Kwanini unasema huna mtaji? Ni kisingizio?

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,480
5,506
Leo nataka nigusie eneo tata na ambalo ni moja kati ya kitu kinatamkwa sana na vijana na watu wengine wanapotaka kufanya Biashara nalo ni ukosefu wa MTAJI.

Mtaji ni nini? Ni uwekezaji wa mmiliki katika biashara yake,yaani ni kile ambacho wewe mmiliki wa biashara unaingiza katika biashara yako,inaweza kuwa ni gari yako binafsi,nyumba yako, muda wako, akili yako, nguvu zako au vyote kwa pamoja. Katika zama hizi za utandawazi hata elimu na maarifa yako ni uwekezaji tosha katika biashara yako.Ili nieleweke vizuri ngoja nitoe mfano rahisi wa hili andiko langu.

Kuandaa hili andiko kumenihtaji mimi kufikiria kwa kina,kisha nikachukua muda kuandika na kisha nikapost hapa kwenye platform ya JF.Mimi sina PHD katika hili ninaloandika ila nina ufahamu wa kutosha wa kuweza kukuongoza wewe na kukushauri kidogo kuhusu uelekeo wa biashara. Iwapo utasoma andiko hili na kufikiri kwamba mimi naweza kufanya kazi na wewe basi utakuwa umekuwa mteja wangu katika biashara yangu.Ila uwekezaji wangu niliotumia ni muda na bundle,na akili kidgo ili kukuletea taarifa hii fupi tuijadili.

Mtaji sio mkopo, Mkopo katika biashara ni ni Liability yaani ni deni ambalo biashara inapaswa kulipa. Mtaji unatakiwa utoke kwa mmiliki, sisemi kwamba huwezi kukopa kuanzisha biashara hapana ila nasema kwamba unapokopa kuanzisha biashara yule mkopeshaji ndo mmiliki mpaka umalize kulipa deni, wewe utakuwa unamsaidia kusimamia tu.

Kwa kawaida hakuna biashata ambayo inaanzishwa bila mtaji,yaani lazima kuwe na input ili uweze kuwa na outpu. Sasa wengi huwa tunafikiri input lazima iwe ni pesa kumbe wakati mwingine kinachohitajika ni muda na akili basi. Chukulia mfano wa madalali wa nyumba na viwanja, wengi wao mtaji ni muda wao na mguu wao maisha yanaenda.

Leo nataka tujadili kwa uhalisia Je nini kifanyike ili kushughulika na hili tatizo la watu ama kukosa mitaji au kufikiri kwamba hawana mitaji?

Karibu tujadili
 
Tatizo ni biashara ngapi zinahitaji uwe na mtaji pesa na ambazo hazihitaji mtaji pesa? Ki ukweli biashara nyingi unakuta zinahitaji mtaji pesa, muda na akili na hapo ndo tatizo huanzia hapo.
 
Tatizo ni biashara ngapi zinahitaji uwe na mtaji pesa na ambazo hazihitaji mtaji pesa? Ki ukweli biashara nyingi unakuta zinahitaji mtaji pesa, muda na akili na hapo ndo tatizo huanzia hapo.

Sent from my Infinix X608 using JamiiForums mobile app
Mie nadhan hutakuwi kuwaza biashara kuubwa .huwez waza vifaa vyabujenz na huku huna hela..badala yake waza biashara ndogondogo ili ukue kwanza...
 
Mie nadhan hutakuwi kuwaza biashara kuubwa .huwez waza vifaa vyabujenz na huku huna hela..badala yake waza biashara ndogondogo ili ukue kwanza...
Mkuu, nakubaliana na wewe ili najua pia kwamba unaweza kuanzisha Biashara ya vifaa vya ujenzi mradi ujue tu utauza wapi Mfano.Wewe Unaweza kutembelea wamiliki wa H/W au wazalishaji wa vifaa vya Ujenzi ukatafuta Bargaining Power.

