Kwanini sitaki kujua kipato cha mke wangu?

Kwanini sitaki kujua kipato cha mke wangu?

Tarime one

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
2,246
Reaction score
1,740
Wanajanvi,

Leo nilikua najadiliana na best yangu mmoja akinitaka ushauri kuhusu mke wake kuwa msiri kwenye kipato chake cha ofisini na ndoa yake bado ina mwaka mmoja, akaniuliza mie nahandle vp hili swala.

Jibu nililompa amebaki akiniangalia haamini nilichomwambia ni kweli ndani ya miaka 12 ya ndoa yangu sijui mke wangu analipwa sh ngapi na sitaki kujua asilani, akaniuliza why na wewe ndio uligharimia elimu yake?

Nikamjibu kumsomesha sio tiketi ya kujua kipato chake bali ilikua kumwandaa pale nitakapopata tatizo aweze kusimamia familia pia nikamwambia unapooa tu lazima umsome mkeo tabia yake kwa ujumla ili uishi nae kwa amani.

Ndoa nyingi zinaingia kwenye migogoro kuhusiana na vipato vyao,la kufanya kama mwanaume ni kutambua jukumu lako kama kichwa cha nyumba na kusimamia jukumu lako kwa ukamilifu.

Nikamwambia mimi nilitambua tabia ya mke wangu mapema nikajipanga kuishi nae kwa akili, mshahara wake siujui but kuna vitu nimempangia vya kusimamia ndani ya nyumba.

Na bado huwa nawajibika pale ninapoona upungufu na tunaishi kwa amani, ukitaka kuishi na mwanamke mfanyakazi mpe uhuru wa kutumia kipato chake bila kuingiliwa utaona utamu wa ndoa.
 
Tarime one

Sorry, umesema ulimsomesha ili kwamba utakapopata matatizo aweze kusimamia familia. Hiyo familia anasimamia na vidole?

Hata kama ni elimu u adhani itakuwa ni elimu tu? Unajua ni wangapi wamepata matatizo na wake zao wana elimu nzuri tu, lakini bila fedha wameyumba vibaya?

Unachamganya vitu viwili hapa kuna kujua kipato chake na kutegemea kipato chake!
 
Last edited by a moderator:
Kuna tofauti kati yakujua kipato cha mkeo na kutegemea kipato cha mkeo...kuna leo na kesho,ikitokea amepata matatizo au amefariki je unaweza kuwa na uhakika wa kile utachopewa kama stahiki zake??

Unaweza ukajua analipwa kiasi gani ila usitegemee kipato chake ndio kiendeshe familia,swala la msingi nafikiri nikumpa tu majukumu madogo madogo ya ndani ili ajione na yeye ni mmoja ya wanaochangia maendeleo ya familia yenu,na huo ndio uhuru wa kweli...hivi viumbe tumeaagizwa tuvitawale nakuviongoza tena kwa akili,sasa unaposema umuache afanye anavyotaka maana yake wajibu wako kama mume wakumuongoza umekabidhi ulimwengu uyafanye...

Kumbuka "uhuru bila mipaka ni mateso"

Mwisho nafikiri chakumuambia huyo jamaa ni kuwa amkabidhi tu majukumu madogo mke hapo nyumbani ayafanye atapata majibu tu ya kiwango gani analipwa lakini isiwe ndio gear yakumuachia majukumu mke wake...
 
Sorry, umesema ulimsomesha ili lwamva utakapopata matatizo aweze kusimamia familia. Hiyo familia anasimamia na vidole?

Hata kama ni elimu u adhani itakuwa ni elimu tu? Unajua ni wangapi wamepata matatizo na wake zao wana elimu nzuri tu, lakini bila fedha wameyumba vibaya?

Unachamganya vitu viwili hapa kuna kujua kipato chake na kutegemea kipato chake!

Huyu jamaa hajui kipato cha mke wake lakini anakitegemea kisimamie baadhi ya mambo nyumbani,huyu bwana sijui kama anajua alichokiandika, sasa alimpangiaje vitu vya kusimamia bila kujua analipwa kiasi gani.

Naungana na mchangiaji wa kwanza kwamba kutokujua kipato cha mkeo sio ujanja.
 
Uko mbali kiasi gani na mkeo mpaka usijue kipato chake.?
Hatari.
 
Sorry, umesema ulimsomesha ili lwamva utakapopata matatizo aweze kusimamia familia. Hiyo familia anasimamia na vidole?

Hata kama ni elimu u adhani itakuwa ni elimu tu? Unajua ni wangapi wamepata matatizo na wake zao wana elimu nzuri tu, lakini bila fedha wameyumba vibaya?

Unachamganya vitu viwili hapa kuna kujua kipato chake na kutegemea kipato chake!

