Watanzania wenzangu naomba mnisaidie Ujana unaishia miaka mingapi kwani Watanzania wengi hususan Wanasiasa wamekuwa hawataki kutoka kwenye hili daraja na siku zote wanang'ang'ana kwenye Ujana.
JK mwaka 2005 akiwa anagombea Urais alijinadi kuwa ni Kijana wakati akiwa na miaka 55.Watu kama akina Zitto Kabwe na Filikunjombe,Bulaya na January wanajiita vijana wakati umri wao unazidi miaka 35.Nijuavyo mimi Ujana unaanzia miaka 18-35.Naomba mnisaidie katika hili sababu Watz wengi wanapenda kuonekana wadogo kiumri wakati siyo uhalisia wao.
Tumeona hata kwenye Uchaguzi wa Mwanasiasa Kijana humu JF kuna watu wa Makamo nao wanachaguliwa kama vijana wakati umri umeshapita.Naomba Watanzania wote tuelimishane maana ya Kijana sababu kuna Wazee wengine sababu ya mawazo yao mazuri nao wanapenda waonekane Vijana. Lakini Ki uhalisia Ujana ni umri.
JK mwaka 2005 akiwa anagombea Urais alijinadi kuwa ni Kijana wakati akiwa na miaka 55.Watu kama akina Zitto Kabwe na Filikunjombe,Bulaya na January wanajiita vijana wakati umri wao unazidi miaka 35.Nijuavyo mimi Ujana unaanzia miaka 18-35.Naomba mnisaidie katika hili sababu Watz wengi wanapenda kuonekana wadogo kiumri wakati siyo uhalisia wao.
Tumeona hata kwenye Uchaguzi wa Mwanasiasa Kijana humu JF kuna watu wa Makamo nao wanachaguliwa kama vijana wakati umri umeshapita.Naomba Watanzania wote tuelimishane maana ya Kijana sababu kuna Wazee wengine sababu ya mawazo yao mazuri nao wanapenda waonekane Vijana. Lakini Ki uhalisia Ujana ni umri.