wawe vicheche ni wao tu kwa kuwa MTU akilishwa basi jua atakuwa na tamaa hivyo hatakomea kwake tu.
 
Habari ya muda huu mkuu HARUFU
Nipo salama kabisa namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya iliyo bora na nitaendelea zaidi kumshukuru

Ingawa mimi simpendezeshi Mwenyezi Mungu asilimia mia moja kwa anayoyataka/anayoamrisha lakini Mwenyezi Mungu anaendelea kunipendelea pamoja na kiburi changu
 
Mapenzi yangu ndo uganga wangu not otherwise!!
 
Nipo salama kabisa namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya iliyo bora na nitaendelea zaidi kumshukuru

Ingawa mimi simpendezeshi Mwenyezi Mungu asilimia mia moja kwa anayoyataka/anayoamrisha lakini Mwenyezi Mungu anaendelea kunipendelea pamoja na kiburi changu

Allah akuoneshe njia iliyonyooka na akuondoshee lolote linalokukwaza na kukupa wasiwasi....amin
 
Allah akuoneshe njia iliyonyooka na akuondoshee lolote linalokukwaza na kukupa wasiwasi....amin
Inshallah maneno mazito sana

Hiyo ndio njia sahihi sio ya sisi/wale waliopotea, maana kuna moto mkali mno huko mbeleni

Siku ambayo watu .... yaani naogopa kuendelea

Naona kama sheria inanibana
 
Inshallah maneno mazito sana

Hiyo ndio njia sahihi sio ya sisi/wale waliopotea, maana kuna moto mkali mno huko mbeleni

Siku ambayo watu .... yaani naogopa kuendelea

Naona kama sheria inanibana

Usijali HARUFU muelekee Mwenyezi Mungu kwa kila kitu utakua na amani sana...
 
Last edited by a moderator:
Usijali HARUFU muelekee Mwenyezi Mungu kwa kila kitu utakua na amani sana...
Nitajitahidi Maalim wangu utafiti

Najua kuna KIAMA, je ni nini KIAMA? na je ni kitu gani kitakuonyesha kuwa hiki ni kiama?


Siku ambayo watu .....

Naogopa tena kuendelea Maalim
 
Last edited by a moderator:
Nitajitahidi Maalim wangu utafiti

Najua kuna KIAMA, je ni nini KIAMA? na je ni kitu gani kitakuonyesha kuwa hiki ni kiama?


Siku ambayo watu .....

Naogopa tena kuendelea Maalim

Allah atuoneshe kheri kua ni kheri na atuwezeshe kuifuata na atuoneshe shari kua ni shari na atuwezeshe kuiepuka....amin amin
 
Last edited by a moderator:
Allah atuoneshe kheri kua ni kheri na atuwezeshe kuifuata na atuoneshe shari kua ni shari na atuwezeshe kuiepuka....amin amin
Amin kwa uwezo wake inshallah

Muhimu tuwe tunakumbushana mema na kukatazana mabaya
 
he he he! Basi utakuwa unaniotaga!!
Hapana inatokea, kama unavyoona wimbo fulani huwa unakukumbusha tukio fulani

Mfano mimi kuna wimbo wa TATYANA ALI unaitwa EVERYTIME kwa kweli huwa unanikumbusha mbali sana
 
Back
Top Bottom