Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,221
- 79,514
Wapendwa wana jamiiforums, imefika wakati tutafakari kuhusu mwenendo wa taasisi zetu mbili yaani Wizara ya Fedha na Benki Kuu zilizo mihimili mikuu ya mustakabali wetu wa kujikimu hapa nchini! Wakati hali halisi ya mfumuko wa bei inaonekana wazi kila kukicha Gavana wetu Mkuu anasema uchumi uko katika hali nzuri yaani katika akiba za kigeni wakati huo huo hafafanui huu mfumuko unatoka wapi!? Vilevile inayofanywa siri kuhusu mapungufu ya bajeti 2010/2011 na Mh Mkulo si siri tena bali ni ufahamu wa kila mtu wafadhili wa bajeti yetu wamekataa kutoa hela kama walivyohaidi haswa kwa sababu ya kuona hali hairidhishi katika utawala wa nchi hii haswa kuhusu swala zima la uwazi, uwajibikaji na mabadiliko kuelekea mfumo bora wa utawala!
Sasa ni kwanini kama wananchi wa nchi tunafichwa haya? au mpaka wanafunzi waandamane kuhusu fedha za kujikimu zisizotosha tena kutokana na kupanda kwa gharama za maisha kusikodhibitiwa? Au mpaka wafanyakazi waanze nao migomo maana naskia sasa hata mishahara inachelewa kutoka na hata wale walioongezewa wanalipwa mishahara ya zamani! Hivi haki yetu sisi ipo wapi? katika kujua mustakabali wa mambo yanayotuhusu sisi moja kwa moja? Hivi huu uchakachuaji hata wa hali halisi ya uchumi utaendelea hadi lini na kwanini Mh Mkulo anakuwa mtu wa mipasho na si mtu mwenye wajibu kuueleza umma ni nini kinaendelea? Imekuwa tabia ya Mh huyu kuwa mkali pasipo sababu anapoulizwa swala lolote la bajeti na amekuwa akitumia maneno kama "uwongo!?" au "umeskia wapi?" anapoulizwa kuhusu mapungufu makubwa ya bajeti yanayolikabili Taifa kwa sasa! naombeni tutafakari haki yaetu iko wapi katika serikali hii ya usiri isiyo shirikishi katika kueleza yanayojiri kabla mambo hayajafumuka!
Sasa ni kwanini kama wananchi wa nchi tunafichwa haya? au mpaka wanafunzi waandamane kuhusu fedha za kujikimu zisizotosha tena kutokana na kupanda kwa gharama za maisha kusikodhibitiwa? Au mpaka wafanyakazi waanze nao migomo maana naskia sasa hata mishahara inachelewa kutoka na hata wale walioongezewa wanalipwa mishahara ya zamani! Hivi haki yetu sisi ipo wapi? katika kujua mustakabali wa mambo yanayotuhusu sisi moja kwa moja? Hivi huu uchakachuaji hata wa hali halisi ya uchumi utaendelea hadi lini na kwanini Mh Mkulo anakuwa mtu wa mipasho na si mtu mwenye wajibu kuueleza umma ni nini kinaendelea? Imekuwa tabia ya Mh huyu kuwa mkali pasipo sababu anapoulizwa swala lolote la bajeti na amekuwa akitumia maneno kama "uwongo!?" au "umeskia wapi?" anapoulizwa kuhusu mapungufu makubwa ya bajeti yanayolikabili Taifa kwa sasa! naombeni tutafakari haki yaetu iko wapi katika serikali hii ya usiri isiyo shirikishi katika kueleza yanayojiri kabla mambo hayajafumuka!