Kwanini wana CCM wako bize kuzusha kuhusu Lissu?

Kwanini wana CCM wako bize kuzusha kuhusu Lissu?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,838
Reaction score
50,543
Siku Lissu anashambuliwa CCM walitoa tangazo la kulaani kushambuliwa kwa Lissu. Lakini watu wengi humu walitilia shaka kama kweli CCM wanatoa pole kwa dhati ama wanatimiza wajibu tu. Wana CCM wengi sana hata humu JF walikuwa kabla ya Lissu kushambuliwa kwa Risasi, wanatamani Lissu ashikishwe adabu kwa njia yoyote ile hata kwa kunyongwa!

Leo taratibu imeanza kuonekana kumbe hata ile Pole ya chama chao iliyotolewa na Polepole , ilikuwa ni Geresha tu kwani mioyoni mwao bado wana inda na Lissu. Taratibu wameanza kuleta mabandiko kuonesha kwamba kuna uwezekano Lissu kashambuliwa na wabaya wake kwenye mambo ya sheria ama chama chake cha CHADEMA.

kuna jambo wana CCM wanajaribu kulifanya kwenye mitandao ya kijamii ili kuondoa shuku kwa chama chao kuhusika na mashambulizi dhidi ya Lissu. Huku mitaani ni wana CCM peke yao ambao wanaonesha hawajui ni kina nani hasa walikuwa na kiu ya kuona Lissu anaondolewa duniani kwa njia yoyote ile. Lakini watanzania wengi wanajua ni kina nani walikuwa wanatamini Lissu afe.

Lissu hajawa Tishio kwa yeyote yule ndani ya CHADEMA ila kila mwana CHADEMA kuanzia viongozi wa kitaifa wanamuona Lissu kwamba ni mjenga chama jasiri mwenye aina yake ya siasa kuliko wengi wao ndani ya CHADEMA. CHADEMA inamtegemea Lissu na wala Lissu haitegemei CHADEMA kuwa vile alivyo!

Kwanza wana CCM wana bahati kuwa viongozi wa CHADEMA huwa hawajibu uzushi unaoanzishwa nao hata kama una madhara kwa CHADEMA. CCM huko siku za nyuma walikuwa wanamhofia Mbowe peke yake, lakini tangu baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, wanaoogopwa na CCM ndani ya CHADEMA wameongezeka!

Kuhusu Lissu inajulikana na ushahidi upo kwamba viongozi wa CCM kujiapiza kupambana naye kwa njia halali na haramu. Sasa leo hii kuleta uzushi kwamba CHADEMA ndiyo ingefaidika kwa kuuawa kwa Lissu ni upuuzi mtupu unaokuzwa na wale waliotaka Lissu afe kwa lengo la kupoteza watanzania maboya.HAMTAWEZA!
 
Mzee tamko la CCM hutolewa tu na ofisi zenye mamlaka.
Kauli ya Ndugu Raisi na Bwana Polepole ndiyo msimamo wa Chama.
Hao vijana wanaozusha ndiyo wazungumzaji wa Chama ???

Ni sawa na leo Yericko Nyerere atoe kauli zake zile,
Halafu nikimbilie kusema huo ndiyo Msimamo wa BAVICHA au CHADEMA yote.
Hii inakuwa siyo sahihi sana (Japo hutokea mara nyingine)
 
Kuzusha ili iweje!!
Huyu lissu nani hasa kwa Taifa hili!!
Tumepoteza Askari wakutosha Kibiti,
Tumepoteza Raia wakutosha Kibiti,Tanga
Huyu lisu nani kwanza!!

Huu ujinga kutwa lissu lissu Mnachosha tafuteni Kiki zingine
Tanzania nizaidi ya huyo Lissu wenu
Tanzania ni wewe na wenzako ndiyo hamjui Lissu ni nani. Wenzako wenye madaraka kwenye kile chama chenu rafiki wanajua Lissu ni nani na ndiyo maana mwingine alisema "heri msinipe mimi kura lakini msimchague pia na Lissu" na mwingine aliwahi kusema "mkimchagua huyo sitateua mtu toka kwenu"!
 