Kisha ukatatafuta Mafundi na Mabosi ukatengeneza Business Model ambayo Inawezesha wote hao kufaidika na wewe ukafaidika na ikawa Biashara
 
Mkuu kwa nfano me hitaji langu ni kutaka kufungua biashara ya begi na nguo za watoto, nitaanzaje bila mtaji pesa, je mtaji anzia utakuwa ni upi
Good;
Je unajua yanakopatikana hayo mabegi na bei zake na sifa zake na utofauti wake?

Je unajua walipo wateja wa mabegi na bajeti zao na mahitaji yao?
Je unajua kwa wastani utauza mabegi mangapi kwa siku,wiki au mwezi na utauza kwa bei gani?

Je unatarajia kupata faida kiasi gani kwa kila begi?
Je kwa kutumia hivo vipimo je Biashara yako inawezekana kuwapatia watu huduma/bidhaa na kuwaridhisha na kisha kukupa faida ya kutosha kukimu maisha yako?

Ukiweza kunijibu haya maswali basi wewe tayari unayo biashara na unao mtaji ili iwapo huna majibu ya hayo maswali basi tafuta majibu yake.Kama utapata majibu ya hayo maswali na bado usiwe na biashara ambayo inafanya kazi basi RUDI SHULE
 
Jamani hii ya kuanza bila mtaji mie ni muumini...kiukweli sio lazima biashara uanze na mtaji..kama ulovyosema mtaji ni kuwa Na muda na akili hili ndo wengi tunafeli hapa!

Sema tukitoa ushuhuda tutaitwa mamotivesheno supika 😒
Binti biashara gani hiyo ulianza bila mtaji tangiable!?
 
Biashara ndugu zangu ikijadiliwa hap kla kitu kitakuw "positive" kwa point, lakin uhalisia haupo hivyo... huo udalal mnaousema nyinyi atakaeshawishka kuufanya ataanza n mtaji wa kiwanja changu.. aje PM kwa maelezo zaidi alaf tuone! Nyinyi mnafanya masikhara nyinyii.
 
Biashara ndugu zangu ikijadiliwa hap kla kitu kitakuw "positive" kwa point, lakin uhalisia haupo hivyo... huo udalal mnaousema nyinyi atakaeshawishka kuufanya ataanza n mtaji wa kiwanja changu.. aje PM kwa maelezo zaidi alaf tuone! Nyinyi mnafanya masikhara nyinyii
Mkuu,Naelewa Frustration Zako.Biashara yangu ya kwanza nilianza kusaka wateja January nikaja kupata mteja wa kwanza September.Hakuna biashara ambayo ni rahisi hata hio ya udalali.

Tupe Sifa ya kiwanja chako kilipo na Bei yake theni Mimi na wengine ambao wamependa hio challenge yako tutajaribu kutumia huo mtaji.

NB.Hakuna biashara rahisi.
 
Jamani hii ya kuanza bila mtaji mie ni muumini...kiukweli sio lazima biashara uanze na mtaji..kama ulovyosema mtaji ni kuwa Na muda na akili hili ndo wengi tunafeli hapa!

Sema tukitoa ushuhuda tutaitwa mamotivesheno supika 😒
Labda biashara ya pu.ssy ndio haitaji mtaji
 
Mkuu,Naelewa Frustration Zako.Biashara yangu ya kwanza nilianza kusaka wateja January nikaja kupata mteja wa kwanza September.Hakuna biashara ambayo ni rahisi hata hio ya udalali.

Tupe Sifa ya kiwanja chako kilipo na Bei yake theni Mimi na wengine ambao wamependa hio challenge yako tutajaribu kutumia huo mtaji.

NB.Hakuna biashara rahisi.
N wengine mje pm mpate hela huku
 
hivi udalali ni biashara? Mim nadhani neno biashara na neno dalali au udalali ni vitu viwili tofauti.
kwako kama siyo biashara kwa wengine ni biashara wanaingiza pesa

na kupitia hapo anaweza kuwa muhusika kwenye hiyo biashara
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom