Kwanini tunashusha bendera yetu ya Taifa?

Duh!
 
PIa iwepo amri ni marufuku kupandisha au kushusha bendera ya Nchi ukiwa umevaa ndala! BALI ya ccm wanaweza shusha au kupandisha na ndala.
 
Swali la Nyongeza:-

Iweje basi kwenye mkesha wa Mwenge bendera hiyo hiyo ya Taifa haishushwi? Pale hupepezwa usiku kucha. Why?

Maswali haya yangejibiwa vizuri na watu wa Itifaki.
 
Is it semantical to use historical instead of history?
Hata mimi nililiona kosa hilo lakini ilibidi nipite tu nikizingatia aliyepost yupo kwenye umoja wa kupinga kila kitu. They never appreciate even when corrected in their common mistakes.
 
Mimi binafsi japokuwa sio mtaalam wa protokali nafikiria kuna simple logic ya kuishusha bendera kila siku badala ya kuipandisha milele.

Ni kwamba, kile ni kitambaa. Kinapeperuka kutokana na upepo. Upo uwezekano wa kitambaa hicho kuchanwa na upepo mkali. Na pia upo uwezekano wa kitambaa hicho kuchoka tu na kuanza kuchanika kidogo kidogo. Sasa badala ya kuiacha ichanike hadi ianze kuning'inia ovyo ovyo vipande vipande, jambo ambalo linaweza kutafsiriwa kuwa ni uchovu wa nchi, basi ndio maana kuna kuishusha kila siku. Ni katika kuishusha huko ndiko wahusika wanapata nafasi ya kuitazama kama ina kasoro zozote na kuzirekebisha mara moja. Ikiwa itashindikana kurekebishwa basi kesho yake alfajiri hupandishwa nyingine isiyo na kasoro.

Ni mtazamo wangu huu wa kienyeji kabisa na wala sio mtaalam wa itifaki mimi.
 
Haahahahahaaaa, yaani ni shida sana maana hata kiswahili hatujui. Mimi kuna mzungu alinitoa nishai wakati tunagonga kiswahili hadi aibu.
Kiswahili hatujui, kiingereza tunacholazimisha ni Mungu tuhurumie basi ni taabu tupu
 
Hivi ukiwa na bendera yako tofauti na ya Taifa na isiyo ya kisiasa kwa Tanzania na yenyewe unatakiwa uishushe usiku?

Au bongo hairuhusiwi kuwa na bendera binafsi kama ya kampuni kwa mfano?
 
Hivi ukiwa na bendera yako tofauti na ya Taifa na isiyo ya kisiasa kwa Tanzania na yenyewe unatakiwa uishushe usiku?

Au bongo hairuhusiwi kuwa na bendera binafsi kama ya kampuni kwa mfano?
Hakuna pingamizi la kumiliki bendera binafsi.
 
naamini jibu sahihi ni hili hapa, ila mkuu swalo nyongeza kuna hoja humu kuwa bendera za jeshi hipandishwa jioni nankushushwa asubuhi, unaweza fahamu kwani inakuwa hivyo
 
Hili jibu linajitosheleza kabisaaaa...
 
Hili jibu linajitosheleza kabisaaaa...
 
Na yenyewe bendera binafsi inatakiwa kushushwa na kupandishwa mawio na machweo?


Kushusha au kupandisha bendera binafsi ni uamuzi wako tu ukitaka hata wakati wa kula shusha nusu mlingoti na ukienda chooni shusha kabisa ni wewe tu. kumbuka hiyo unayoiita kuwa bendera binafsi kwa wengine ni daso kama yalivyo madaso mengi tu hakina maana yeyote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…