Mkuu,haya mambo ya ndoa yanatushinda kwa kutokujua mambo madogo,yawezekana kuna watu wakaniona mpuuzi au mjinga but kuna kitu nilikiona toka kwa wife na msukumo toka kwa ndugu zake,na kipindi hicho nilikua sijafanikisha malengo yangu na kupitia tabia hiyo niliyokutana nayo nashukuru ilinifanya nijitambue na nikasema kabisa sitakuja kutaka kujua kipato chake au kuulizia,na nashukuru nimeweza na baada ya kuona simfatilii na mambo yanakwenda poa amekua mpole na kuchukua position yake kama mke.
 
Hivii hii mifumo dume itaisha lini? Mi naona Kama mume kufuhamu kipato cha mkewe inapendeza kwani inakufanya ujue mahitaj ya nyumba na kwakiasi gani mnaweza kufanya vitu vya maendeleo kwa urahis zaidi

Ila kila nyumba/ndoa inamipaka yake ila ni bora kuwa kitu kimoja na kunafaida mno kwa mume kujua kipato cha mkewee.
 
Afadhali usikijue tu, kama anatimiza majukumu yake vyema yanini uanze kutaka salary slip kwani wewe bank kwamba anaomba mkopo. mwache mdada awe huru na chake kama anasimamia vema majukumu ya nyumbani.

Kuna wanaume povu linawatoka loh!! sijui ndio wale wa ikifika mwisho wa mwezi tunaulizana "mshahara wako ushaingia???"" loh!!!!!!!!!
 
Afadhali usikijue tu, kama anatimiza majukumu yake vyema yanini uanze kutaka salary slip kwani wewe bank kwamba anaomba mkopo. mwache mdada awe huru na chake kama anasimamia vema majukumu ya nyumbani.

Kuna wanaume povu linawatoka loh!! sijui ndio wale wa ikifika mwisho wa mwezi tunaulizana "mshahara wako ushaingia???"" loh!!!!!!!!!

Aaaah hapo naunganisha dots sasa na yale mambo ya siku ileeeee!!!!
 
Mke mwema wala huhitaji kuuliza kipato chake, atasema tu mwenyewe. Na shida sio kuuliza, bali kutegemea kipato chake. Hao magumegume yanayoficha vipato vyao wala huna haja ya kuwauliza vipato vyao coz tayari wanaonyesha umimi ndani ya nyumba.
 
Mke mwema wala huhitaji kuuliza kipato chake, atasema tu mwenyewe. Na shida sio kuuliza, bali kutegemea kipato chake. Hao magumegume yanayoficha vipato vyao wala huna haja ya kuwauliza vipato vyao coz tayari wanaonyesha umimi ndani ya nyumba.

Tatizo mkuu kuna watu wanafikiri ndoa zinafanana au labda kuna formula ya ndoa,kila mtu anautaratibu wake wa kudumisha ndoa.
 
Kuna tofauti kati yakujua kipato cha mkeo na kutegemea kipato cha mkeo...kuna leo na kesho,ikitokea amepata matatizo au amefariki je unaweza kuwa na uhakika wa kile utachopewa kama stahiki zake??

Unaweza ukajua analipwa kiasi gani ila usitegemee kipato chake ndio kiendeshe familia,swala la msingi nafikiri nikumpa tu majukumu madogo madogo ya ndani ili ajione na yeye ni mmoja ya wanaochangia maendeleo ya familia yenu,na huo ndio uhuru wa kweli...hivi viumbe tumeaagizwa tuvitawale nakuviongoza tena kwa akili,sasa unaposema umuache afanye anavyotaka maana yake wajibu wako kama mume wakumuongoza umekabidhi ulimwengu uyafanye...

Kumbuka "uhuru bila mipaka ni mateso"

Mwisho nafikiri chakumuambia huyo jamaa ni kuwa amkabidhi tu majukumu madogo mke hapo nyumbani ayafanye atapata majibu tu ya kiwango gani analipwa lakini isiwe ndio gear yakumuachia majukumu mke wake...

Maswali ya msingi
 
Misingi ya ndoa ilizama baharini tangu enzi za Nuhu, kilichobaki ni maigizo ya ndoa.... Hatujui maana ya mke wala mme, je maana ya ndoa tutaijuaaaaaaaaaaaaa?????????????
 
Inashangaza sana, hivi kweli natoka nyumbani kwangu giza narudi giza in the name of looking for money inakuwaje wale ninaowapenda kuliko chochote wasijue ninapata nini huko ninakotumia muda wangu na wao mwingi hivi. Je kama anaweza kunisaidia nikapata mahali bora kuliko hapa nilipo sasa. Ninachopata ni kwa ajili yao hao wengine ni ziada tu.

Na hata kama akiniachia majukumu nitafanya pale ninapoweza lakini isiwe kwa makusudi.

Mke mwema wala huhitaji kuuliza kipato chake, atasema tu mwenyewe. Na shida sio kuuliza, bali kutegemea kipato chake. Hao magumegume yanayoficha vipato vyao wala huna haja ya kuwauliza vipato vyao coz tayari wanaonyesha umimi ndani ya nyumba.
 
Back
Top Bottom