TIN namba anakuwa nayo mwajiri wako ambaye ndiye mwenye jukumu la kupeleka kodi zote za wafanyakazi walioko chini yake
Kwa nn inafanyika hivyo?
Naamini ni kutoa urahisi wa usimamizi na ufuatiliaji wa kodi husika hasa kwa kuzingatia kuwa anaewasilisha kodi ni Mwajiri.
Chukulia mfano una wafanyakazi 200 kila mmoja akiwa na TIN namba yake maana yake italazimika kodi kulipwa kwa namba hizo....inaweza kuwa kwa namna mbili....moja ni wewe mwenyewe kwenda kulipa TRA mwenyewe au mwajiri kuwa na sheet ambayo itakuwa na jina, TIN namba na PAYE ya kila mfanyakazi jambo ambalo ni usumbufu mkubwa na huweka ugumu wa ufuatiliaji
Kwa watu wa TRA ni rahisi kwao kufuatilia kwani wakitaka kujua nidhamu ya uwasilishaji wanaweza kuja kwenye shirika/ofisi na ku-sample baadhi ya salary slip na kuangalia kama kilochowalishwa TRA kwa kila mfanyakazi ni sawa na kilichopo
kwenye makato yao ya PAYE kwenye salary slip
Hivyo binafsi naona itakuwa na ugumu wa administration ya PAYE kama kila mfanyakazi atakuwa na TIN yake
Nionavyo mimi lakini and I stand to be ccorrect