Hii jumuiya mfu Faida zake ni kiduchu sana ukilinganisha na hasara lukuki.
Misingi ya kujiunga na jumuiya hii ni ya kizezeta na haijaweka kukuza MAENDELEO ya mwananchi wa kawaida wa nchi wanachama.
Huu na mipango mingi ya VIONGOZI wa kiafrika ndio kiini cha mabalaa na majanga katika baraka letu, UFISADI, uchu wa madaraka, ubinafsi na RUSHWA ndio Misingi ya kuanzishwa kwa jumuiya ya Afrika mashariki na watanzania wamelipotezea hilo litaasisi la kikabila kabla halijakomaa.
KUSHIRIKIANA SIO MPAKA MUUNGANE , KUJUANA MWISHO MIPAKANI, KILA MMOJA A BAKI KWAO
Wewe utakuwa unaishi koromije sio burehakuna mtz anaekubali mchina auze karanga tz
NI kweli tupu neno la wahenga, tushirikiane pale inapibidi lakini kuungana HAPANA,tulijaribu awali tukaishia njiani hakuna sababu ya Kurudisha tena NO.La, mie naona Wahenga walikuwa sawa: "Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu"
NI kweli tupu neno la wahenga, tushirikiane pale inapibidi lakini kuungana HAPANA,tulijaribu awali tukaishia njiani hakuna sababu ya Kurudisha tena NO.
Kwa tabia za akina Museveni et-al kutaka kuwa marais wa milele.
Heri nusu shari kuliko shari kamili, wahenga walinena , ukishaumwa na NYOKA basi hata unyasi utaogopa, hivyo watanzania tulishagongwa na NYOKA kwenye jumuiya iliyokufa sasa msitulaumu kwa kuwa na tahadhari, NI RAHISI SANA KWA MLAKUNDE(KENYA NA UGANDA) KUSAHAU ILA SISI WATUPA MAGANDA (TANZANIA) HATUWEZI SAHAU TULIVYOSALITIWA.Sentebe, umeoa wewe? Kama ume, utajua "mavi ya kale hayanuki" na...."yaliyopita si ndwele (ugonjwa) tugange yajayo."
Halafu, mara nyingi watu wenye mawazo kama yako huwa hawaja interact na Mkenya kama mtu binfsi au hata pengine kumwona. Ni mawazo ya kujumuisha (generalization) yanayochochewa na wivu na chuki za kisiasa na...to be frank, a sense of inferiority tuliyonayo Watanzania!
Zaidi, hii siyo thread juu ya Ukenya na Utanzania. Soma kichwa cha habari.
Maandishi mengi umejaza pumba tupu. Eti kuongea kiingereza unaijua EAC wewe au unabwabwaja tu. Nenda kaulizie EAC human capital ya jumuiya inategemea watu wa kutoka wapi! !!.Mnaongea vitu msivyofanyia utafiti. Pale EAC think tankers zinatoka Tanzania. Kwa kuhakikisha NENDA EAC kafanye utafiti siyo kubwabwaja tuuu . EAC ni Tanzania bila Tanzania hakuna EAC. Wanatuhitaji kuliko wao tunavyowahitaji tulia wanyooshweLa hasha! Siyo nchi zote zinahitajia Tanzania. Hivi ndivyo tunavyodanganywa. Kweli, huenda nchi kama Kenya inatuhitajia kama soko tu, lakini haina maana kama hatufungulii hawatapata masoko mengine. Kenya pengine inafanya business kubwa zaidi na South Sudan na Ethiopia kuliko Tanzania. Hivyo usidanganywe kuwa Tanzania ni muhimu mno kwa Kenya kiasi isipokuwepo Kenya itakufa. Haya ni mawazo ya watu wasio safiri na wanaolishwa daily dish of propaganda.
Pili, wasema hakuna faida kwa nchi ambazo hazikuweka vikwazo? Nenda Rwanda leo. Kitu cha kwanza utakachokishuhudia ni maendeleo makubwa ya kupatikana kwa bidhaa. Hilo limefanya bei zake zishuke. Ukiwa Rwada unaweza kupiga simu Kenya, Uganda kwa tarrif ile ile kama ambavyo ungekuwa Kenya. Hebu jaribu kupiga simu Tanzania kwenda Kenya uone gharama zake. Lakini faida kubwa ni ugurishaji wa ujuzi unakuja kwa kuingiliana na watu wenye experience mbali mbali.
Kwa vile Rwada imekubali "movement of people" watu wengi "wenye akili" kutoka Kenya, Uganda etc wanafanya kazi Rwanda, na hivyo kuongeza ufanisi wa nchi hiyo. Leo hii Wanyarwanda wanazungumza Kiingereza, Kiswahili na Kinyarwanda pengine more proficient kuliko sisi. Jambo hili si suala la lugha pekee. Hii inamaanisha mwekezaji atachagua Rwanda kuliko Tanzania kutokana na "human development" iliyoko Rwanda.
