Kwanini unaniacha wakati nakuhitaji?

Kwanini unaniacha wakati nakuhitaji?

Habari Waungwana
Najuwa wapo watakaonibeza na kunidharau ila haya yalionikuta usiombe yakufike yasikie tuu kwa mwenzako maana mzigo wa mwenzako ni polo la usufi.

Naamini hakuna mahusiano ambayo hayana Changamoto ila mengine Kiboko siku ya 30/12/2020 nimeachwa na mke wangu bila ya sababu ya msingi na kuondoka na watoto wangu 2 ambao mmoja yuko na miaka 5 na mwengine ni miaka 2. Kwa hakika ni kuwa hakuna kosa la msingi tulipishana na lugha tuuu akanuna kwa siku 3 nikimpigia simu asubuhi hapokei na mimi nilikua safarini basi na mimi kama hakupokea simu humtumia sms na kumpigia tena siku itayofuata asubuhi.

Baada ya siku tatu nilisikia kutoka kwa ndugu wa familia kuwa mke wako anakunja vyombo nikajibu sawa ila baada ya muda alinitumia sms kuwa siku inayofuata atondoka na mimi sikujibu, akanipigia simu akaniuliza hivi "kesho mimi naondoka mchana unataka nikuachie kitu gani chako nisikichukue" na mimi nikamjibu " niachie wanangu tuuu " akasema kuwa hatowaacha siku iliyofuata nilifunga safari kurudi nyumbani saa 10 za jioni nilimkuta ameshavaa yeye na watoto kwa ajili ya safari nikamuita ndani na kumuliza kwa nini unaondoka akajibu kuwa nimemtolea jeuri nikamuambia basi yaishe akagoma na akaondoka na wanangu. Ndani amekunja nguo zake zote na za wanawe, chumbani kaacha vyombo tuuu kasema atakuja kufuata siku nyengine.

Naomba ushauri wenu kwa hakika bado namuhitaji hasa siwezi kuwa mbali na wanangu, wengine wanasema nimpotezee tuuu na watoto wakikua watanitafuta ila moyo wangu haukubali, nimesema nimpelekee chakula maana kwao sio safi sana wengine wanasema nisimpelekee ili ajifunze maisha kwa hakika niko njiia panda usiku umekua mkubwa nipeni mawazo.

Natanguliza shukrani
Nina imani kuwa huyo mwanamke ana akili timamu na wazo la kuondoka kwako ni lake yeye mwenyewe. Ninahisi atakuwa kapata mtu wa kumchezea akili na hisia zake huko aendako....jamaa akimchoka na kumsaliti baada ya kumla atarudi kwako huku akilia. Njaa mbaya wewe usisiskie...mara nyingi wanawake wenyewe ndiyo huharibu ndoa zao kwa ajili ya tamaa ya shilling 1000 tu ya mshikaki na muhogo wa kuchoma.
 
Brother c kwamba una mapenzi na wanao tu hapana unampenda mkeo sana, ila mapenzi uliyonayo hayo yatakuua. Ningekuwa mimi hata matumizi ya watoto nisingetoa bila yeye kuniomba, ningemlia kimya nikafunga Vioo kabisa, na anayemuharibu ni Shost yake mama yake.

Hukupeleka mahari kwa mama yake bali ulipeleka kwa baba. Mimi hata kwa mama mkwe nisingekanyaga. Since ushamwambia baba usithubutu kupiga simu au sms hizo zinakuchora. Siku ya kikao chenu usikubali kifanyikie kwa mama kifanyikie kwa baba basi. Ukimkazia huyu atakuheshimu ila usipomkazia utakuwa shamba boy kwako
 
Brother c kwamba una mapenzi na wanao tu hapana unampenda mkeo sana, ila mapenzi uliyonayo hayo yatakuua. Ningekuwa mimi hata matumizi ya watoto nisingetoa bila yeye kuniomba, ningemlia kimya nikafunga Vioo kabisa, na anayemuharibu ni Shost yake mama yake,Hukupeleka mahali kwa mama yake bali ulipeleka kwa baba. Mimi hata kwa mama mkwe nisingekanyaga. Since ushamwambia baba usithubutu kupiga simu au sms hizo zinakuchora. Siku ya kikao chenu usikubali kifanyikie kwa mama kifanyikie kwa baba bas. Ukimkazia huyu atakuheshimu ila usipomkazia utakuwa shamba boy kwako

Asante nitaufanyia kazi ushauri wako asante
 
Habari Waungwana
Najuwa wapo watakaonibeza na kunidharau ila haya yalionikuta usiombe yakufike yasikie tuu kwa mwenzako maana mzigo wa mwenzako ni polo la usufi.

Naamini hakuna mahusiano ambayo hayana Changamoto ila mengine Kiboko siku ya 30/12/2020 nimeachwa na mke wangu bila ya sababu ya msingi na kuondoka na watoto wangu 2 ambao mmoja yuko na miaka 5 na mwengine ni miaka 2. Kwa hakika ni kuwa hakuna kosa la msingi tulipishana na lugha tuuu akanuna kwa siku 3 nikimpigia simu asubuhi hapokei na mimi nilikua safarini basi na mimi kama hakupokea simu humtumia sms na kumpigia tena siku itayofuata asubuhi.