Bora mkuu umewafungukia hawa mazwazwa maana kuna propaganda chafu sana na nadharia za kishenzi wanazisambaza hivi sasa kwa kasi ya ajabu!
Kuna mabandiko yao wanaleta humu ambayo hayana kichwa wala miguu, mara kwa nini mbowe anachangisha pesa za matibabu, mara kwa nini dereva hakujeruhiwa, kwa nini dereva ndiye aliyepewa nguo badala ya mkewe!
Yaani vimaada vya ajabu ajabu vinavyoashiria kama wanataka kujisafisha kwenye hili.
Ni ukweli usiopingika kuwa Lisu hajawahi kuwa adui wa yeyote ndani ya cdm. Hakuna mwana cdm asiyempenda Lisu...
Ila maccm hawampendi kabisa na hata humu jf kuna mmoja alijitokeza wazi kabisa na kuanzisha uzi kuwa hampendi Lisu.
 
Kuzusha ili iweje!!
Huyu lissu nani hasa kwa Taifa hili!!
Tumepoteza Askari wakutosha Kibiti,
Tumepoteza Raia wakutosha Kibiti,Tanga
Huyu lisu nani kwanza!!

Huu ujinga kutwa lissu lissu Mnachosha tafuteni Kiki zingine
Tanzania nizaidi ya huyo Lissu wenu

Mngekesha usiku kucha kuandaa propaganda chafu kwasababu yake? Kama Lissu sio chochote kwanini mlitaka kummaliza?
 
Hujachoka wewe, ungekuwa umechoka hata usingefungua huu uzi!
Kuzusha ili iweje!!
Huyu lissu nani hasa kwa Taifa hili!!
Tumepoteza Askari wakutosha Kibiti,
Tumepoteza Raia wakutosha Kibiti,Tanga
Huyu lisu nani kwanza!!

Huu ujinga kutwa lissu lissu Mnachosha tafuteni Kiki zingine
Tanzania nizaidi ya huyo Lissu wenu
 
Askari Mmoja anaweza linda Uhai wa Watanzania 200
Kupoteza Askari 10
umehatarisha Uhai wa Watanzania 2000!
Nikwanini Hamkuja na Upbavu wenu kama huu kutwa ili kulaani Kuuliwa kwa Askari wetu!

Huyo Lissu analipi lamaana kwa Taifa hili zaidi yakuwa Msaliti na mnafiki kwa Taifa,
Huyo yupo radhi kutetea Wazungu na kuiponda nchi yake!

Tanzania Imepoteza watu muhimu zaidi ya huyo Tundu lissu
msiwafanye watanzania wajinga kiasi hicho
Watanzania gani unaowaongelea?
 
Kuzusha ili iweje!!
Huyu lissu nani hasa kwa Taifa hili!!
Tumepoteza Askari wakutosha Kibiti,
Tumepoteza Raia wakutosha Kibiti,Tanga
Huyu lisu nani kwanza!!

Huu ujinga kutwa lissu lissu Mnachosha tafuteni Kiki zingine
Tanzania nizaidi ya huyo Lissu wenu
Kumbe hua uko hivi lo
 
Kuzusha ili iweje!!
Huyu lissu nani hasa kwa Taifa hili!!
Tumepoteza Askari wakutosha Kibiti,
Tumepoteza Raia wakutosha Kibiti,Tanga
Huyu lisu nani kwanza!!

Huu ujinga kutwa lissu lissu Mnachosha tafuteni Kiki zingine
Tanzania nizaidi ya huyo Lissu wenu
We ni lofaaaaaaaaa yan kitu kama hicho unaweza sema ni kiki? We ni wakupimwa mkojo,mana ni mbumbumbu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ficha upumbavu wako
Ammalize nani huyo!
Atajimaliza na upuuzi wake,
Ukikubari kutimiwa na wazungu jua mwisho wako unakaribia
wale hawana Rafiki
mlitegemea apewe kazi na aendelee kupeta!!

Tanzania nizaidi ya Lissu

Ficha upumbavu wako na wachama chako.
 
Kuzusha ili iweje!!
Huyu lissu nani hasa kwa Taifa hili!!
Tumepoteza Askari wakutosha Kibiti,
Tumepoteza Raia wakutosha Kibiti,Tanga
Huyu lisu nani kwanza!!

Huu ujinga kutwa lissu lissu Mnachosha tafuteni Kiki zingine
Tanzania nizaidi ya huyo Lissu wenu
Una utahira ndani yako kama unachoka kalale hujalazimishwa kusoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom