Mzee
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 13,620
- 5,863
Habari za hapa Jukwaani.
Serikali ya Halmashauri Manispaa ya Kahama wanaendesha zoezi la kukagua bidhaa zilizoExpire pamoja na bidhaa ambazo haziruhusiwi kuuzwa. Ni jambo jema sana.
Ijumaa walipita dukani, wakakuta soda 6 za aina tofauti katika freezer pamoja na Blue band kopo 1 zikiwa zimeexpire, kila moja wakanipiga faini ya laki 1, Jumla ya faini Laki 7 i.e 700,000/=.
#1 Ni jambo jema sana kuzungukia na kuona mazingira tunayofanya kazi, lakini wanapokuta kosa wanapiga faini za kuumiza ili kuruhusu Mazingira ya Rushwa?
Je, Serikali yetu ni katili namna hii?
#2 Nilijarbu kurepoti tukio langu siku hiyo hoyo kupitia Portal ya Serikali ya kutoa malalamiko lakini hakuna majibu mpaka leo, na wanaendelea kupiga faini za kuumiza ili kujenga Mazingira ya Rushwa.
#3 Hakuna mtu anataka kuuza bidhaa iliyoexpire maana hata sisi hatupendi kununua bidhaa zilizoexpire. Mnapokuta makosa jaribu kupiga faini ambazo zitatoa elimu lakini sio kumaliza Biashara. Unapiga faini ya laki 7, unataka nifunge Biashara?
NB: Endeleni kuja na kiburi chenu, kuna siku tutawavizia. Haiwezekani mtuonee namna hii.
Nawasilisha.
Serikali ya Halmashauri Manispaa ya Kahama wanaendesha zoezi la kukagua bidhaa zilizoExpire pamoja na bidhaa ambazo haziruhusiwi kuuzwa. Ni jambo jema sana.
Ijumaa walipita dukani, wakakuta soda 6 za aina tofauti katika freezer pamoja na Blue band kopo 1 zikiwa zimeexpire, kila moja wakanipiga faini ya laki 1, Jumla ya faini Laki 7 i.e 700,000/=.
#1 Ni jambo jema sana kuzungukia na kuona mazingira tunayofanya kazi, lakini wanapokuta kosa wanapiga faini za kuumiza ili kuruhusu Mazingira ya Rushwa?
Je, Serikali yetu ni katili namna hii?
#2 Nilijarbu kurepoti tukio langu siku hiyo hoyo kupitia Portal ya Serikali ya kutoa malalamiko lakini hakuna majibu mpaka leo, na wanaendelea kupiga faini za kuumiza ili kujenga Mazingira ya Rushwa.
#3 Hakuna mtu anataka kuuza bidhaa iliyoexpire maana hata sisi hatupendi kununua bidhaa zilizoexpire. Mnapokuta makosa jaribu kupiga faini ambazo zitatoa elimu lakini sio kumaliza Biashara. Unapiga faini ya laki 7, unataka nifunge Biashara?
NB: Endeleni kuja na kiburi chenu, kuna siku tutawavizia. Haiwezekani mtuonee namna hii.
Nawasilisha.