Asanti. Nikumbushe ilipoandikwa hiyo stori ya Uno Maggy... Nakumbuka faintly, Unono alikuwa Meneja or something kwenye shirika la umma, na wazazi wake walipomtafuta kwa jina la Unono (mmojawao akipronounce 'Wunono'), walipata taabu kumpata kwa vile sasa alijitambulisha kama 'Uno Maggy', na akakana kuwatambua wazazi wake... Reading in 1980s, Sweet Memories.
By the way, pana kitabu kinaitwa "
Uasi wa Pakanga", nimekitafuta toka mwaka 1982, sikuwahi kukiona tena. Nilikisoma partially, mwenye kitabu akakichukua. Now I wish I could finish reading the story. Mkuu
Magonjwa Mtambuka
Kwanini Waafrika tunajidharau?
Ignore Watch
[IMG alt="Memtata"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/159/159427.jpg?1619246891[/IMG]
Member
Jul 27, 2013 74 400
Wengi wetu huamini sisi (Waafrika) ni dhaifu na bila mzungu tungekuwa bado tunavaa majani, binafsi sikubaliana na hili. Labda niwakumbushe, katika zama zote za binadamu wa kale alikuwa akipiga hatua kutoka moja kwenda nyingine, na wakati mkoloni anafika Afrika alitukuta tumeshahama kutoka zama za kuishi porini tukila mizizi na matunda kwenda katika kilimo na ufugaji na mbali zaidi tulikuwa na tawala zetu.
Kitu kingine ni mfumo wa elimu, tumecopy elimu ya kikoloni ambayo zaidi inaelezea mapungufu ya mtu mweusi kuliko maendeleo ya mtu mweusi kabla ya ukoloni. Naamini kabisa hata asingekuja mzungu bado tungekuwa tumepiga hatua kubwa sana, walichokosea wazee wetu ni kuacha maendeleo yao na kubweteka kusubiri mkoloni akuletee kisha yeye achukue mali zetu. Hii ndio inaendelea hadi ulimwengu wa sasa, tumewekeza kwenye ajira (kama lengo kuu) kuliko kwenye tafiti na uvumbuzi.
Wapo wanaoamini kila kitu amegundua mzungu, tunaamini hivyo kwasababu hatupendi kujifunza kuhusu tulipotoka ila tunaamini kile kilichoandikwa na mzungu zaidi, mf. tuliaminishwa (shuleni) kuwa mtu wa kwanza kuuona mlima Kilimanjaro alikuwa
Johannes Rebmann wakati amekuta watu wakiishi na kuwinda hapo. Japokuwa sasaivi wamebadili badala ya kusema “mtu wa kwanza kuvumbua mlima Kilimanjaro” wanasema “mzungu wa kwanza kuvumbua mlima Kilimanjaro”. Hii ni inanikumbusha scnene ya movie ya
Malcolm X akijadili dictionary ya kale katika tafsiri ya maneno
“white” and
“black”
White: (whit), adj. Of the color of pure snow;
reflecting all the rays of the spectrum. The
opposite of black, hence free from spot or
blemish; innocent, pure, without evil intent,
harmless. Honest, square-dealing, honorable.
Black: (blak), adj. Destitute of light, devoid
of color, enveloped in darkness. Hence, utterly
dismal or gloomy, as the future looked black.
Soiled with dirt, foul; sullen, hostile,
forbidding -- as a black day. Foully or
outrageously wicked, as black cruelty.
Indicating disgrace, dishonor or culpability.
Mfumo wetu wa elimu umetuandaa kuona mzungu ni bora kuliko mtu mweusi, ndomana hata leo hii watani zangu wasukuma wanatoa ng’ombe nyingi kwa binti mweupe kuliko yule mweusi, na si ajabu kuona dada zetu wanavyohangaika kujichubua na kuweka dawa nywele zao bila kujali wanadhurika kwa kiasi gani.
