Nashangazwa na hii hali. Kwanini tusubiri matukio ndio yatuibulie mijadala juu ya mambo muhimu kama kiwango cha elimu. Je, kama matokeo ya mwaka huu yangekuwa wanafunzi wamepasi kwa asilimia 80 tungesema kuwa madarasa yasiyo na madawati, shule zisizo na maabara, walimu wanaokaririsha majibu na wanafunzi wasio na maadili ndio vinaleta ushindi? Kwanini, mitihani ndio kipimo chetu cha elimu?