Kwanini tunashusha bendera yetu ya Taifa?

Kwanini tunashusha bendera yetu ya Taifa?

Sawa sawa Ritz, sasa kwa nini hiyo bendera ya Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama haipandishwi sehemu zote bendera ya Taifa inaposhushwa, kuashiria sasa nchi ipo chini ya himaya yake?🙁🙁

Halafu unapozungumzia majeshi ya ulinzi na usalama ni mpaka polisi au😵

Mbona maeneo ya vituo vya polisi hawapandishi bendera yao? Au wao siyo sehemu ya jeshi la usalama wa nchi??
Mkanda wa Jeshi la Polisi una rangi gani.
 
Mtoa mada
Kwanza nikupe historia fupi kuhusu bendera.
Matumizi ya bendera yalianza miaka mingi huko nyuma hasa kwenye mapambano na mapigano ya kivita.
Nchi nyingi zilianza kutumia bendera katika karne ya kumi na nane.
Aina ya bendera,namna ya kuipandisha na kuihifadhi inaongozwa ni swala la kiprotokali zaidi.
Zipo protokali ambazo nchi zote zinafuata.
1. Bendera kuwa na umbo la mstatiri
2. Nguzo ya bendera kuwa wima
3. Heshima na matumizi stahiki ya bendera

Kuna mengi ila kwa sababu ya muda nitamalizia mengine nikifika ofisini.
Tuje kwenye swali
Bendera Za taifa zina mambo makubwa mawili
1. kuonyesha uhuru wa nchi na utambulisho wake.Ukiwa UN hutakuta bendera ya Zanzibar kwa kuwa UN haiitambui Zanzibar kama nchi.
2. kuonyesha mamlaka
Kupandisha bendera asubuhi na kuishusha jioni inafanywa hivi kwa mazoea ambayo nchi nyingi imekuwa nazo.
Bendera kwa kuwa ni alama inapaswa kuwekwa mahali ambapo itaoneka na muda ambao itaonekana.
Hivyo nchi nyingi hazipeperushi bendera usiku kwa sababu ya giza. Mfano India pia wanashusha bendera usiku.
Mfano Marekani wao kama bendera inapepea usiku basi hilo eneo lazima liwe na mwanga wa kuifanya bendera hiyo ionekane la sivyo lazima ishushwe. Kwa waliofika Marekani watakubaliana na mimi hapa.


Note. BENDERA kushushwa usiku haina uhusiano wowote na mamlaka ya Rais wala Jeshi la Ulinzi ni utaratibu wa kiprotokali usioathiri nguvu wala majukumu ya Rais ama taasisi yoyote ya Serikali.

Nitarudi baadaye.

Umetisha xn mkuu!!!
Nimejifunza vitu ving xn hapa lkn bila kusahau kuwa asilimia nying za wadau humu wana jibu vitu hata kama hawana elimu nalo so inanipa shaka kubwa kuwa hata nyuzi nyingi zinazopandishwa humu na kujadiliwa bas hujadiriwa kwa Mihemuko na sio ujuzi wa kile kilichoandikwa!!!
LAAM RASHID kaleta maada ambayo haina siasa ndani yake lkn watu wanajibu kama vile wajuzi xn kunbe hawajui kitu so Nakupa pongezi mkuu kwa jinsi ulivojibu hata kama mimi sina ujuzi na hicho ulichokijibu lkn umejitahid kujibu swali lililoulizwa na sio kama wengne humu!!!
 
Anazungumzia giza? mbona kuna taasisi zinafanya kazi nyakati za usiku? na wakati huohuo bendera ya Taifa imeshashushwa.
Lakini mie naona kama nchi yetu historia haijakaa sawa, make ata wale wanajeshi wanaopandishisha bandera yao jioni na kuishusha asubuhi hawajui ni kwanini.
Hiyo bendera ya jeshi hupandishwa wap?
 
Kuanzia saa 12 asubuhi, mpaka saa 12 jioni nchi inakuwa kwenye himaya ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ndiyo maana ikifika muda huo siyo bendera ya Taifa tu, bali hata ile ya Rais huwa inashushwa kuashiria kuwa sasa TPDF Tanzania people defence foces nchi ipo kwenye himaya yao na bendera ya mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa nchi inapandishwa mara moja.
Hio bendera ya jeshi sijawahi kuiona....inapandishiwa wapi mkuu na mimi niione japo mara moja
 
katiba haitoi utaratibu, naona watu wengi hawajua nini maana ya katiba, wakizani kila kitu kimeandikwa kwenye katiba, pia hawajui tofauti ya katiba na sheria nyingine, ndiyo maana hata wakati wa kutoa maoni ya katiba mpya kila mtu alisema la kwake akidhani katiba inaandika kila kitu. kuna vitu vingine vingi haviandikwi kwenye katiba, na katiba ingekuwa inaandika kila kitu sijui ingekuwa na ukubwa gani

...thank you, writing under pressure
Wabongo wengi wamezoea ushabiki, kuelezea mambo wasiyoyasoma. Wanadhani kujua sheria ni jukumu la Wanasheria tu.
 
Kuanzia saa 12 asubuhi, mpaka saa 12 jioni nchi inakuwa kwenye himaya ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ndiyo maana ikifika muda huo siyo bendera ya Taifa tu, bali hata ile ya Rais huwa inashushwa kuashiria kuwa sasa TPDF Tanzania people defence foces nchi ipo kwenye himaya yao na bendera ya mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa nchi inapandishwa mara moja.
Hapo sawa mkuu nimekupata safi kabisa coz hata mm nilikuwa cjui hyo
 
Hio bendera ya jeshi sijawahi kuiona....inapandishiwa wapi mkuu na mimi niione japo mara moja
images-40.jpeg

Hiyo hapo.
 
Kuanzia saa 12 asubuhi, mpaka saa 12 jioni nchi inakuwa kwenye himaya ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ndiyo maana ikifika muda huo siyo bendera ya Taifa tu, bali hata ile ya Rais huwa inashushwa kuashiria kuwa sasa TPDF Tanzania people defence foces nchi ipo kwenye himaya yao na bendera ya mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa nchi inapandishwa mara moja.
Huwa inapandishwa wapi? Kwahiyo usiku nchi huwa inatawaliwa kijeshi?
 
your question is illogical and some sort of non sense, the threader has a well reasoned question, why you are asking for his age does not make sense, and i don't see the relationship between the history of our country and the raising/lowering of the national flag, besides the subject (History) is no where teaching about raising/lowering of the flag, if you were to ask, you probably asked "who was your civics teacher?"
He wanted to belittle the other guy but ended up writing broken English. He wanted to sound sarcastic by mocking the other fellow, but instead he becomes a laughing stock.
 
Back
Top Bottom