Sio kwamba kwasababu natumia simu kutoka ulaya, computer, gari n.k basi ndio nionekane dhaifu, wakati mwingine ni
kwasababu tunakosa fursa na si kwamba hatuna akili. Fikiria mwanzoni Amerika mtu mweusi hakuruhusiwa kusoma, kumiliki ardhi hata kushiriki michezo kitaifa na kimataifa lakini bado alipopata fursa hiyo alifanya vizuri sana japokuwa ilibidi uwe na uwezo mara kumi zaidi ya mzungu ili ushinde maana ukiwa na ushindi mwepesi ilikuwa ni rahisi kupindua matokeo. Kuna ambao walisingiziwa kesi za mauaji ili wasichukue ushindi mf. mwana masumbwi
Rubin "Hurricane" Carter (1937-2014) alisingiziwa kesi ya mauaji na alikaa jela kwa miaka 20 hadi alipokuja kuachiwa na ikagundulika alionewa.
Kuna wavumbuzi wengi sana wa Kiafrika ambao wengi hatuwajui na inawezekana kuna baadhi ya vitu tunaviona tunaamini vimevumbuliwa na wazungu.
Leo naorodhesha vitu vichache vilivyovumbuliwa na mtu mweusi (Black American):
- Improved Ironing Board, Invented by Sarah Boone in 1892
- Home Security System, Co-Invented by Mary Van Brittan Brown in 1966
- The Three-Light Traffic Light, Invented by Garrett Morgan in 1923
- Refrigerated Trucks, Invented by Frederick McKinley Jones in 1940
- Automatic Elevator Doors, Invented by Alexander Miles in 1887
- Electret Microphone, Co-Invented by James E. West in 1964
- Carbon Light Bulb Filament, Invented by Lewis Latimer in 1881
- Color IBM PC Monitor and Gigahertz Chip, Co-Invented by Mark Dean c. 1980 and 1999
(Source: History channel)
Mtata 🇨🇩
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
Reactions:
NestoryJ and Smart911
[IMG alt="Smart911"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/194/194588.jpg?1614162869[/IMG]
JF-Expert Member
Jan 3, 2014 55,293 2,000
Hakika na ni kweli kabisa...
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
Reactions:
Shunie
[IMG alt="My Next Thirty Years"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/633/633343.jpg?1622749947[/IMG]
Senior Member
May 12, 2021 179 250
Ili mtu akutawale ni lazima afanye yafuatayo. Ahakikishe HUJIAMINI, HUJITHAMINI na hatimaye HUJITAMBUI. Haya ndio mambo katika harakati ya wazungu kututawala, waliyafanya.
Leo Afrika yote majina yetu ni John, Anna, Jean, Abdulaziz na sio tena Masanja au Manka. Leo wadada wanavaa mawigi na kuwa na nywele kama za kizungu, leo tunajichubua rangi na kuwa 'weupe' hii yote ni kutojiamini.
Leo tunasomeshwa historia za ulaya na sio zetu, tunajua zaidi kuhusu Ottoman Empire na sio Milambo Empire, tumeacha elimu zetu za uvuvi na ufugaji badala yake tumeng'ang'ania elimu ambazo tukimliza tunazunguka na bahasha kutafuta kazi, wakati kijijini tuna mashamba na mazizi ya ng'ombe sababu hatujitambui.
Leo kwenye kampuni mzungu analipwa Mil 60 kwa mwezi huku wanaofanya kazi hasa wanalipwa laki nane, leo utafiti wa dawa zetu hatutaki eti ni za kishamba na tuliaminishwa ni za kishirikina sababu hatujithamini, hatujitambui na hatujiamini.
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
Reactions:
You, Mazindu Msambule, kilam and 1 other person
[IMG alt="Gamic"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/637/637380.jpg?1624604104[/IMG]
Member
Jun 24, 2021 8 45
Kweli Mkuu
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
JF-Expert Member
Nov 19, 2010 23,393 2,000
Memtata said:
Wengi wetu huamini sisi (Waafrika) ni dhaifu na bila mzungu tungekuwa bado tunavaa majani,
hata kuheshimu tu yaliyoandikwa kwenye katiba za nchi zetu hatuwezi - hayo maendeleo na heshima zitoke wapi?