Umezungumzia rasilmali. Kuna "kutoelewa" kwa watu katika suala hili la rasilimali. Kuwa na "rasilimali" hakumaanishi nchi kuwa tajiri. Rasilimali yabakia kuwa rasilimali tu hadi utakapoweza kuigeuza kuwa 'mali". Ndiyo maana DRC ina rasilimali kuliko Tanzania au nchi yeyote Afrika. Jee, DRC ni tajiri kuliko Egypt ambayo ni jangwa tu? Ili kuifanya rasilimali kuwa "mali" unahitajia "critical mass" ya watu wenye "practical knowledge". Ili kupata idadi hiyo kubwa ya watu wa "caliber" hiyo, Tanzania itahitajia miaka 100-200 ijayo (tena pamoja na juhudi kubwa za kusudi). Njia fupi ni kuwaruhusu watu kama hawa waliofundishwa kwingine kuja na kuchangia maendeleo ya nchi. Hii ndiyo faida kuu kwa kweli itakayopatikana kutokana na muungano wa EAC. Nchi zote kuu duniani zilizoendelea, labda ukitoa China (na hii ni stori nyingine na ndefu), zimefanya hivi. Soma asili ya maendeleo ya Marekani na nchi za Magharibi, nani walichangia....utaona kulikuwa na "infusion" kubwa wakati fulani ya watu waliotoka kwingine.
Mi nadhani watu wengi humu wanaojadili masuala haya, hawajadili kwa "usomi" bali kwa hisia, jazba na matamshi ya viongozi! Changanya na akili zako. Na zaidi, fanya utafiti. Siku hizi kuna kitu kinaitwa Google!
unaandika ujinga..unasifia uchumi unaopendelea wasomi wachache na watu wenye mtaji kwenye jamii ambayo sehemu kubwa hawakwenda shule!?Sipendi kuugeuza uzi huu kuwa ni wa kuzungumzia Kenya na Tanzania. Hayo siyo makusudio. Lakini kwa kutaka kukufahamisha tu na kuondoa ufahamu makosa wa Watanzania wengoi juu ya Kenya:
Uliwahi kufika Kenya wewe? Usingeuliza hilo. Watu wanaopata taabu Kenya ni wale ambao wana "deficit" ya elimu. Kwa sababu uchumi wa Kenya umepiga hatua kubwa, naturally, unahitaji watu walioelimika kuweza kupata manufaa. Hi ni kawaida kabisa. Kuna Watanzania chungu nzima wame-invest Kenya, katika stock exchange yao treasury bills au hata hisa za kawaida. Sasa kipi cha kuchukia? Angalia: ubepari (capitalism) kama system ya utawala, haiwezi kumchukia yeyote mwenye "capital" aidha ya akili au ya pesa. Ni system za kuchelewa-chelewa na kuangalia nyuma (atavistic ) ndio zina wivu kama huo!
Maandishi mengi umejaza pumba tupu. Eti kuongea kiingereza unaijua EAC wewe au unabwabwaja tu. Nenda kaulizie EAC human capital ya jumuiya inategemea watu wa kutoka wapi! !!.Mnaongea vitu msivyofanyia utafiti. Pale EAC think tankers zinatoka Tanzania. Kwa kuhakikisha NENDA EAC kafanye utafiti siyo kubwabwaja tuuu . EAC ni Tanzania bila Tanzania hakuna EAC. Wanatuhitaji kuliko wao tunavyowahitaji tulia wanyooshwe
Ungemjibu swali lake na wewe ugejulikana kuwa unaishi mjini.Alama kuu ya mtu anayeishi kijijini ni matamshi haya!
lete statistics za watu wenye elimu na huo mtaji..tuone ni kiasi gani inafaaStatistics or you are writing rubbish.
Nimekuwa nikifuatia kwa karibu sana tabia ya Tanzania ya kukwamisha maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kuanzia kuzuia uhuru wa kugura (movement) kwa raia wa Jumuiya, hadi kulipisha ushuru bidhaa za nchi hizo; ingawaje yote mawili hayo yalizungumzwa na kuafikiwa kwa ndiyo na hapana.
Kwa kweli uhuru wa movement (kugura) kwa raia wa nchi za EAC ndiyo msingi mkubwa wa Jumuiya hii kufikia muungano kamili.
Nini hasa kinachoendelea kwa nchi hii ambayo mwanzishi wake alisifika kupigania Umoja wa Afrika, na alidiriki kutaka kuchelewesha uhuru wa Tanzania ili mradi nchi zote tatu ziungane?
Watawala wetu (nawaita watawala na wala siyo viongozi) wanawarubuni Watanzania eti kukataa mambo fulani ni kwa sababu ya kuchunga maslahi ya Watanzania. La hasha! Ukweli ni kuwa wanasiasa wetu wanaogopa kwamba endapo Jumuiya hii itasimama kama inavyopendekezwa, basi wataumbuka.
Kwa maana ule uwongo wanaowalisha Watanzania kila siku kwamba sisi tuko "huru sana" na tuna "amani na demokrasia sana", "hatuna ukabila" "tumeendelea kuliko..." nk utaonekana wazi ni mangati (mirage). Pindi Watanzania watakapoingiliana na kuwajua kikweli Wakenya, au Banyarwanda au hata Waganda wataona dhahiri kuwa wenzetu hawa wameendelea mno kifikra na kisiasa kuliko sisi.
