Kwanini TANESCO walidanganya wananchi?

Kwanini TANESCO walidanganya wananchi?

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,533
Reaction score
3,838
Siku chache baada ya Raisi Magufuli kutangaza kubomolewa kwa jengo la Tanesco kuna sms ilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa watu wajiandae, wanunue umeme mapema maana siku yoyote yawezekana LUKU inaweza kuwa shida kununua.

Tanesco walijitokeza hadharani kupinga hicho kitu, lakini jana jioni wakasambaza taarifa kuwa mfumo wa LUKU utakuwa haufanyi kazi kuanzia saa mbili usiku mpaka saa nne. Huu ni uongo, jana kuanzia asubuhi ulikuwa huwezi kununua umeme mpaka muda huu asubuhi naandika hapa huwezi kununua umeme.

1. Tanesco wangesema ukweli, watu wangenunua umeme mapema. Kuna watu wana mashine za kusaga hazifanyi kazi toka jana, sisi wafugaji hatuna pumba. Vipi wenye bucha, wachomeleaji, viwanda nk ambao waliishiwa umeme jana? Tanesco mna akili kweli?

2. Jana umesema watu hawataweza kununua umeme kuanzia saa mbili usiku wakati kiuhalisia watu hawawezi kununua umeme toka jana asubuhi. Kwanini hili taifa limekuwa la uongo uongo? kwanini hatupendi ukweli
 
Mkuu tena wamekusogezea huduma karibu, ngoja tusikie majibu yao
tanesco.png

cc @TANESCO mje huku kutoa majibu
 
Mwanangu huwa anasema hivi mama tanesco wanakata umeme wako
 
Morning sweetheart.

Leo ndio mara ya kwanza kuona post yako tangu Babu seya aachiwe huru [emoji2] [emoji2]
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] yawezekana nimeachiwa huru na mimi

Mbona nimo tangu juzi baby

Umemuona padri anavyohangaika na wengine kubebishwa hahahahahah pole yake
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] yawezekana nimeachiwa huru na mimi

Mbona nimo tangu juzi baby

Umemuona padri anavyohangaika na wengine kubebishwa hahahahahah pole yake
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
No comment
 
Hivi kauli hizi, za kulaumu na kulalamika, hamjachoka nazo? Hazina tija kwenu zaidi ya kuonyesha kuwa kiwango chenu cha kufikiri kimefikia mwisho!
Kama kiwango chenu cha kufikiri hakijafikia mwisho kwa nini mnashindwa kutatua hayo matatizo badala yake yanaongezeka?
 
Mkuu kwenye Ilani ya awamu hii kuna chapter inasema "Uongo unaweza kutumika ili kuonyesha ufanisi ya -utawala- wetu! Danganya kadri uwezavyo maadamu tu tuendelee kuitafuna nchi, mwenye uchungu sana na nchi ahamie chamani na yeye ajimegee"
 
Kama kiwango chenu cha kufikiri hakijafikia mwisho kwa nini manshindwa kutatua hayo matatizo badala yake yanaongezeka?

Hilo la wewe kuendelea kunung'unika, kulalama na kulaumu ni ushahidi tosha kuwa na wewe unashindwa kutatua tatizo lako hilo. Kwa kiasi kikubwa sasa unadhihirisha hicho ndicho kiwango chako cha juu cha kufikiri!

Kama duniani changamoto zingekwisha, basi maendeleo yangesimama, au sivyo mkuu Mwifwa?

Lialia ni dalili za unyonge au kukata tamaa, mwanaume.

ALWAYS THINK POSITIVELY AND FACE CHALLENGES AS OPPORTUNITIES.
 
Back
Top Bottom