GE2025 Kwanini wanasiasa wa CCM huimiza kujiajiri wakati wao hawataki kujiari?

GE2025 Kwanini wanasiasa wa CCM huimiza kujiajiri wakati wao hawataki kujiari?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,146
Reaction score
48,382
Bila ya kujali Elimu zao au umri wao, wanasiasa wa CCM wamejazana huko kwenye kugombea nafasi za udiwani na ubunge.

Hawahawa wakichaguliwa ama wasipochaguliwa na kupewa madaraka mengine ya kisiasa, utawasikia wakihimiza vijana kujiajiri.

Imekuwaje wao wanajazana kwenye siasa wakiwa na watoto zao huku wakiwaambia watoto wa maskini wajiajiri?
 
Kwani wewe nani kakuzuia kuingia na kujiunga kwenye siasa ikiwepo kutimiza haki yako na uhuru wa kugombea nafasi utakayo?
 
Just imagine mzee wa miaka 80, Wasira bado anaogopa kujiajiri.
 
... TENA WENGINE WAMEISHAKAA BUNGENI VIPINDI ZAIDI YA VIWILI, KIASI MTU UNAJIULIZA WANAWEZAJE KUKOSA MITAJI YA HATA VIWANDA VIDOGOVIDOGO!
NB: PATO LA MBUNGE KWA MWEZI MMOJA NI MTAJI TOSHA!
 
Bila ya kujali Elimu zao au umri wao, wanasiasa wa CCM wamejazana huko kwenye kugombea nafasi za udiwani na ubunge.

Hawahawa wakichaguliwa ama wasipochaguliwa na kupewa madaraka mengine ya kisiasa, utawasikia wakihimiza vijana kujiajiri.

Imekuwaje wao wanajazana kwenye siasa wakiwa na watoto zao huku wakiwaambia watoto wa maskini wajiajiri?
Kwa sababu wameshindwa kutengeneza FURSA mpya za ajira!
 
Umeelewa nilichoandika? Au umekuja fasta na baiskeli yako bila ya kusoma nilichoandika?
Huyo hana akili mtu unakua mtumwa wa chama baada ya nchi Nyerere mwenyewe alisema CCM sio mama ake baba ake Nchi kwanza Tanzania watu wanakua wazalendo wa vyama alafu wanawacheka Kenya na Ukabila Kenya na sisi tuko Kwenye kapu Moja
 
Hii hoja kubwa Sana... Kwa ivo wanajua hata watoto wao hawatapata ajira.
Ndio maana yake. Na kama wakitengeneza FURSA za ajira za maana kabisa then hawatapata chawa wa kuwajaza kwenye malori ili kuuhadaa umma,watashindwa namna ya kuhalalisha uharamia wao wa kuonesha kwamba still wanakubalika hasa na wanyonge huko vijijini. Mtu kama Lucas Mwashambwa atakuwa busy na shughuli zake za kumuingizia kipato,hatakuwa na muda wa kumbubujikia mtu machozi. Ndio hii wanasemaga ukikimbia nchale,ukikaa nchale!.

HAKI NA KWELI HUMWEKA MTU HURU WAKATI WOTE!
 
Back
Top Bottom