Kwanini Rais wa JMT hafanyiwi 'Interview' kwenye Media?

Kwanini Rais wa JMT hafanyiwi 'Interview' kwenye Media?

Kwa kuwa ni mbongo anawajua wabongo vizuri wafukunyuku sana hawako straight kama hao wa CNN NA BBC
Mbongo mpe nafasi akuhoji maswali ndo utamjua.......
Unajua kuna mambo/matukio mengi sana yanatokea nchini ambayo naamini anatakiwa mwandishi wa habari mwenye kujua kazi yake na mkongwe afanye mahojiano ya ana kwa ana na raisi ili aweze kuyatolea ufafanuzi.

Cha ajabu watakuja kumuhoji siku chache kabla ya kustaafu au hata baada ya kustaafu.
 
Raisi Kikwete akitoka nje ya nchi anaweza kufanya mahojiano(interview) na waandishi au vyombo vya habari vya kimataifa kama CNN n.k.

Lakini najiuliza ni lini Raisi Kikwete amewahi kuhojiwa TBC1,ITV,Star tv,Channel 10 n.k?

Au ni lini Raisi Kikwete amewahi kufanya mahojiano na waandishi mashuhuri wa nchi tangu aingie madarakani?

Au tatizo ni waandishi wenyewe kukosa ujasiri au kutokujiamini kufanya mahojiano na raisi?

Kama aliwahi,basi ni wakati anaingia madarakani.

Tutofautishe kuitisha "press conference" na kufanya mahojiano ya "ana kwa ana" na chombo cha habari au na mwandishi maarufu wa habari.

Charity begins at home.

Alifanya mahojiano na shaban kisu baada ya hapo akampatia udc
 
Tatizo viongozi wa Tz hupenda tu kujiita watanzania lakini si wazalendo na kujiskia fahari kama watanzania wanadharau sana kwao na kujihs wapo dunia nyengine.

Kwanza waandishi wa Tz wanadharauliwa sana ni viongoz wa Tz kumbukeni alipokuja Obama ni viongozi wa Tz waliowambia waandish wa hapa eti wavae vizuri wanyooshe pasi nguo zao na baadhi ya waandish weng wa hapa hawakupata nafas kumuuliza Obama na wengine ata kuruhusiwa kuingia katika ukumbi alokuwemo Obama.

Lakini utashangaa JK akienda marekani anaulizwa na wale diaspora maswali ata hayana macho lakini kwasabab yupu United States basi anapata fursa kuulizwa chochote tu kile.

Leo hii pesa ya Tanzania imeshuka tena 20% zaid kwa fedha ya marekani lakini ukimuuliza Rais swali hili au pale bungeni bas jibu litakalotoka ni matusi tu na kebehi lakin akiulizwa nje ya Tz atakuwa serious.
 
Angepangiwa masako ningefurahi..wengine hawana cha kumuuliza zaidi ya kupangiwa cha kuuliza na kubaki kusikiliza hadi amalize kusema anachopenda.Bila kuchomekea viswali fulanifulani vitakavyomsukuma kujibu hoja na malalamiko ya msingi ktk nchi.
 
Mahojiano na waandishi wa bongo wakati wanamjua nje ndani, nani wa hivyo?
 
Mahojiano na kikwete tena na mwandishi wa habari mkongwe? Wewe mtoto wa vidudu tu ukinwambia amulize maswali atakuwa hana majibu itakuwa ya mwandishi mkongwe jamani jamani mwacheni baba ritz mwenyewe anatamani dunia ingekuwa inafoward batten abonyeze october ifike asepe mana mambo yamekuwa magumu.
 
Bado linasumbua naenda Marekani tena nikamuone yule mtaalamu. Sikujua kama haya matezi dume yanasumbua kiasi hiki.

Hali ni mbaya nchi imesha mshinda.... Je unadhani Ana jibu LA swali gani zaidi 'UNAENDELEAJE NA TEZI DUME?'
 
Mfano: swali: kwanini thamani ya shilingi ina shuka?Jibu:hata mi na shangaa!!uchumi unakua kwa kasi
 
Jibu ni kwamba JK anapoongea na hao waandishi wa huko nje anajua anaweza kuwapiga 'fix' bila hao waandishi, kubaini changa hilo la macho.

