J C
JF-Expert Member
- Dec 12, 2013
- 3,139
- 2,635
Habari za muda huu.
Eid Moubarak.
Napenda kuuliza Hili suala la sikukuu za dini ya kiislamu zikoje? Leo ni siku ya Jumatano naona watoto wanaenda shule kisha wanatawanyishwa na kurudi nyumbani. Sio hivyo tu siku ya Jumatatu kumetokea mkanganyiko mkubwa wapo walioenda shule na waliobaki nyumbani kusherehekea Idd.
Kwa watoto ambao hawakuenda shule siku ya Jumatatu wanakabiliwa na adhabu kali ya utoro. Na leo Jumatano naona wamekwenda ila kwa hofu japo wapo walio manunda wamebaki home liwalo na liwe.
Sasa nauliza je hili suala kwa Waislamu limekaaje? Kulinganisha na wenzetu Wakristo ambao sikukuu zao huwa na mpangilio mzuri japo hawapatani kiitikadi na kimadhehebu.
Kwanini Waislamu msikae mkakubaliana ili Idd iwe siku tatu na kama msipo kubaliana basi kundi moja liwe pole tu likubaliane na jingine ili kuondoka sitofahamu iliyopo inayoleta usumbufu na kuonea shaka imani kutokuwa na kueleweka na kukosa misimamo thabiti ya kiimani na kimafundisho. Heri ya sikuu ya Eid.
Eid Moubarak.
Napenda kuuliza Hili suala la sikukuu za dini ya kiislamu zikoje? Leo ni siku ya Jumatano naona watoto wanaenda shule kisha wanatawanyishwa na kurudi nyumbani. Sio hivyo tu siku ya Jumatatu kumetokea mkanganyiko mkubwa wapo walioenda shule na waliobaki nyumbani kusherehekea Idd.
Kwa watoto ambao hawakuenda shule siku ya Jumatatu wanakabiliwa na adhabu kali ya utoro. Na leo Jumatano naona wamekwenda ila kwa hofu japo wapo walio manunda wamebaki home liwalo na liwe.
Sasa nauliza je hili suala kwa Waislamu limekaaje? Kulinganisha na wenzetu Wakristo ambao sikukuu zao huwa na mpangilio mzuri japo hawapatani kiitikadi na kimadhehebu.
Kwanini Waislamu msikae mkakubaliana ili Idd iwe siku tatu na kama msipo kubaliana basi kundi moja liwe pole tu likubaliane na jingine ili kuondoka sitofahamu iliyopo inayoleta usumbufu na kuonea shaka imani kutokuwa na kueleweka na kukosa misimamo thabiti ya kiimani na kimafundisho. Heri ya sikuu ya Eid.