Kutokana na elimu yao kubwa, hawatishwitishwi kama Watanzania. Hilo huenda likawageuza Watanzania na kuona wazi ukiukaji mkubwa wa haki zao za kibinadamu unaofanywa na Watawala na vyombo vyao...polisi na wakuu wa kisiasa, na huenda wakataka uhuru kama walionao wenzao.
Kwa mfano, wakati Tanzania mtu mmoja tu (rais) anaweza kuzuia matangazo mubashara ya Bunge, jambo kama hilo haliwezekani Kenya au Uganda. Kwa maana nyingine, taasisi (institutions) za Kenya, Uganda na hata Rwanda zimeendelea zaidi kuliko za Tanzania.
HII HASA NDIYO SABABU WAJANJA HAWA WANAKWAMISHA MUUNGANO KAMILI WA EAC.
Na ndiyo maana watawala hawa hupendelea zaidi SADCC, kwa vile shirikisho hili ni butu, halina ndani yake mechanism ya kuweza kuwabadilisha Watanzania kifikra.
Wewe ni mTanzania?Nimekuwa nikifuatia kwa karibu sana tabia ya Tanzania ya kukwamisha maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kuanzia kuzuia uhuru wa kugura (movement) kwa raia wa Jumuiya, hadi kulipisha ushuru bidhaa za nchi hizo; ingawaje yote mawili hayo yalizungumzwa na kuafikiwa kwa ndiyo na hapana.
Kwa kweli uhuru wa movement (kugura) kwa raia wa nchi za EAC ndiyo msingi mkubwa wa Jumuiya hii kufikia muungano kamili.
Nini hasa kinachoendelea kwa nchi hii ambayo mwanzishi wake alisifika kupigania Umoja wa Afrika, na alidiriki kutaka kuchelewesha uhuru wa Tanzania ili mradi nchi zote tatu ziungane?
Watawala wetu (nawaita watawala na wala siyo viongozi) wanawarubuni Watanzania eti kukataa mambo fulani ni kwa sababu ya kuchunga maslahi ya Watanzania. La hasha! Ukweli ni kuwa wanasiasa wetu wanaogopa kwamba endapo Jumuiya hii itasimama kama inavyopendekezwa, basi wataumbuka.
Kwa maana ule uwongo wanaowalisha Watanzania kila siku kwamba sisi tuko "huru sana" na tuna "amani na demokrasia sana", "hatuna ukabila" "tumeendelea kuliko..." nk utaonekana wazi ni mangati (mirage). Pindi Watanzania watakapoingiliana na kuwajua kikweli Wakenya, au Banyarwanda au hata Waganda wataona dhahiri kuwa wenzetu hawa wameendelea mno kifikra na kisiasa kuliko sisi.
Kutokana na elimu yao kubwa, hawatishwitishwi kama Watanzania. Hilo huenda likawageuza Watanzania na kuona wazi ukiukaji mkubwa wa haki zao za kibinadamu unaofanywa na Watawala na vyombo vyao...polisi na wakuu wa kisiasa, na huenda wakataka uhuru kama walionao wenzao.
Kwa mfano, wakati Tanzania mtu mmoja tu (rais) anaweza kuzuia matangazo mubashara ya Bunge, jambo kama hilo haliwezekani Kenya au Uganda. Kwa maana nyingine, taasisi (institutions) za Kenya, Uganda na hata Rwanda zimeendelea zaidi kuliko za Tanzania.
HII HASA NDIYO SABABU WAJANJA HAWA WANAKWAMISHA MUUNGANO KAMILI WA EAC.
Na ndiyo maana watawala hawa hupendelea zaidi SADCC, kwa vile shirikisho hili ni butu, halina ndani yake mechanism ya kuweza kuwabadilisha Watanzania kifikra.
Nilijua wewe ni boya, na wala siyo raia wa hapa.Ajabu sana process ya kufikiria kwako. Yaani kutojiunga ndiyo kutaifanya Tanzania iwe na viwanda? Miaka zaidi ya 60 ya Uhuru hamkujiunga popote kwa nini hamkuleta viwanda wakati huo?
Angalia bara Ulaya. Si wote wana/walikuwa na maendeleo sawa. Wakati Ureno na Spain zajiunga na EEC mwaka 1986 zilikuwa nchi mkia barani Ulaya. Angalia hii leo. Hivyo hivyo nchi mpya kujiunga kama Hungary, Bulgaria zote zinaelekea kuimarika zaidi. Yaani waona suluhisho la matatizo na kuzorota kwa Tanzania ni kujichimbia kwenye shimo? Twashindwa na Rwanda kijinchi kimeanza juzi juzi hapa, leo hii kina watu wanaojiamini, wasioogopaogopa mwingine kuliko jinchi jikubwa la Tanzania? Huu Ujamaa umewazubaisha sana Watanzania. Kila mtu ataka alelewe na kubembelezwa kuwa "usiogope huko nje nitakukinga" Hatutafika.
Bahati mbaya, viongozi wako pia wanafikiria kama wewe!