Sijali
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 2,700
- 1,853
- Thread starter
- #41
Well said, na ukiangalia Nchi zote wanachama wa EAC yenye neema ya Rasilimali asilia nyingi ni Tanzania wote wanangalia namna ya kutupiga tu, ukizingatia bado Hatuna Sheria na taratibu madhubuti ya kulinda rasilimali zetu ni bora tusiwe vimbele mbele, turekebishe na kuimarisha kwanza mifumo ya ndani. Muungano sio wakutegemea sana na kujiachia kijinga siku ukivunjika unaweza jikuta unaingiza taifa shimoni
La hasha! Siyo nchi zote zinahitajia Tanzania. Hivi ndivyo tunavyodanganywa. Kweli, huenda nchi kama Kenya inatuhitajia kama soko tu, lakini haina maana kama hatufungulii hawatapata masoko mengine. Kenya pengine inafanya business kubwa zaidi na South Sudan na Ethiopia kuliko Tanzania. Hivyo usidanganywe kuwa Tanzania ni muhimu mno kwa Kenya kiasi isipokuwepo Kenya itakufa. Haya ni mawazo ya watu wasio safiri na wanaolishwa daily dish of propaganda.
Pili, wasema hakuna faida kwa nchi ambazo hazikuweka vikwazo? Nenda Rwanda leo. Kitu cha kwanza utakachokishuhudia ni maendeleo makubwa ya kupatikana kwa bidhaa. Hilo limefanya bei zake zishuke. Ukiwa Rwada unaweza kupiga simu Kenya, Uganda kwa tarrif ile ile kama ambavyo ungekuwa Kenya. Hebu jaribu kupiga simu Tanzania kwenda Kenya uone gharama zake. Lakini faida kubwa ni ugurishaji wa ujuzi unakuja kwa kuingiliana na watu wenye experience mbali mbali.
Kwa vile Rwada imekubali "movement of people" watu wengi "wenye akili" kutoka Kenya, Uganda etc wanafanya kazi Rwanda, na hivyo kuongeza ufanisi wa nchi hiyo. Leo hii Wanyarwanda wanazungumza Kiingereza, Kiswahili na Kinyarwanda pengine more proficient kuliko sisi. Jambo hili si suala la lugha pekee. Hii inamaanisha mwekezaji atachagua Rwanda kuliko Tanzania kutokana na "human development" iliyoko Rwanda.
Umezungumzia rasilmali. Kuna "kutoelewa" kwa watu katika suala hili la rasilimali. Kuwa na "rasilimali" hakumaanishi nchi kuwa tajiri. Rasilimali yabakia kuwa rasilimali tu hadi utakapoweza kuigeuza kuwa 'mali". Ndiyo maana DRC ina rasilimali kuliko Tanzania au nchi yeyote Afrika. Jee, DRC ni tajiri kuliko Egypt ambayo ni jangwa tu? Ili kuifanya rasilimali kuwa "mali" unahitajia "critical mass" ya watu wenye "practical knowledge". Ili kupata idadi hiyo kubwa ya watu wa "caliber" hiyo, Tanzania itahitajia miaka 100-200 ijayo (tena pamoja na juhudi kubwa za kusudi). Njia fupi ni kuwaruhusu watu kama hawa waliofundishwa kwingine kuja na kuchangia maendeleo ya nchi. Hii ndiyo faida kuu kwa kweli itakayopatikana kutokana na muungano wa EAC. Nchi zote kuu duniani zilizoendelea, labda ukitoa China (na hii ni stori nyingine na ndefu), zimefanya hivi. Soma asili ya maendeleo ya Marekani na nchi za Magharibi, nani walichangia....utaona kulikuwa na "infusion" kubwa wakati fulani ya watu waliotoka kwingine.
Mi nadhani watu wengi humu wanaojadili masuala haya, hawajadili kwa "usomi" bali kwa hisia, jazba na matamshi ya viongozi! Changanya na akili zako. Na zaidi, fanya utafiti. Siku hizi kuna kitu kinaitwa Google!