Baada ya siku tatu nilisikia kutoka kwa ndugu wa familia kuwa mke wako anakunja vyombo nikajibu sawa ila baada ya muda alinitumia sms kuwa siku inayofuata atondoka na mimi sikujibu, akanipigia simu akaniuliza hivi "kesho mimi naondoka mchana unataka nikuachie kitu gani chako nisikichukue" na mimi nikamjibu " niachie wanangu tuuu " akasema kuwa hatowaacha siku iliyofuata nilifunga safari kurudi nyumbani saa 10 za jioni nilimkuta ameshavaa yeye na watoto kwa ajili ya safari nikamuita ndani na kumuliza kwa nini unaondoka akajibu kuwa nimemtolea jeuri nikamuambia basi yaishe akagoma na akaondoka na wanangu. Ndani amekunja nguo zake zote na za wanawe, chumbani kaacha vyombo tuuu kasema atakuja kufuata siku nyengine.

Naomba ushauri wenu kwa hakika bado namuhitaji hasa siwezi kuwa mbali na wanangu, wengine wanasema nimpotezee tuuu na watoto wakikua watanitafuta ila moyo wangu haukubali, nimesema nimpelekee chakula maana kwao sio safi sana wengine wanasema nisimpelekee ili ajifunze maisha kwa hakika niko njiia panda usiku umekua mkubwa nipeni mawazo.

Natanguliza shukrani
Huyo mwache aende mbona atarudi mwenyewe tu
 
Baba na mama yake wameshatengana, wewe ni nani hata usitengwe!
 
Halafu acha lugha ya ubinafsi kwa watoto, kila kitu watoto wangu watoto wangu... ni watoto 'wenu' sio watoto wako.
 
Inabidi umtafute mama akiwa peke yake muyajenge, ikibidi andaa vitenge vya kutosha.

Ukiweka na kiasi cha kueleweka (cash) wife anarudi haraka sana.

Ila baada ya hapo inabidi wewe na huyo mama na mkeo muwe na ukaribu mzuri, ikibidi kila mwezi uwe na bajeti yake, hii itasababisha mama asimshauri mwanae kuondoka kwako, maana anafaidika na wewe.

Ila ukimkaushia ndo anakufanyia haya.

Unamshauri ujinga, huwezi kuishi kwa kujilamba kwa mama mkwe namna hiyo... hiyo si sawa.
 
Unamshauri ujinga, huwezi kuishi kwa kujilamba kwa mama mkwe namna hiyo... hiyo si sawa.

Mkuu kwenye ushauri tofauti tofauti ndipo mtu unachagua ushauri unaokidhi hitaji lako.

Kumbuka hapa tunatoa ushauri bila kuwa na taarifa za pande zote, hivyo tutakuwa tunajitahidi kutafuta suluhu.

Halafu nikupe ushauri, jifunze jinsi ya ku-address kitu kilicho tofauti na mawazo yako kiustaarabu, haikupunguzii kitu.
 
Kama ni mtu wa Dodoma aisee achana naye narudia tena achana naye utaumiza kichwa mwili muda utapoteza Ila hatarudi nikuashauri Tu fanya kama unapotezea wanao wataletwa Ila mwanamke hutampata na hakupendi jua hilo Tu hakupendi utapambana utashindwa ni ayo Tu pole sana
 
Inabidi umtafute mama akiwa peke yake muyajenge, ikibidi andaa vitenge vya kutosha.

Ukiweka na kiasi cha kueleweka (cash) wife anarudi haraka sana.

Ila baada ya hapo inabidi wewe na huyo mama na mkeo muwe na ukaribu mzuri, ikibidi kila mwezi uwe na bajeti yake, hii itasababisha mama asimshauri mwanae kuondoka kwako, maana anafaidika na wewe.

Ila ukimkaushia ndo anakufanyia haya.
Hivi wanaume wengine mko Sawa kweli, vipi mama yake akifariki mtu kama hajui umuhimu wa ndoa haezi kubadilika na ushauri Tu ukiona mwanamke kalelewa Sana na mama yake muogope kama ukoma amuweke mama karibu kwani kamuowa yeye apo hapendwi aangakie ustaarabu mwingine maisha mengine tunajipa stress Tu alafu tumamsingizia Muumba wakati akili tumepewa za kuchanganua
 
Huyu mwanamke ana gubu, hana subira, hana hekima wala hana busara..... Nakushangaa unavyolialia kuhusu mtu wa namna hii
Mimi siku zote humsamehe ila yeye hufutuka, kuna siku alilalamika hana nguo nikamuambia nitakununulia mwisho wa mwezi kwani hali ya maisha sio sawa akalalamika nikamuambia mbona mambo yalipokuwa safi ulikua husemi nakununulia basi alisema nimemsumbulia na akavhukuq nguo zote nilizomnunuliq na kuzipeleka kwa mama angu kwangu lilikuq tusi kubwa ila nilimsamehe
 
Basi Acha nikupe Hali halisi.

