Sijali
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 2,700
- 1,853
Nimekuwa nikifuatia kwa karibu sana tabia ya Tanzania ya kukwamisha maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kuanzia kuzuia uhuru wa kugura (movement) kwa raia wa Jumuiya, hadi kulipisha ushuru bidhaa za nchi hizo; ingawaje yote mawili hayo yalizungumzwa na kuafikiwa kwa ndiyo na hapana.
Kwa kweli uhuru wa movement (kugura) kwa raia wa nchi za EAC ndiyo msingi mkubwa wa Jumuiya hii kufikia muungano kamili.
Nini hasa kinachoendelea kwa nchi hii ambayo mwanzishi wake alisifika kupigania Umoja wa Afrika, na alidiriki kutaka kuchelewesha uhuru wa Tanzania ili mradi nchi zote tatu ziungane?
Watawala wetu (nawaita watawala na wala siyo viongozi) wanawarubuni Watanzania eti kukataa mambo fulani ni kwa sababu ya kuchunga maslahi ya Watanzania. La hasha! Ukweli ni kuwa wanasiasa wetu wanaogopa kwamba endapo Jumuiya hii itasimama kama inavyopendekezwa, basi wataumbuka.
Kwa maana ule uwongo wanaowalisha Watanzania kila siku kwamba sisi tuko "huru sana" na tuna "amani na demokrasia sana", "hatuna ukabila" "tumeendelea kuliko..." nk utaonekana wazi ni mangati (mirage). Pindi Watanzania watakapoingiliana na kuwajua kikweli Wakenya, au Banyarwanda au hata Waganda wataona dhahiri kuwa wenzetu hawa wameendelea mno kifikra na kisiasa kuliko sisi.
Kutokana na elimu yao kubwa, hawatishwitishwi kama Watanzania. Hilo huenda likawageuza Watanzania na kuona wazi ukiukaji mkubwa wa haki zao za kibinadamu unaofanywa na Watawala na vyombo vyao...polisi na wakuu wa kisiasa, na huenda wakataka uhuru kama walionao wenzao.
Kwa mfano, wakati Tanzania mtu mmoja tu (rais) anaweza kuzuia matangazo mubashara ya Bunge, jambo kama hilo haliwezekani Kenya au Uganda. Kwa maana nyingine, taasisi (institutions) za Kenya, Uganda na hata Rwanda zimeendelea zaidi kuliko za Tanzania.
HII HASA NDIYO SABABU WAJANJA HAWA WANAKWAMISHA MUUNGANO KAMILI WA EAC.
Na ndiyo maana watawala hawa hupendelea zaidi SADCC, kwa vile shirikisho hili ni butu, halina ndani yake mechanism ya kuweza kuwabadilisha Watanzania kifikra.
Kwa kweli uhuru wa movement (kugura) kwa raia wa nchi za EAC ndiyo msingi mkubwa wa Jumuiya hii kufikia muungano kamili.
Nini hasa kinachoendelea kwa nchi hii ambayo mwanzishi wake alisifika kupigania Umoja wa Afrika, na alidiriki kutaka kuchelewesha uhuru wa Tanzania ili mradi nchi zote tatu ziungane?
Watawala wetu (nawaita watawala na wala siyo viongozi) wanawarubuni Watanzania eti kukataa mambo fulani ni kwa sababu ya kuchunga maslahi ya Watanzania. La hasha! Ukweli ni kuwa wanasiasa wetu wanaogopa kwamba endapo Jumuiya hii itasimama kama inavyopendekezwa, basi wataumbuka.
Kwa maana ule uwongo wanaowalisha Watanzania kila siku kwamba sisi tuko "huru sana" na tuna "amani na demokrasia sana", "hatuna ukabila" "tumeendelea kuliko..." nk utaonekana wazi ni mangati (mirage). Pindi Watanzania watakapoingiliana na kuwajua kikweli Wakenya, au Banyarwanda au hata Waganda wataona dhahiri kuwa wenzetu hawa wameendelea mno kifikra na kisiasa kuliko sisi.
Kutokana na elimu yao kubwa, hawatishwitishwi kama Watanzania. Hilo huenda likawageuza Watanzania na kuona wazi ukiukaji mkubwa wa haki zao za kibinadamu unaofanywa na Watawala na vyombo vyao...polisi na wakuu wa kisiasa, na huenda wakataka uhuru kama walionao wenzao.
Kwa mfano, wakati Tanzania mtu mmoja tu (rais) anaweza kuzuia matangazo mubashara ya Bunge, jambo kama hilo haliwezekani Kenya au Uganda. Kwa maana nyingine, taasisi (institutions) za Kenya, Uganda na hata Rwanda zimeendelea zaidi kuliko za Tanzania.
HII HASA NDIYO SABABU WAJANJA HAWA WANAKWAMISHA MUUNGANO KAMILI WA EAC.
Na ndiyo maana watawala hawa hupendelea zaidi SADCC, kwa vile shirikisho hili ni butu, halina ndani yake mechanism ya kuweza kuwabadilisha Watanzania kifikra.