Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Kwa nini Wakristo wanawasifia Waisraeli? Kwa nini wanawatetea, wanawaombea na hata kuwatakia baraka? Je, si hao hao waliomkataa Yesu na kumsulibisha?
Ukweli wa kibiblia ni huu: Waisraeli ni Wakristo watarajiwa. Ingawa kwa sasa hawamkiri Yesu kuwa ni Masihi, Biblia inaonyesha kuwa watamkiri baadaye—kwa toba ya kweli na ya kitaifa.
Hebu tuangalie japo kwa kifupi, sababu muhimu zinazowafanya Wakristo kuwashabikia Waisraeli:
1. Waisraeli ni Wateule wa Mungu kwa Agano la Kale
“Mungu hajawakataa watu wake aliowajua tangu mwanzo.” (Warumi 11:2)
Waisraeli waliitwa tangu zamani za kale kupitia Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Hadi sasa Mungu hajabadili agano lake kwao. Ahadi za Mungu kwao bado hazijafutwa. “Kwa maana karama za Mungu na mwito wake havina majuto.” (Warumi 11:29). Ahadi za Mungu kwa Israeli bado zinasimama, hata kama kwa sasa hawaiamini injili.
2. Tumeagizwa kuwabariki Waisraeli
“Nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani.” (Mwanzo 12:3)
Kuwatakia baraka Israeli ni sehemu ya kutii mpango wa Mungu. Anayeilaani Israeli analaaniwa.
3. Waisraeli watamkiri Yesu - soon
“Nao watamtazama yeye waliyemchoma, nao watamwombolezea...” (Zekaria 12:10)
Mambo yanayofanyika sasa Mashariki ya Kati ni ishara ya wazi kuwa unabii huo unakaribia kutimia. Siku yaja, kutakuwepo na toba ya kweli ya kitaifa kutoka kwa Waisraeli. Watamkiri Yesu kuwa ni Masihi wao.
4. Watajiunga na Wakristo katika Wokovu
“Na hivyo Israeli wote wataokolewa.” (Warumi 11:26)
Yesu aliwaambia Wayahudi:
“Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa hadi mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.” (Mathayo 23:39)
Yesu aliposema “Hamtaniona tena...” alimaanisha hatakuwepo kwa muda, hadi Israeli kwa ujumla wao watakapomkiri kwa imani ya kweli. Hii itatimia siku za mwisho, watakapomkaribisha Yesu kwa toba na kusema kwa dhati: “Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.”
Siku hiyo ikifika, Waisraeli wataungana na Kanisa lote duniani na kuwa ndugu wa kiroho.
Soma sababu ya 5 katika post inayofuata...
Ukweli wa kibiblia ni huu: Waisraeli ni Wakristo watarajiwa. Ingawa kwa sasa hawamkiri Yesu kuwa ni Masihi, Biblia inaonyesha kuwa watamkiri baadaye—kwa toba ya kweli na ya kitaifa.
Hebu tuangalie japo kwa kifupi, sababu muhimu zinazowafanya Wakristo kuwashabikia Waisraeli:
1. Waisraeli ni Wateule wa Mungu kwa Agano la Kale
“Mungu hajawakataa watu wake aliowajua tangu mwanzo.” (Warumi 11:2)
Waisraeli waliitwa tangu zamani za kale kupitia Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Hadi sasa Mungu hajabadili agano lake kwao. Ahadi za Mungu kwao bado hazijafutwa. “Kwa maana karama za Mungu na mwito wake havina majuto.” (Warumi 11:29). Ahadi za Mungu kwa Israeli bado zinasimama, hata kama kwa sasa hawaiamini injili.
2. Tumeagizwa kuwabariki Waisraeli
“Nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani.” (Mwanzo 12:3)
Kuwatakia baraka Israeli ni sehemu ya kutii mpango wa Mungu. Anayeilaani Israeli analaaniwa.
3. Waisraeli watamkiri Yesu - soon
“Nao watamtazama yeye waliyemchoma, nao watamwombolezea...” (Zekaria 12:10)
Mambo yanayofanyika sasa Mashariki ya Kati ni ishara ya wazi kuwa unabii huo unakaribia kutimia. Siku yaja, kutakuwepo na toba ya kweli ya kitaifa kutoka kwa Waisraeli. Watamkiri Yesu kuwa ni Masihi wao.
4. Watajiunga na Wakristo katika Wokovu
“Na hivyo Israeli wote wataokolewa.” (Warumi 11:26)
Yesu aliwaambia Wayahudi:
“Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa hadi mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.” (Mathayo 23:39)
Yesu aliposema “Hamtaniona tena...” alimaanisha hatakuwepo kwa muda, hadi Israeli kwa ujumla wao watakapomkiri kwa imani ya kweli. Hii itatimia siku za mwisho, watakapomkaribisha Yesu kwa toba na kusema kwa dhati: “Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.”
Siku hiyo ikifika, Waisraeli wataungana na Kanisa lote duniani na kuwa ndugu wa kiroho.
Soma sababu ya 5 katika post inayofuata...