Kwanini Waislam msikubaliane kuhusu sikukuu ya Idi?

Kwanini Waislam msikubaliane kuhusu sikukuu ya Idi?

J C

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2013
Posts
3,139
Reaction score
2,635
Habari za muda huu.

Eid Moubarak.

Napenda kuuliza Hili suala la sikukuu za dini ya kiislamu zikoje? Leo ni siku ya Jumatano naona watoto wanaenda shule kisha wanatawanyishwa na kurudi nyumbani. Sio hivyo tu siku ya Jumatatu kumetokea mkanganyiko mkubwa wapo walioenda shule na waliobaki nyumbani kusherehekea Idd.

Kwa watoto ambao hawakuenda shule siku ya Jumatatu wanakabiliwa na adhabu kali ya utoro. Na leo Jumatano naona wamekwenda ila kwa hofu japo wapo walio manunda wamebaki home liwalo na liwe.

Sasa nauliza je hili suala kwa Waislamu limekaaje? Kulinganisha na wenzetu Wakristo ambao sikukuu zao huwa na mpangilio mzuri japo hawapatani kiitikadi na kimadhehebu.

Kwanini Waislamu msikae mkakubaliana ili Idd iwe siku tatu na kama msipo kubaliana basi kundi moja liwe pole tu likubaliane na jingine ili kuondoka sitofahamu iliyopo inayoleta usumbufu na kuonea shaka imani kutokuwa na kueleweka na kukosa misimamo thabiti ya kiimani na kimafundisho. Heri ya sikuu ya Eid.
 
Fungeni kwa kuona kuandama kwa mwezi na fungulieni kwa kuona kuandama kwa mwezi ila cha ajabu bado uhakika wa sikukuu haupo
 
Fungeni kwa kuona kuandama kwa mwezi na fungulieni kwa kuona kuandama kwa mwezi ila cha ajabu bado uhakika wa sikukuu haupo
Kwa hiyo mkuu nani yuko sahihi kati ya wa jumatatu au jumanne?.
 
Walimu wa nchi hii ndio Mama wa tatizo la rasilimali akili

kwa mifano ya kishule shule uliyotoa inaonesha Wewe ni Mwalimu wa Shule ya Msingi ila uwezo wako wa kujenga na kuwasilisha hoja uko 'PUA'
 
Habari za muda huu.

Eid Moubarak.

Napenda kuuliza Hili suala la sikukuu za dini ya kiislamu zikoje?. Leo ni siku ya Jumatano naona watoto wanaenda shule kisha wanatawanyishwa na kurudi nyumbani. Sio hivyo tu siku ya Jumatatu kumetokea mkanganyiko mkubwa wapo walioenda shule na waliobaki nyumbani kusherehekea Idd.

Kwa watoto ambao hawakuenda shule siku ya Jumatatu wanakabiliwa na adhabu kali ya utoro. Na leo Jumatano naona wamekwenda ila kwa hofu japo wapo walio manunda wamebaki home liwalo na liwe.

Sasa nauliza je hili suala kwa Waislamu limekaaje?. Kulinganisha na wenzetu Wakristo ambao sikukuu zao huwa na mpangilio mzuri japo hawapatani kiitikadi na kimadhehebu.

Kwa nini Waislamu msikae mkakubaliana ili Idd iwe siku tatu na kama msipo kubaliana basi kundi moja liwe pole tu likubaliane na jingine ili kuondoka sitofahamu iliyopo inayoleta usumbufu na kuonea shaka imani kutokuwa na kueleweka na kukosa misimamo thabiti ya kiimani na kimafundisho. Heri ya sikuu ya Eid.
Huo ujinga wa kutofoutiana siku uko kwenye viongozi wa dini ya kiislamu Tz tu, nchi zingine hamna ujinga kama huo.
 
Walimu wa nchi hii ndio Mama wa tatizo la rasilimali akili

kwa mifano ya kishule shule uliyotoa inaonesha Wewe ni Mwalimu wa Shule ya Msingi ila uwezo wako wa kujenga na kuwasilisha hoja uko 'PUA'
PUA ndio nini Shekhe?.
 
Habari za muda huu.

Eid Moubarak.

Napenda kuuliza Hili suala la sikukuu za dini ya kiislamu zikoje?. Leo ni siku ya Jumatano naona watoto wanaenda shule kisha wanatawanyishwa na kurudi nyumbani. Sio hivyo tu siku ya Jumatatu kumetokea mkanganyiko mkubwa wapo walioenda shule na waliobaki nyumbani kusherehekea Idd.

Kwa watoto ambao hawakuenda shule siku ya Jumatatu wanakabiliwa na adhabu kali ya utoro. Na leo Jumatano naona wamekwenda ila kwa hofu japo wapo walio manunda wamebaki home liwalo na liwe.