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
Reactions:
Mazindu Msambule
[IMG alt="Magonjwa Mtambuka"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/378/378880.jpg?1548113618[/IMG]
JF-Expert Member
Aug 2, 2016 23,755 2,000
Kuna jamaa alikuwa anaitwa Unono Maganga lakini alipokwenda ulaya tu aliporudi akajibadilisha na kujiita Uno Maggy ilimradi tu aonekane amekuwa mzungu.
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
Reactions:
You
JF-Expert Member
Apr 1, 2020 576 1,000
Huwa najiuliza sijui itafikia kipindi na sisi tunarusha space craft, au kuwa na viwanda vya vitu kama electronics components au vifaa tiba maana kwa jinsi tulivyo labda lakini.
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
[IMG alt="Mlenge"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/0/450.jpg?1269740701[/IMG]
Verified Member
✅
Oct 31, 2006 2,130 2,000
Radio Butiama ukuye huku.
Sikiliza:
Post by Mlenge, user "Mlenge".
© 2006 - 2021 by Mlenge. All rights reserved.
Quote Reply
Select for moderation
Report Edit Delete
[IMG alt="Mlenge"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/0/450.jpg?1269740701[/IMG]
Verified Member
✅
Oct 31, 2006 2,130 2,000
Magonjwa Mtambuka said:
Kuna jamaa alikuwa anaitwa Unono Maganga lakini alipokwenda ulaya tu aliporudi akajibadilisha na kujiita Uno Maggy ilimradi tu aonekane amekuwa mzungu.
Wewe utakuwa ni muhenga... hicho kisa kilikuwa kwenye kitabu gani? Umenikumbusha mbali sana.
Post by Mlenge, user "Mlenge".
© 2006 - 2021 by Mlenge. All rights reserved.
Quote Reply
Select for moderation
Report Edit Delete
Reactions:
Magonjwa Mtambuka
[IMG alt="Mlenge"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/0/450.jpg?1269740701[/IMG]
Verified Member
✅
Oct 31, 2006 2,130 2,000
Lumoge said:
Huwa najiuliza sijui itafikia kipindi na sisi tunarusha space craft, au kuwa na viwanda vya vitu kama electronics components au vifaa tiba maana kwa jinsi tulivyo labda lakini.
Kiwanda cha sindano za kushonea space suit na Kaunda Suit tukishakuwa nacho, itakuwa ni hatua kubwa kuelekea huko.
Post by Mlenge, user "Mlenge".
© 2006 - 2021 by Mlenge. All rights reserved.
Quote Reply
Select for moderation
Report Edit Delete
[IMG alt="Magonjwa Mtambuka"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/378/378880.jpg?1548113618[/IMG]
JF-Expert Member
Aug 2, 2016 23,755 2,000
Mlenge said:
Wewe utakuwa ni muhenga...
Umepatia.
Thanks Quote Reply
Select for moderation
Report
[IMG alt="Mlenge"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/0/450.jpg?1269740701[/IMG]
Verified Member
✅
Oct 31, 2006 2,130 2,000
Asante. Nikumbushe ilipoandikwa hiyo stori ya Uno Maggy... Nakumbuka faintly, Unono alikuwa Meneja or something kwenye shirika la umma, na wazazi wake walipomtafuta kwa jina la Unono (mmojawao akipronounce 'Wunono'), walipata taabu kumpata kwa vile sasa alijitambulisha kama 'Uno Maggy', na akakana kuwatambua wazazi wake... Reading in 1980s, Sweet Memories.
By the way, pana kitabu kinaitwa "
Uasi wa Pakanga", nimekitafuta toka mwaka 1982, sikuwahi kukiona tena. Nilikisoma partially, mwenye kitabu akakichukua. Now I wish I could finish reading the story. Mkuu
Magonjwa Mtambuka nisaidie kama una nakala yake.
Attach files
Attach files
Similar Discussions
Share:
Facebook Twitter Reddit WhatsApp Email