Acheni uongo kile kiingereza gani cha English course, kiingereza anachoongea kwa lafudhi ya kiswahili?Popote pale ulipo Rais wangu Mstaafu wa Awamu ya Nne Mzee Jakaya Mrisho Kikwete Shikamoo kwa Kuzungumza Kwako vizuri na kiufasaha kabisa Lugha ya Kiingereza jana ulipokuwa umealikwa.
Na ulichonifurahisha zaidi GENTAMYCINE ulikuwa unakiongea huku ukiwa hutetemeki, unajiamini na unatiririka nacho vizuri kama Mchezaji wako wa Yanga SC Tuisila Kisinda halafu na hata Kiingereza chenyewe nacho kinakupenda na kinakupendeza vile vile.
Kwa jinsi ninavyojijua GENTAMYCINE ndiyo ingekuwa Mimi jana pale ningechapia sana hiyo Lugha na kwa Kuzuga ningeishia tu Kuongea Kizanaki au Kimakuwa changu, Kukasirika ( Kufoka ) hovyo huku Komwe langu Kubwa likitokwa na Jasho na Kulazimisha nitumie Lugha ya Kiswahili hata kama 99% ya Wanaonisikiliza hawakijui na watatafsiriwa na Wenyeji au Wakalimani wao.