Sasa nauliza je hili suala kwa Waislamu limekaaje?. Kulinganisha na wenzetu Wakristo ambao sikukuu zao huwa na mpangilio mzuri japo hawapatani kiitikadi na kimadhehebu.

Kwa nini Waislamu msikae mkakubaliana ili Idd iwe siku tatu na kama msipo kubaliana basi kundi moja liwe pole tu likubaliane na jingine ili kuondoka sitofahamu iliyopo inayoleta usumbufu na kuonea shaka imani kutokuwa na kueleweka na kukosa misimamo thabiti ya kiimani na kimafundisho. Heri ya sikuu ya Eid.
Habari ni njema mkuu.
Kwa kawaida sikukuu ya Idi inayoadhimishwa baada ya mfungo wa Ramadhan ina siku mbili za mapumziko yaani Idi mosi na Idi pili.

Kama ujuavyo, sikukuu hizi hazina tarehe maalumu za kalenda ya jua isipokuwa zinafuata mwandamo wa mwezi. Na mwandamo wa mwezi nao una tofauti, unaweza kuandama kwa siku 29 au 30.

Sasa mkanganyiko uliousema umetokana na hali kwamba mataifa mengine walitangaza mwezi kuonekana siku ya Jumamosi, mengine kama mataifa jirani Kenya na Uganda walitangaza kuonekana siku ya Jumapili.

Na Tanzania ikatangazwa haujaonekana na hivyo kikalimilisha siku 30 na Idi ikaswaliwa Jumanne.

Sasa wapo waislam walioswali Idi siku ya Jumapili, wengine wakaswali Jumatatu na wengine Jumanne.

Kwakuwa serikali inasikiliza BAKWATA wanasema nini, hivyo kwa mujibu wa BAKWATA siku za mapumziko ni Jumanne na Jumatano.

Na hili si jambo jipya kutokea nchini, labda sasa serikali kwa kutumia busara itambue wapo waislam wanaswali Idi kwa kuonekanwa mwezi mahala popote na wapo wanaswali kwa kuonekanwa Tanzania pekee.

Hii ndio sababu ya mkaganyiko kiongozi.
 
Habari ni njema mkuu.
Kwa kawaida sikukuu ya Idi inayoadhimishwa baada ya mfungo wa Ramadhan ina siku mbili za mapumziko yaani Idi mosi na Idi pili.

Kama ujuavyo, sikukuu hizi hazina tarehe maalumu za kalenda ya jua isipokuwa zinafuata mwandamo wa mwezi. Na mwandamo wa mwezi nao una tofauti, unaweza kuandama kwa siku 29 au 30.

Sasa mkanganyiko uliousema umetokana na hali kwamba mataifa mengine walitangaza mwezi kuonekana siku ya Jumamosi, mengine kama mataifa jirani Kenya na Uganda walitangaza kuonekana siku ya Jumapili.

Na Tanzania ikatangazwa haujaonekana na hivyo kikalimilisha siku 30 na Idi ikaswaliwa Jumanne.

Sasa wapo waislam walioswali Idi siku ya Jumapili, wengine wakaswali Jumatatu na wengine Jumanne.

Kwakuwa serikali inasikiliza BAKWATA wanasema nini, hivyo kwa mujibu wa BAKWATA siku za mapumziko ni Jumanne na Jumatano.

Na hili si jambo jipya kutokea nchini, labda sasa serikali kwa kutumia busara itambue wapo waislam wanaswali Idi kwa kuonekanwa mwezi mahala popote na wapo wanaswali kwa kuonekanwa Tanzania pekee.

Hii ndio sababu ya mkaganyiko kiongozi.
Una maanisha kwa Tanzania mwandamo wa mwezi unategemea bakwata?

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo ni taasisi inayosimamia waislamu kuongozwa na wasiojua kuongoza
Kuna tetesi kwamba pia huingiliwa kazi zake na kupangiwa na wengine labda hata wasiokuwa waislamu?
Mikanganyiko ni mingiiiii, kila ukisikiza kauli zao zinazidi kukuchanganya,
So suluhisho ni kufuata pale uislamu ulipoanzia kama dini zingine zifatazo machimbuko yao,
Kufuata tu viongozi kama n'gombe kwa madai ya kwamba watawajibishwa wao huko ni kujidanganya
Kwani uislamu unakutaka usome na kujifundisha dini yako ili kujua na kufata yakini,
Waislamu kuweni kitu kimoja mutafaulu vinginevyo mutagawanywa na mutagawanyika mpaka kiyama kisimame
 
Fungeni kwa kuona kuandama kwa mwezi na fungulieni kwa kuona kuandama kwa mwezi ila cha ajabu bado uhakika wa sikukuu haupo
Inasemekana Jumapili Kenya waliona mwezi ila Tanzania haukuonekana
 
Back
Top Bottom