Kwanini Rais wa JMT hafanyiwi 'Interview' kwenye Media?

Kwanini Rais wa JMT hafanyiwi 'Interview' kwenye Media?

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
Habari ndugu zangu,

Kuna swali limekuwa likinitatiza kwa kipindi kirefu sasa. Mwanzoni nilidhani labda 'itifaki' haziruhusu kwa kiongozi wa juu wa nchi (Rais), kufanyiwa mahojiano na vyombo vya habari nchini, mfano Televisheni / Radio / Magazeti.. Lakini hili nimepingana nalo baada ya kuona akialikwa mara kwa mara nchi za ugenini na kuhojiwa kuhusu masuala mbalimbali na Media za huko.

Kwa mfano, Nishawahi kumsikia Mheshimiwa Rais akihojiwa mara kwa mara na vyombo vikubwa vya habari kama vile BBC, Deutsche Welle, na vinginevyo.. Lakini kwa vyombo vya habari vya hapa nyumbani si jambo lililozoeleka, Kwanini?

SIJAWAHI kuona Rais akialikwa let's say ITV / TBC / Channel 10 kufanyiwa mahojiano kuhusu masuala yanayoendelea au jambo lolote kwa manufaa ya wananchi. Kama ishawahi kutokea basi ningependa kujuzwa kwanini imekuwa ni nadra kwa kiwango hicho?!

Je, ni sheria za nchi haziruhusu? Au ni utaratibu usiozoeleka na hivyo umeridhiwa uendelee hivyo hivyo tu? Kwanini iwe hapa kwetu tu na akienda nchi za nje afanyiwe Interview?

Nimeshashuhudia mara kwa mara Rais wa Kenya akihojiwa na vyombo vya habari vya huko mfano KTN (Sio ile Press Conf.), yaani namaanisha yale Mahojiano yaliyoratibiwa na Channel husika!

Juzi juzi nilimuona Mhe. Rais JK akiwa kwenye uzinduzi wa Kituo cha Azam TV International na kufanyiwa TEST INTERVIEW na Tido Mhando - Nilivutiwa sana na kujiuliza kwanini hili suala halifanyiki kabisa kiuhalisia na vyombo vyetu!?

Nimejaribu kuandika kwa kirefu ili nieleweke na kupata majibu ya kina kutoka kwenu wadau!

Nawasilisha kwenu nyote Wakuu wote wa JF tujadili, wakiwemo;

RUCCI Chachu Ombara Msamiati Pasco FaizaFoxy Watu8 figganigga Mag3 Donatila Mapengo 17
 
Last edited by a moderator:
tatizo mkuu viongozi wengi hasa wa kiafrika tawala zao sio rafiki kwa watawaliwa na ndio maana wanaogopa kuitwa ktk vipindi kama hivo kwa kuhofia maswali yatakayoulizwa,mfano halisi si unaona hata kwenye chaguzi kuu za nchi ,viongozi wengi hasa wa kiafrika huwa wanaogopa midahalo kwa kuhofia kuulizwa maswali ambayo yatawafedhehesha
 
Hawana cha kujieleza mbele ya wananchi wenye hasira dhidi ya utawala wao uliojaa usanii.
 
Nani alitaka kuongea nae akakataliwa. Waandishi wengi waoga
 
rais anajikweza saana utafkr haendi choon anakunya kwa bruetooth wakati kla mwanadam ana mavi tumbon
 
Aliwahi kuhojiwa na Mtangazaji wa zamani wa BBC huko London mara baada ya kuingia Ofisi ya Rais. Mtihani ulikuwa mgumu na Watanzania wengi tuliona aibu kwa kweli maana majibu yake hayakuwa ya kiwango.

Hata hivyo mwaka jana mwishoni (kama sikosei) alipokuwa Uingereza tena alihojiwa na TV Station ya BBC alijitahidi kujieleza kuhusu juhudi zake katika kupambana na ujangili.
 
Alihojiwa na Amanpour wa CNN mwaka Jana February kuhusu biashara ya ndovu na ujangili ICHECK...amanpour.blogs.cnn.com/2014/2/13/tanzanias-blood-ivory-this-is-madness-now/ PIA CHECK Interview yake na ICCF mwaka 2013 @ www.youtube.com/watch?v=Hxp1EN-_NUY
 
Aisee... Mahojiano hayo siyo. Nazungumzia zile official interviews..! Kwamba anaalikwa kwenye kipindi, mfano DK 45 cha ITV, kisha anaulizwa maswali.
Nimewahi kumuona akihojiwa na mtangazaji ila sikumbuki kama ni TBC AU STAR TV
 
Huwa anahojiwa na waandishi wa habari vilaza kama Rweyemamu kule Magogoni!! Hii kurugenzi ya habari ya DHAIFU imejaa mediocrity kweli; embu nendeni mkasome kule kwenye blog ya Michuzi walivyoharibu kiingereza kwenye salaam za Dhaifu za rambi rambi kwenda kwa waziri mkuu wa Singapore!! Aibu tupu kwa ofisi kuu ya nchi!
 
tatizo mkuu viongozi wengi hasa wa kiafrika tawala zao sio rafiki kwa watawaliwa na ndio maana wanaogopa kuitwa ktk vipindi kama hivo kwa kuhofia maswali yatakayoulizwa,mfano halisi si unaona hata kwenye chaguzi kuu za nchi ,viongozi wengi hasa wa kiafrika huwa wanaogopa midahalo kwa kuhofia kuulizwa maswali ambayo yatawafedhehesha

kama ambavyo mh huyu wa sasa alivyokimbia mdahalo na dr Slaa badala yake akaletwa kinana mjadala ulikua star tv
 
Acheni utani jamani..huyu rais wenu huyu waje kumhoji CNN au BBC !? Eeeh labda wamhojo kwa kiswahili huku akiwa na madesa pembeni..
 
Raisi Kikwete akitoka nje ya nchi anaweza kufanya mahojiano(interview) na waandishi au vyombo vya habari vya kimataifa kama CNN n.k.

Lakini najiuliza ni lini Raisi Kikwete amewahi kuhojiwa TBC1,ITV,Star tv,Channel 10 n.k?

Au ni lini Raisi Kikwete amewahi kufanya mahojiano na waandishi mashuhuri wa nchi tangu aingie madarakani?

Au tatizo ni waandishi wenyewe kukosa ujasiri au kutokujiamini kufanya mahojiano na raisi?

Kama aliwahi,basi ni wakati anaingia madarakani.

Tutofautishe kuitisha "press conference" na kufanya mahojiano ya "ana kwa ana" na chombo cha habari au na mwandishi yoyote maarufu na mkongwe katika fani ya habari hasa kwenye kufanya interview na viongozi.

Charity begins at home.
 
Kwa kuwa ni mbongo anawajua wabongo vizuri wafukunyuku sana hawako straight kama hao wa CNN NA BBC
Mbongo mpe nafasi akuhoji maswali ndo utamjua.......
 
Back
Top Bottom