Mada nzuri sana hii
Gambamala.
Hata mimi huwa najiuliza sana juu ya hawa jamaa. Ni watu wa movements sana popote walipo, hata wawe UK ama US ama Australia ni lazima utawakuta na associations zao za kiharakati kuhusu jamii yao. Kwangu mimi hawatofautiani sana na jews pamoja na catalans. Hawa wote focus yao kubwa ni mataifa kwa ajili ya jamii zao. Jews wamepata lakini hawa wengine bado. Ndiyo maana wakurdi katika nchi zote ambamo jamii yao ipo kwa wingi ni harakati tu za kisiasa, kijamii hata kijeshi. Wao wanahisi kuwa wanakandamizwa, sina hakika sana juu ya hilo ama tu ni inferiority complex ndani yao.
Kule Uturuki kuna PKK na kiongozi wao Abdullah Ocalan alisumbua sana kabla ya kutiwa rupango, pale Iran wana KDPI nayo ni moto. Pia wana harakati kubwa sana Syria na Iraq hadi miaka ile ya mwanzo ya 1990's Saddam Hussein akawafanyia umafia mkubwa katika kuzima up-rising yao. Pia ni jamii yenye ushawishi sana katika siasa za kimataifa hasa ndani ya mataifa makubwa ya ulaya na america ndiyo maana mara nyingi wanapoguswa intervention huwa kubwa. Ni harakati zao hizi ambazo zimepelekea wao kijijengea uadui mkubwa na jamii zingine papo hapo kujitengenezea marafiki wanaowaunga mkono.