Mfano mmoja ni wakati ule alipoenda Ethiopia kwenye kikao cha AU.

Alipoulizwa ni kwa nini gazeti la ----------- limefungiwa kwa muda usiojulikana, akajibu kuwa gazeti hilo limefungiwa kutokana na kuandika habari za uchochezi za 'kuwashawishi' wanajeshi wafanye uasi na akaapa kuwa hatalifungulia kamwe!

Alitumia 'kucheat' huko kwa waandishi wa nje kwa kuwa alijua waandishi hao hawajui 'undani' wa kufungiwa gazeti hilo la -----------.

Hivi unadhani JK angeweza kufanya 'usanii' wa aina hiyo kwa waandishi wa hapa nchini, wakati anajua kuwa waandishi hao wanajua 'siri' ya kufungiwa gazeti hilo?
 
Wakati wa Mkapa waandishi waliuliza maswali mpaka yakaisha, wakati kwa wenzetu Rais mpaka koo linamkauka kwa maswali mafupi, mazuri yenye mantiki. Waandishi watueleze lini walitaka mahojiano nae wakakataliwa na lkulu. Huenda ni udhaifu wao na kukosa ujasiri, hata kwenye michezo kocha asie jua Kiswahili haulizwi maswali, nadhani kuna shida ni muda muafaka wa kuwajengea uwezo
 
ni mzito sana kupambanua hoja,pia ni mkorofi na ana jazba sana,kwa hiyo ukimuuliza swali gumu anaweza kukupiga -kumbuka ni mwanajeshi yule,na hivi wabongo huwa mnaulizaga maswali ya kuudhi!! so he can't do that!
 
Habari ndugu zangu,

Kuna swali limekuwa likinitatiza kwa kipindi kirefu sasa. Mwanzoni nilidhani labda 'itifaki' haziruhusu kwa kiongozi wa juu wa nchi (Rais), kufanyiwa mahojiano na vyombo vya habari nchini, mfano Televisheni / Radio / Magazeti.. Lakini hili nimepingana nalo baada ya kuona akialikwa mara kwa mara nchi za ugenini na kuhojiwa kuhusu masuala mbalimbali na Media za huko.

Kwa mfano, Nishawahi kumsikia Mheshimiwa Rais akihojiwa mara kwa mara na vyombo vikubwa vya habari kama vile BBC, Deutsche Welle, na vinginevyo.. Lakini kwa vyombo vya habari vya hapa nyumbani si jambo lililozoeleka, Kwanini?

SIJAWAHI kuona Rais akialikwa let's say ITV / TBC / Channel 10 kufanyiwa mahojiano kuhusu masuala yanayoendelea au jambo lolote kwa manufaa ya wananchi. Kama ishawahi kutokea basi ningependa kujuzwa kwanini imekuwa ni nadra kwa kiwango hicho?!

Je, ni sheria za nchi haziruhusu? Au ni utaratibu usiozoeleka na hivyo umeridhiwa uendelee hivyo hivyo tu? Kwanini iwe hapa kwetu tu na akienda nchi za nje afanyiwe Interview?

Nimeshashuhudia mara kwa mara Rais wa Kenya akihojiwa na vyombo vya habari vya huko mfano KTN (Sio ile Press Conf.), yaani namaanisha yale Mahojiano yaliyoratibiwa na Channel husika!

Juzi juzi nilimuona Mhe. Rais JK akiwa kwenye uzinduzi wa Kituo cha Azam TV International na kufanyiwa TEST INTERVIEW na Tido Mhando - Nilivutiwa sana na kujiuliza kwanini hili suala halifanyiki kabisa kiuhalisia na vyombo vyetu!?

Nimejaribu kuandika kwa kirefu ili nieleweke na kupata majibu ya kina kutoka kwenu wadau!

Nawasilisha kwenu nyote Wakuu wote wa JF tujadili, wakiwemo;

RUCCI Chachu Ombara Msamiati Pasco FaizaFoxy Watu8 figganigga Mag3 Donatila Mapengo 17 Yericko Nyerere Jestina et cetera et cetera...........
Hana cha kuongea anawaza safari tu
 
Back
Top Bottom