mahirtwahir
JF-Expert Member
- Jan 12, 2013
- 614
- 322
Habari Waungwana
Najuwa wapo watakaonibeza na kunidharau ila haya yalionikuta usiombe yakufike yasikie tuu kwa mwenzako maana mzigo wa mwenzako ni polo la usufi.
Naamini hakuna mahusiano ambayo hayana Changamoto ila mengine Kiboko siku ya 30/12/2020 nimeachwa na mke wangu bila ya sababu ya msingi na kuondoka na watoto wangu 2 ambao mmoja yuko na miaka 5 na mwengine ni miaka 2. Kwa hakika ni kuwa hakuna kosa la msingi tulipishana na lugha tuuu akanuna kwa siku 3 nikimpigia simu asubuhi hapokei na mimi nilikua safarini basi na mimi kama hakupokea simu humtumia sms na kumpigia tena siku itayofuata asubuhi.
Baada ya siku tatu nilisikia kutoka kwa ndugu wa familia kuwa mke wako anakunja vyombo nikajibu sawa ila baada ya muda alinitumia sms kuwa siku inayofuata atondoka na mimi sikujibu, akanipigia simu akaniuliza hivi "kesho mimi naondoka mchana unataka nikuachie kitu gani chako nisikichukue" na mimi nikamjibu " niachie wanangu tuuu " akasema kuwa hatowaacha siku iliyofuata nilifunga safari kurudi nyumbani saa 10 za jioni nilimkuta ameshavaa yeye na watoto kwa ajili ya safari nikamuita ndani na kumuliza kwa nini unaondoka akajibu kuwa nimemtolea jeuri nikamuambia basi yaishe akagoma na akaondoka na wanangu. Ndani amekunja nguo zake zote na za wanawe, chumbani kaacha vyombo tuuu kasema atakuja kufuata siku nyengine.
Naomba ushauri wenu kwa hakika bado namuhitaji hasa siwezi kuwa mbali na wanangu, wengine wanasema nimpotezee tuuu na watoto wakikua watanitafuta ila moyo wangu haukubali, nimesema nimpelekee chakula maana kwao sio safi sana wengine wanasema nisimpelekee ili ajifunze maisha kwa hakika niko njiia panda usiku umekua mkubwa nipeni mawazo.
Natanguliza shukrani
Najuwa wapo watakaonibeza na kunidharau ila haya yalionikuta usiombe yakufike yasikie tuu kwa mwenzako maana mzigo wa mwenzako ni polo la usufi.
Naamini hakuna mahusiano ambayo hayana Changamoto ila mengine Kiboko siku ya 30/12/2020 nimeachwa na mke wangu bila ya sababu ya msingi na kuondoka na watoto wangu 2 ambao mmoja yuko na miaka 5 na mwengine ni miaka 2. Kwa hakika ni kuwa hakuna kosa la msingi tulipishana na lugha tuuu akanuna kwa siku 3 nikimpigia simu asubuhi hapokei na mimi nilikua safarini basi na mimi kama hakupokea simu humtumia sms na kumpigia tena siku itayofuata asubuhi.
Baada ya siku tatu nilisikia kutoka kwa ndugu wa familia kuwa mke wako anakunja vyombo nikajibu sawa ila baada ya muda alinitumia sms kuwa siku inayofuata atondoka na mimi sikujibu, akanipigia simu akaniuliza hivi "kesho mimi naondoka mchana unataka nikuachie kitu gani chako nisikichukue" na mimi nikamjibu " niachie wanangu tuuu " akasema kuwa hatowaacha siku iliyofuata nilifunga safari kurudi nyumbani saa 10 za jioni nilimkuta ameshavaa yeye na watoto kwa ajili ya safari nikamuita ndani na kumuliza kwa nini unaondoka akajibu kuwa nimemtolea jeuri nikamuambia basi yaishe akagoma na akaondoka na wanangu. Ndani amekunja nguo zake zote na za wanawe, chumbani kaacha vyombo tuuu kasema atakuja kufuata siku nyengine.
Naomba ushauri wenu kwa hakika bado namuhitaji hasa siwezi kuwa mbali na wanangu, wengine wanasema nimpotezee tuuu na watoto wakikua watanitafuta ila moyo wangu haukubali, nimesema nimpelekee chakula maana kwao sio safi sana wengine wanasema nisimpelekee ili ajifunze maisha kwa hakika niko njiia panda usiku umekua mkubwa nipeni mawazo.
Natanguliza shukrani