It seems sasa hivi hapo home maisha yameyumba kidogo... Ambayo ni kawaida na hasa kwa mwaka huu.

Sasa inabidi ujikaze kiume hata Kama unampenda for the sake of the kids. Ukimuendekeza kuwa anaondoka Kila Mara watakaoteseka Ni wanao sababu itawakosti Hadi shule.

So nakushauri ujikaze. Kata mawasiliano na yeye. Usimpigie, usimtext, mkaushie. Hela ya matumizi mtumie then kausha. Uchune kabisa. Akikupigia pokea lakini make it short na kuhusu watoto tu. Then kata na akipiga usipokee tena.

Kwao usiende eti kumfata arudi. Acha akae akili atarudi mwenyewe. Bahati nzuri watoto bado wadogo.

Mwanamke ganii unataka kumnyayansa mumeo kisa ameyumba kimaisha. Uchukue nguo alizokununulia kweli umpelekee Mamake mzazi? With no shame at all? Sio sahihi.

Man Up ndugu! For the sake of your kids. Weka mapenzi pembeni.
Asipozingatia haya mtoa mada atakuwa zumbukuku ulimwengu upo huku
 
Habari Waungwana
Najuwa wapo watakaonibeza na kunidharau ila haya yalionikuta usiombe yakufike yasikie tuu kwa mwenzako maana mzigo wa mwenzako ni polo la usufi.

Naamini hakuna mahusiano ambayo hayana Changamoto ila mengine Kiboko siku ya 30/12/2020 nimeachwa na mke wangu bila ya sababu ya msingi na kuondoka na watoto wangu 2 ambao mmoja yuko na miaka 5 na mwengine ni miaka 2. Kwa hakika ni kuwa hakuna kosa la msingi tulipishana na lugha tuuu akanuna kwa siku 3 nikimpigia simu asubuhi hapokei na mimi nilikua safarini basi na mimi kama hakupokea simu humtumia sms na kumpigia tena siku itayofuata asubuhi.

Baada ya siku tatu nilisikia kutoka kwa ndugu wa familia kuwa mke wako anakunja vyombo nikajibu sawa ila baada ya muda alinitumia sms kuwa siku inayofuata atondoka na mimi sikujibu, akanipigia simu akaniuliza hivi "kesho mimi naondoka mchana unataka nikuachie kitu gani chako nisikichukue" na mimi nikamjibu " niachie wanangu tuuu " akasema kuwa hatowaacha siku iliyofuata nilifunga safari kurudi nyumbani saa 10 za jioni nilimkuta ameshavaa yeye na watoto kwa ajili ya safari nikamuita ndani na kumuliza kwa nini unaondoka akajibu kuwa nimemtolea jeuri nikamuambia basi yaishe akagoma na akaondoka na wanangu. Ndani amekunja nguo zake zote na za wanawe, chumbani kaacha vyombo tuuu kasema atakuja kufuata siku nyengine.

Naomba ushauri wenu kwa hakika bado namuhitaji hasa siwezi kuwa mbali na wanangu, wengine wanasema nimpotezee tuuu na watoto wakikua watanitafuta ila moyo wangu haukubali, nimesema nimpelekee chakula maana kwao sio safi sana wengine wanasema nisimpelekee ili ajifunze maisha kwa hakika niko njiia panda usiku umekua mkubwa nipeni mawazo.

Natanguliza shukrani
Pole Sana, kwa kipindi hiki, usimfuatilie, huenda ikawa bado ana hasira na wewe au pengine kuna mtu anampotosha, jipe hata miezi 3, kuhusu watoto, usiwe na shaka, watakula na watavaa vizuri tu, naamini kabla ya mkeo kufanya hayo maamuzi, alikwishajipanga na huenda kuna mfadhili, MUNGU akutie nguvu kwakuwa ni mambo yanayoumiza Sana.
 
Tuliza akili, jifanye umepotezea, kimya hata mwaka mzima - atajileta na kuomba msamaha. Najua utaumia hasa watoto wako ila jipe moyo.
 
Daah niseme wewe umeolewa kimwili na kiakili yaani kama ni zobe au zombi una viwango. Hongera sana kwa mahaba niue
 
Kuna maswali mawili ya msingi inabidi ujiulize na ujijibu kwa uwazi

Je umemkosea sana au kawaida? Kama umemkosea sana basi shuka mbembeleze hata kwa kutumia mtu anayemuheshimu

ILA nasema tena ILA kama ameondoka kwa sababu ya kawaida na kibr ndani yake ni bora aondoke moja kwa moja kuliko wewe kujishusha maana kwa kujishusha kwako uta prove udhaifu ambao ndo itakuwa mwanzo wa kupoteza heshima yako kama mwanaume...

Mwanaume msimamo. Na msimamo ni kitu kidogo ukikiangalia but trust me ni muhimu sana
 
Back
Top Bottom